Uko tayari kuoa au kuolewa lini?

Jpinduzi

Senior Member
Feb 26, 2011
136
68
Utasikia mwingine anasema, siku Mungu atakapo nipa mume au mke, hii ni hatari sana! Biblia inasema kwenye kile kitabu cha Mhubiri.3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.
Kila kitu kilichoko chini ya mbingu kimeratibiwa, kwa lugha nyingine, ni kwamba kila mwanadamu ana kalenda yake, iko kalenda yako ya kuzaliwa, na ipo kalenda ya matukio na mipango mbalimbali. Mungu anaijua. Mungu anatangaza mwisho tangu mwanzo, anajua mwisho wa maisha yako wakati wewe unapozaliwa.

Katika mwanzo wa maisha yako, Mungu anakuwa amekwishajua mwisho wako; utakavyokuwa; na kama amekwishajua mwisho wako, maana yake ameshatembea kwenye maisha yako yote toka mwanzo mpaka alipofika mwisho, na alipokamilisha maisha yako akarudi mwanzo ndipo akakuongoza kuzaliwa.

Mungu anapokuacha uzaliwe duniani, hakika ujue kabisa ya kwamba amekwisha tembea na wewe katika maisha yako, amesharatibu mambo yako na yako hatua kwa hatua; kwa mfano, kitu gani utafanya, wapi utasoma, utasoma nini, utaolewa na nani au utaoa nani na itakuwa, lini, maisha yako yatakuwaje, utamtumikiaje, mpaka mwisho wako. Akiishafika mwisho wa maisha yako anarudi mwanzo, akishafika mwanzo anatangaza mwisho tangu mwanzo; kwa hiyo kuanzia hapo unapozaliwa ujue maisha yako yote yamesharatibiwa!

Ni vizuri ufahamu hii mistari itakusaidia, maana inakujengea msingi mzuri wa maisha hapa. Isaya.46:9-10 inasema, “Kumbukeni mambo ya zamani za kale maana mimi ni Mungu wala hapana mwingine, mimi ni Mungu wala hapana aliye kama mimi. Nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado, nikisema, shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.

Kwa lugha nyingine anatuambia ya kwamba, ‘wewe unaona kila kitu ni kipya, unapoishi kila siku ni mpya, kila dakika inayokuja ni mpya, Mungu anasema hiyo safari unayopita, mimi nilikwishaipita tayari, nikafika mwisho wa maisha yako ndipo nikakuruhusu uzaliwe. Ulipokuwa unazaliwa nikatangaza mwisho wako tangu wakati unazaliwa.

Sasa mimi ninataka nikuambie kama Mungu anajua, na shauri lake anasema litasimama katika maisha yako, ili mapenzi yake ayatende katika maisha yako, unahitaji kuwa mwangalifu. Kwa sababu kuna mpango na saa ya Mungu ya kuoa au kuolewa, - ipo!
Mungu anapokuletea mawazo ya kuoa au kuolewa, ni kwa ajili yakuimarisha maisha yako na wito wako na kazi na makusudi, ambayo ameyaweka hapa duniani. Atakuletea mtu atakaye imarisha wito wako, atakuletea mtu atakaye saidiana na wewe, uwe ni mwanamke au uwe ni mwanaume.

Mungu anapo kukutanisha na mtu wa kuoana naye ni kwa ajili ya kuimarisha nguvu zenu ili mtimize kusudi la Mungu. Kwa hiyo lazima anajua kuna saa huyu mvulana anahitaji mke, au huyu msichana anahitaji mume! Lakini watu wengi sana hawalifuatilii hili. Wakati sisi tunaoana na mke wangu tulikuwa bado vijana, tulioana hatujafikisha hata miaka thelathini, ninakumbuka nilikuwa na miaka 28. Tulijaliwa kuwapata watoto tungali bado vijana sana. Lakini tuna watoto ambao ni wakubwa kwa sasa. Tumefika kipindi ambacho tunaweza tukafuatilia masuala ya utumishi kwa namna ambayo haiwaumizi watoto wetu sana!

Maana watoto wakiwa wadogo wote, mimi ninakuambia kumtumikia Mungu ni kunakuwa kugumu sana, usije ukafikiri ni kurahisi. Maana unahitaji kuwa karibu nao; wanahitaji kusoma shule, wanahitaji kufanya vitu mbalimbali, wanahitaji kuwa na baba karibu, wanahitaji kuwa na mama karibu. Saa nyingine mnataka kusafiri nao; unaweza ukasafiri nao lakini usije ukafikiri ni kitu kirahisi.
Tulisafiri na Joshua (mtoto wetu wa nne) akiwa na wiki sita. Sijawahi kuona watu wakisafiri na watoto wao wakiwa wadogo namna hiyo, Joshua alikwenda kwenye huduma akiwa na wiki sita tu. Hatukuwa na namna ambavyo tungeweza kumwacha. Sasa unaweza ukaelewa akiwa na wiki sita; maana yake mama yake ana muda wa wiki sita tu tangu ajifungue na tulisafiri kwa gari, sio kwa ndege, bali kwa gari!

Tulisafiri masaa karibu kumi na mbili, tumebeba kila kitu, tumebeba mpaka unga wa kutengenezea uji, na beseni la kuogea, na maji. Huwezi kumwogeshea mtoto mchanga wa wiki sita maji yoyote tu, kwa hiyo tulibeba maji ya kumwogeshea. Huwezi kwenda ‘spidi’ unayotaka, ikifika saa yake ya kula lazima usimame! Ukifika kwenye hoteli huwezi kumlaza jinsi unavyotaka, lazima uingie kwanza uombe, uangalie yale mashuka yaliyoko halafu uombe, uangalie kile kitanda halafu uombe, uangalie kila kitu kule ndani halafu uombe!

Wewe ni mtumishi wa Mungu, ukienda na mtoto kienyeji kienyeji tu, ibilisi anaweza akamvamia na ukapata shida, na huduma yako yote uliyoiendea ikaharibika. Unaweza ukatamani saa nyingine usinge- safiri naye. Lakini mnaposafiri pamoja, kumbuka ina gharama yake.

Lakini mambo haya unahitaji kufiri mapema, ili uweke kwenye agenda yako ya maombi ujue kabisa mpango wa Mungu ya kuwa unatakiwa kuoa au kuolewa lini. Ninajua kwa wengi kinakuwa kigumu hicho, maana wengine wametamani kuolewa jana, hawajapata wanaume, wengine wangetaka kuoa leo, lakini bado hawajapata msichana wa kuoa.
Wengine wanatamani kuolewa si kwa sababu mpango wa Mungu umefika wa kuolewa; ila ni kwa sababu wanaona muda wao wa kuolewa umefika, wengine wanaona umri umesogea. Mpango wa Mungu juu ya maisha yako, haubabaishwi na jinsi wewe unavyohesabu miaka,jirani zako wanavyohesabu miaka, ndugu zako wanavyohesabu miaka, au rafiki zako wanavyohesabu miaka.
Mungu anajua alichopanga kwa ajili yako, ana kalenda yako kabisa, na kila alichokichagua Mungu ndicho sahihi.(source-mwakasege)
 
- Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa
- Kuna wakati wa kuoa na wakati wa kuolewa
- Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka
- kuna wakati wa kupanda na wakati wa kushuka
 
Utasikia mwingine anasema, siku Mungu atakapo nipa mume au mke, hii ni hatari sana! Biblia inasema kwenye kile kitabu cha Mhubiri.3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.
Kila kitu kilichoko chini ya mbingu kimeratibiwa, kwa lugha nyingine, ni kwamba kila mwanadamu ana kalenda yake, iko kalenda yako ya kuzaliwa, na ipo kalenda ya matukio na mipango mbalimbali. Mungu anaijua. Mungu anatangaza mwisho tangu mwanzo, anajua mwisho wa maisha yako wakati wewe unapozaliwa.

Katika mwanzo wa maisha yako, Mungu anakuwa amekwishajua mwisho wako; utakavyokuwa; na kama amekwishajua mwisho wako, maana yake ameshatembea kwenye maisha yako yote toka mwanzo mpaka alipofika mwisho, na alipokamilisha maisha yako akarudi mwanzo ndipo akakuongoza kuzaliwa.

Mungu anapokuacha uzaliwe duniani, hakika ujue kabisa ya kwamba amekwisha tembea na wewe katika maisha yako, amesharatibu mambo yako na yako hatua kwa hatua; kwa mfano, kitu gani utafanya, wapi utasoma, utasoma nini, utaolewa na nani au utaoa nani na itakuwa, lini, maisha yako yatakuwaje, utamtumikiaje, mpaka mwisho wako. Akiishafika mwisho wa maisha yako anarudi mwanzo, akishafika mwanzo anatangaza mwisho tangu mwanzo; kwa hiyo kuanzia hapo unapozaliwa ujue maisha yako yote yamesharatibiwa!

Ni vizuri ufahamu hii mistari itakusaidia, maana inakujengea msingi mzuri wa maisha hapa. Isaya.46:9-10 inasema, “Kumbukeni mambo ya zamani za kale maana mimi ni Mungu wala hapana mwingine, mimi ni Mungu wala hapana aliye kama mimi. Nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado, nikisema, shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.

Kwa lugha nyingine anatuambia ya kwamba, ‘wewe unaona kila kitu ni kipya, unapoishi kila siku ni mpya, kila dakika inayokuja ni mpya, Mungu anasema hiyo safari unayopita, mimi nilikwishaipita tayari, nikafika mwisho wa maisha yako ndipo nikakuruhusu uzaliwe. Ulipokuwa unazaliwa nikatangaza mwisho wako tangu wakati unazaliwa.

Sasa mimi ninataka nikuambie kama Mungu anajua, na shauri lake anasema litasimama katika maisha yako, ili mapenzi yake ayatende katika maisha yako, unahitaji kuwa mwangalifu. Kwa sababu kuna mpango na saa ya Mungu ya kuoa au kuolewa, - ipo!
Mungu anapokuletea mawazo ya kuoa au kuolewa, ni kwa ajili yakuimarisha maisha yako na wito wako na kazi na makusudi, ambayo ameyaweka hapa duniani. Atakuletea mtu atakaye imarisha wito wako, atakuletea mtu atakaye saidiana na wewe, uwe ni mwanamke au uwe ni mwanaume.

Mungu anapo kukutanisha na mtu wa kuoana naye ni kwa ajili ya kuimarisha nguvu zenu ili mtimize kusudi la Mungu. Kwa hiyo lazima anajua kuna saa huyu mvulana anahitaji mke, au huyu msichana anahitaji mume! Lakini watu wengi sana hawalifuatilii hili. Wakati sisi tunaoana na mke wangu tulikuwa bado vijana, tulioana hatujafikisha hata miaka thelathini, ninakumbuka nilikuwa na miaka 28. Tulijaliwa kuwapata watoto tungali bado vijana sana. Lakini tuna watoto ambao ni wakubwa kwa sasa. Tumefika kipindi ambacho tunaweza tukafuatilia masuala ya utumishi kwa namna ambayo haiwaumizi watoto wetu sana!

Maana watoto wakiwa wadogo wote, mimi ninakuambia kumtumikia Mungu ni kunakuwa kugumu sana, usije ukafikiri ni kurahisi. Maana unahitaji kuwa karibu nao; wanahitaji kusoma shule, wanahitaji kufanya vitu mbalimbali, wanahitaji kuwa na baba karibu, wanahitaji kuwa na mama karibu. Saa nyingine mnataka kusafiri nao; unaweza ukasafiri nao lakini usije ukafikiri ni kitu kirahisi.
Tulisafiri na Joshua (mtoto wetu wa nne) akiwa na wiki sita. Sijawahi kuona watu wakisafiri na watoto wao wakiwa wadogo namna hiyo, Joshua alikwenda kwenye huduma akiwa na wiki sita tu. Hatukuwa na namna ambavyo tungeweza kumwacha. Sasa unaweza ukaelewa akiwa na wiki sita; maana yake mama yake ana muda wa wiki sita tu tangu ajifungue na tulisafiri kwa gari, sio kwa ndege, bali kwa gari!

Tulisafiri masaa karibu kumi na mbili, tumebeba kila kitu, tumebeba mpaka unga wa kutengenezea uji, na beseni la kuogea, na maji. Huwezi kumwogeshea mtoto mchanga wa wiki sita maji yoyote tu, kwa hiyo tulibeba maji ya kumwogeshea. Huwezi kwenda ‘spidi’ unayotaka, ikifika saa yake ya kula lazima usimame! Ukifika kwenye hoteli huwezi kumlaza jinsi unavyotaka, lazima uingie kwanza uombe, uangalie yale mashuka yaliyoko halafu uombe, uangalie kile kitanda halafu uombe, uangalie kila kitu kule ndani halafu uombe!

Wewe ni mtumishi wa Mungu, ukienda na mtoto kienyeji kienyeji tu, ibilisi anaweza akamvamia na ukapata shida, na huduma yako yote uliyoiendea ikaharibika. Unaweza ukatamani saa nyingine usinge- safiri naye. Lakini mnaposafiri pamoja, kumbuka ina gharama yake.

Lakini mambo haya unahitaji kufiri mapema, ili uweke kwenye agenda yako ya maombi ujue kabisa mpango wa Mungu ya kuwa unatakiwa kuoa au kuolewa lini. Ninajua kwa wengi kinakuwa kigumu hicho, maana wengine wametamani kuolewa jana, hawajapata wanaume, wengine wangetaka kuoa leo, lakini bado hawajapata msichana wa kuoa.
Wengine wanatamani kuolewa si kwa sababu mpango wa Mungu umefika wa kuolewa; ila ni kwa sababu wanaona muda wao wa kuolewa umefika, wengine wanaona umri umesogea. Mpango wa Mungu juu ya maisha yako, haubabaishwi na jinsi wewe unavyohesabu miaka,jirani zako wanavyohesabu miaka, ndugu zako wanavyohesabu miaka, au rafiki zako wanavyohesabu miaka.
Mungu anajua alichopanga kwa ajili yako, ana kalenda yako kabisa, na kila alichokichagua Mungu ndicho sahihi.(source-mwakasege)

Ni ujumbe mzuri.
 
- Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa
- Kuna wakati wa kuoa na wakati wa kuolewa
- Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka
- kuna wakati wa kupanda na wakati wa kushuka

Hili neno "Mhubiri 3:1-8" lilitolewa wakati wa msiba wa mdogo wangu, ninapolisoma hapa namkumbuka sana, i wish she could be alive!!!
God rest her soul in peace.
 
Hili neno "Mhubiri 3:1-8" lilitolewa wakati wa msiba wa mdogo wangu, ninapolisoma hapa namkumbuka sana, i wish she could be alive!!!
God rest her soul in peace.

Pole Evarm,stay strong and courageous
 
Hili neno "Mhubiri 3:1-8" lilitolewa wakati wa msiba wa mdogo wangu, ninapolisoma hapa namkumbuka sana, i wish she could be alive!!!
God rest her soul in peace.

Pole sana mpendwa na mipango ya Mungu hiyo!
 
Last edited by a moderator:
Asante Jp kwa kutukumbusha na kutupa wimbo mzuri wa marehemu Sedekia Mungu ampumzishe kwa amani....ubarikiwe sana.
 
Kama anajua kila jambo na amepanga nilifanye ukifika wakati nitaoa no matter what!Ukiona nakataa kuoa leo jua wakati haujafika,ukifika sitakua na uwezo wa kuyapinga yalixmangwa na Mungu!
 
Back
Top Bottom