Huyo ni mjinga sana, na mwanaume wa namna hiyo hana akili ni tegemezi na hawezi kuwa na maendelea ktk maisha yake, huyo Jamaa mwenye hicho kichomi atafanikiwa,Ndugu yangu huyu ni mwaka na nusu sasa anadunda na mke wa mtu. Mwaka jana nikamshauri amwache mara moja,akakubali ila akaendelea kwa kificho.
Siku ya valentine day akampost kidogo whatsapp halafu akafuta. Ikabidi nimuweke kikao cha kishikaji na washkaji. Tukampa risala nzito,kumbe alivyotoka pale wakaenda chocho na yule mke wa mtu wakafanya tendo. Wakati wa tendo jamaa akamchana yule dada kwamba mimi namshauri amuache ila yeye hayuko tayari.
Kesho yake yule dada akatuma sms akaniambia kama naona ndugu yangu anafaidi basi na mimi anitafutie mke wa mtu. Sikumjibu...badae akaandika au nataka mimi ndio namtaka yule ndugu yangu.
Kitendo kile kiliniuma sana,nilidhalilika sana.
Mume wa yule dada alikuwa masomoni alikuwa akija mara moja moja. Ni jamaa niliwahi kufanya naye kazi. Sasa juzi kati nikakutana naye anatamba mke wake amemshauri arudi tena shule akachukue masters kabisa amalize kila kitu
Dadeki jamaa jinga sana. Lakini najiuliza wake za watu wana utamu gani?