kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,686
HAKUNA anayeweza kubisha kwamba maisha bila kujishughulisha ni magumu sana. Wakati mwingine wapo ambao wanautengeneza ugumu kwa kutopenda kujishughulisha. Wao ni tegemezi kwa kila kitu, yaani bila watu wengine maisha yao hayajakamilika, hili ni tatizo kubwa katika jamii yetu.
Maisha ni kufanya kazi, tena kwa bidii. Wengi walioweka hiyo kama kanuni ya maisha yao wamefanikiwa. Lakini katika suala la kazi kuna zile za kujiajiri na za kuajiriwa. Ninachotaka kukizungumzia leo kinawahusu wale ambao wameajiriwa na wana malengo ya kuwa na maisha yaliyotawaliwa na mafanikio.
Mjasiriamali mmoja maarufu nchini aliwahi kuniambia kwamba, hata siku moja mshahara hauwezi kunitosha. Akaniambia naweza kuwa nalipwa mshahara mnono lakini nikiutegemea huo na nikahisi unaweza kuniwezesha kufanya mambo makubwa katika maisha yangu, lazima nitakwama.
Lakini akaenda mbele zaidi kwa kuniambia kwamba, wengi waliofanikiwa katika maisha yao siyo watu waliokuwa wakitegemea chanzo kimoja cha mapato, walianzisha vyanzo vingi, wakavisimamia kwa umakini mkubwa na leo hii wako kwenye ramani ya watu wenye mafanikio makubwa.
Ukifuatilia utabaini ni kweli kabisa. Waangalie watu kama Said Salim Bakhresa, Reginald Abraham Mengi na wengineo ambao ni mabilionea. Hawa wana mafanikio makubwa lakini wamefika hapo walipo leo kwa kuanzisha vyanzo mbalimbali ya mapato.
Kutokana na ukweli huo, ni vizuri sasa na wewe ukaanza kufikiria chanzo kingine cha mapato ukiachilia mbali mshahara wako unaoupata kila mwezi. Kumbuka kuna mahitaji mengi ya msingi ambayo ukiangalia na gharama za maisha zilivyopanda, unaweza kukuta kila unapochukua mshahara unaishia kwenye kula, kuvaa na kusomesha watoto tu.
Sasa jiulize, furaha yako itakuwa imetimia kwa kufanikiwa kujitimizia mahitaji hayo tu? Huna malengo mengine ambayo ungetamani kuyatimiza yanayohitaji fedha? Naamini yapo na huenda changamoto unayokumbana nayo ni wapi kwa kupata fedha za ziada za kufanya mambo mengine ya muhimu.
Ndiyo maana nasema licha ya kwamba unafanya kazi lakini jitahidi sana kuwa na kijimradi ambacho kinaweza kukuingizia vijisenti ambavyo ukichanganya na mshahara, unaweza ukafanya mambo yakaonekana.
Angalia ni kipi unachoweza kukifanya?
Kikubwa ni kuhakikisha unajiwekea malengo kwamba kutoka kwenye mshahara wako unasevu pesa ambayo baada ya muda itakufanya upate mtaji wa kuanzisha biashara nyingine.
Biashara hiyo inaweza kuwa ya genge, duka, saluni, ufugaji wa kuku au nyingine utakayoona inafaa.
Maisha ni kufanya kazi, tena kwa bidii. Wengi walioweka hiyo kama kanuni ya maisha yao wamefanikiwa. Lakini katika suala la kazi kuna zile za kujiajiri na za kuajiriwa. Ninachotaka kukizungumzia leo kinawahusu wale ambao wameajiriwa na wana malengo ya kuwa na maisha yaliyotawaliwa na mafanikio.
Mjasiriamali mmoja maarufu nchini aliwahi kuniambia kwamba, hata siku moja mshahara hauwezi kunitosha. Akaniambia naweza kuwa nalipwa mshahara mnono lakini nikiutegemea huo na nikahisi unaweza kuniwezesha kufanya mambo makubwa katika maisha yangu, lazima nitakwama.
Lakini akaenda mbele zaidi kwa kuniambia kwamba, wengi waliofanikiwa katika maisha yao siyo watu waliokuwa wakitegemea chanzo kimoja cha mapato, walianzisha vyanzo vingi, wakavisimamia kwa umakini mkubwa na leo hii wako kwenye ramani ya watu wenye mafanikio makubwa.
Ukifuatilia utabaini ni kweli kabisa. Waangalie watu kama Said Salim Bakhresa, Reginald Abraham Mengi na wengineo ambao ni mabilionea. Hawa wana mafanikio makubwa lakini wamefika hapo walipo leo kwa kuanzisha vyanzo mbalimbali ya mapato.
Kutokana na ukweli huo, ni vizuri sasa na wewe ukaanza kufikiria chanzo kingine cha mapato ukiachilia mbali mshahara wako unaoupata kila mwezi. Kumbuka kuna mahitaji mengi ya msingi ambayo ukiangalia na gharama za maisha zilivyopanda, unaweza kukuta kila unapochukua mshahara unaishia kwenye kula, kuvaa na kusomesha watoto tu.
Sasa jiulize, furaha yako itakuwa imetimia kwa kufanikiwa kujitimizia mahitaji hayo tu? Huna malengo mengine ambayo ungetamani kuyatimiza yanayohitaji fedha? Naamini yapo na huenda changamoto unayokumbana nayo ni wapi kwa kupata fedha za ziada za kufanya mambo mengine ya muhimu.
Ndiyo maana nasema licha ya kwamba unafanya kazi lakini jitahidi sana kuwa na kijimradi ambacho kinaweza kukuingizia vijisenti ambavyo ukichanganya na mshahara, unaweza ukafanya mambo yakaonekana.
Angalia ni kipi unachoweza kukifanya?
Kikubwa ni kuhakikisha unajiwekea malengo kwamba kutoka kwenye mshahara wako unasevu pesa ambayo baada ya muda itakufanya upate mtaji wa kuanzisha biashara nyingine.
Biashara hiyo inaweza kuwa ya genge, duka, saluni, ufugaji wa kuku au nyingine utakayoona inafaa.