tang'ana
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 11,809
- 15,059
Jana kuna msala niliufanya barabarani, nikakamatwa na traffic, wakanipeleka kituoni, sasa wakati wanajiandaa kuniingiza lock up wakaniambia nivue viatu vyangu, nitoe na vyote nilivyo navyo mfukoni, mimi nikatii nikatoa vitu vyangu ikiwemo kadi yangu ya CCM, yule afande aliyekuwa pale counter akaiona akaichukua akaingalia akaniambia nikae pembeni kwanza, baadae nikasikia anaongea na mkubwa wake kwenye simu, kwa maelezo niliyoyasikia mkubwa wake alimwambia aniachie haraka sana nisije kumsababishia matatizo.
Basi, me nikarudishiwa vitu vyangu nikaambiwa niendelee na shughuli zangu.
Basi, me nikarudishiwa vitu vyangu nikaambiwa niendelee na shughuli zangu.