Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Mie jamani huyu shoga yangu wala simwelewi. Mwanzoni mwa mwezi ulopita, alikuja kunazima vidani vyangu vya dhahabu ili kuhudhuria pamvu ya dada yake. Siku kadhaa baadae akaja kunambia kwamba, vidani vyangu vimepotea, lakini akaahidi kunilipa. Sasa naona karibu mwezi wesha, mwenzangu kimya! Juzi nimemkumbusha, imekuwa nongwa. Anapita kila mtaa kuntangaza ubaya.
Jamani wenzangu hebu nambieni, ubaya wangu uwapi? Yaani kudai changu ndiyo niwe mbaya! Vidani vyangu, mwenyewe nimepewa na bibi yangu Al Marhum Bi Kijakazi, leo hii huyu hayawani asiye na haya anletea za kuleta! Mwenyewe nilikuwa na mtoko weekend hii na nilitaka nikaoshee huko kwenye mtoko, lakini huyu majununi ananipa majibu ya kifedhuli. Ama kweli, wafadhilaka wapundaka, heri kumfadhili mbuzi, kuliko binadamu mwenye maudhi!
Eti wana JF wenzangu, nimfanye nini huyu baradhuli?
Jamani wenzangu hebu nambieni, ubaya wangu uwapi? Yaani kudai changu ndiyo niwe mbaya! Vidani vyangu, mwenyewe nimepewa na bibi yangu Al Marhum Bi Kijakazi, leo hii huyu hayawani asiye na haya anletea za kuleta! Mwenyewe nilikuwa na mtoko weekend hii na nilitaka nikaoshee huko kwenye mtoko, lakini huyu majununi ananipa majibu ya kifedhuli. Ama kweli, wafadhilaka wapundaka, heri kumfadhili mbuzi, kuliko binadamu mwenye maudhi!
Eti wana JF wenzangu, nimfanye nini huyu baradhuli?