We ungeridhika na kuonyesha adabu kwa mumeo(mdada wa kizungu mwenye pesa yake) hata usingeamua kuachika,,
Ulikuwa umeolewa usijibaraguze hapa,,
kuolewa si lelemama maana yake uwe mtiifu kwa aliyekuoa,
unawasakama wadada wa tz ilhali we mwenyewe maisha ya kuolewa yalikushinda
Dada. Ngoja nikupe story yote labda ndio utanielewa.
First of all, mimi ni mtu na hela yangu pia. Tulikuwa tunaendesha magari yangu, na kuishi kwa nyumba yangu. Wakati najenga lodges za tours. Ila spending money ilikuwa ni yeye anatoa, after all, hizo vacations zote tulienda ilikuwa ni ideas zake. Kuna appliances pia nilinunua mimi alivyokuja tanzania. Nilinunua washing machine, dryer, electric oven, etc ili kufanya maisha yake yawe rahisi akiwa Tz. Kwa hio nilichangia sana sana. Na sio kuwa yeye tu ndio alikuwa anachangia kifedha. Lakini tatizo ikawa maamuzi yote kama tunakula nini, tunaenda wapi, tunafanya nini, nk ni yeye tu vile anataka na si vinginevyo. Wazungu wanasema, "it was her way, or the highway". Ni atakavyo yeye, ama sivyo nipite hivi. Hadi ananikataza nikitaka kwenda site mara nyingine. Ila kweli kwa kitandani, muda wowote nikitaka, ananipa. Tena anasema baby mwili wangu umeumbwa kwa ajili yako, nifanye utakavyo na nitakupa kila kitu upate raha zote. Ila mwisho wa siku her controlling ways zikafanya nikaamua kupita hivi. Unavyoona hivyo ni sawa alivyofanya? Mimi sikutaka kum-control mtu. Ila pia sikutaka kuwa controlled namna hio. Mahusiano ni maelewano. After all, nilichangia sehemu kubwa sana kifedha pia.
Nilichokuwa naongelea ni kwamba wadada Tz, asilimia kubwa hata upambanaji katika biashara hamna. Na ukifunguliwa biashara mnaziua tu. Afadhali hata huyo mzungu, tungefungua biashara angechangia sana, kimawazo, kwa nguvu zake, na capital pia. Tatizo lake ndio lilikuwa hilo kwamba hakutaka kunipatia nafasi ktk mahusiano. Kwangu that defect of hers was a major issue indeed.
Nyie wadada Tz. Tunawapenda lakini mbadilike. Mie sitaki hela ya mtu, lakini nikiwa nawe, nataka uchangie hata kimawazo. Pisi kali za bongo hapo ndio mnashindwa kabisa.
Ps: Pia jitahidi usijibu kwa dharau. Hapa tuna elimishana. Hakuna sababu ya kubezana. Na kwa taarifa yako niliumia sana mimi na yeye tulivyoachana. Nilikataa kwenda kwao new zealand, alishaweka mambo sawa niende huko. Nikakataa. Nikaona kama huku tz kwetu ananifanyia hivyo, huko kwao je? Pia teari mimi na permanent residence USA, na nikiwa huko marekani ndio nilikutana naye. Ni mtu anapenda adventures, akasema atapenda kuja tz kuishi na mimi sababu nilishamwambia sina plans sana za kuishi USA. Akaja Tz tukaishi pamoja, ila ndio pakamshinda. Tz palimshinda sababu ya mbu alikuwa akiumwa na mmoja tu anavimba mwili. Yeye ni raia wa nchi mbili za USA na New zealand (Dual citizenship). Sababu alikuwa hapendi sana USA, na Tz palivyomshinda, na sababu Alipenda new zealand zaidi, na familia yake ilikuwa na branch huko New zealand ya kampuni yao, basi ndio akataka tuhamie New zealand.
Kwenda Nz kwangu ikawa issue. Nikaona tz, USA, na New zealand = nchi tatu and that was just too much. Nilishaanza wekeza USA na Tz, sikuwa teari kuhamia nchi nyingine for a woman. Kwa hio nikaone huyu atanipoteza kimaisha na direction-wise. Hapo ndio tukashindwana. Miezi michache baadae, akawa amepata mzungu wakaja kuoana 2 years later. LAKINI SASA HIVI NIKIANGALIA ULIKUWA UAMUZI SAHIHI KABISA. NIMEFANYA MAMBO MAKUBWA AMBAYO NAJUA NINGEKUWA NAYE NISINGEFANYA. YEYE ALIKUWA MTU WA KULA BATA TU. NA MIMI NI MTU WA KUWEKEZA (KU-INVEST). Tena hata hela yangu binafsi alishaanza kui-control. Nikaanza kukosa uhuru wa kuiwekeza nk. Uhuru huo umenisaidia sana. Na nimefanya mambo makubwa. Na sasa nina mali zangu binafsi, ambazo siingiliwi na mtu. That is an amazing feeling.