Uko wapi Dk Wilbroad Slaa? Njoo ushuhudie anguko la Mafisadi

Uko wapi Dk Wilbroad Slaa? Njoo ushuhudie anguko la Mafisadi

maramia

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2015
Posts
2,029
Reaction score
1,345
Nitaendelea kuamini ktk maisha yangu yote kwamba, kwa Chadema kumpokea Edward Ngoway Lowassa, fisadi mkubwa aliyetimka kutoka CCM na kumtimua kishenzi katibu mkuu wao Dk Wilbroad Slaa, Chadema walifanya dhambi kubwa ambayo itawagharimu na wataijutia kwa zaidi ya miaka 50 ijayo.

Eti Lowassa aliyechukuliwa na Chadema kama fisadi namba moja ghafla aligeuka kuwa mfalme asiye na doa na Slaa aliyechukuliwa na Chadema kama malaika ghafla akageuka kuwa shetani na mchawi ktk chama hicho.

Kwa matokeo ya uchaguzi wa leo napenda kumwalika Dk Slaa akae mkao wa kula ashuhudie anguko la mafisadi waliomfukuzisha kutoka chama alichokipigania kufa na kupona kwa zaidi ya miaka 20.
 
dr slaa ndio tumani pekee lililokuwa limebaki
 
Mkuu hii inaitwa style ya kimya kimya....kama dodoma!!
 
halmashauri nyingi miji manispaa na majiji zitaendeshwa na ukawa-ccm haina nguvu kwenye base.najua kwa upeo wa mtoaa hoja uchaguzi kwake ni kutwaa uraisi lakini kwa wanamageuzi ni fursa ya kufanya maamuzi katika ugawaji raslimali Lowassa ametupa tulichotaka-Slaa haingii hata robo nadhani umeona CCM walivoingia gharama kubwa hovyooooooooooooo
 
Gia ya angani leo inazimiwa ardhini kwa kura ....Bring back our Dr Slaa ....
 
Nipo kwenye foleni karibia watu wote wanasema bila kufunga macho kura ni kwa lowassssssa kwa maana hiyo na lazima tuzilinde
 
Huyo Dr Slaa amepishana na uwaziri. Aendelee kutumia posho aliyopewa.
 
Acha ujinga boya wewe. Sio siku ya campaign leo. Tunaongelea upigaji wa kura tu hayo mengine ni propaganda zisizokuwa na maana.
 
Huyu "fisadi" Lowassa lazima tukamfunge jela ya miaka 10 pale ikulu magogoni...
 
Gia ya angani leo inazimiwa ardhini kwa kura ....Bring back our Dr Slaa ....

Mkuu sio kwamba imezimiwa ardhini. hii gia ya mbowe haina tofauti na ile iliyopigwa na rubani wa ndege ya malasya, mpaka leo ndege haijajulikana iliko. Mwisho wa chadema ni leo
 
Back
Top Bottom