Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 15,848
- 20,697
UKISTAAJABU ya Musa utayashuhudia ya Firauni, utamaduni wa watu wa magharibi mwa Uganda ni wa ajabu sana.
Wakazi wa kijiji cha Nakapyata, wilayani Buyende nchini Uganda wamefanya sherehe ambapo watoto wawili wenye umri wa miaka tisa na sita waliozwa.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari nchini Uganda, mvulana mwenye umri wa miaka tisa ambaye anasoma darasa la nne katika shule ya msingi ya Buyende na msichana mwenye miaka sita ambao wote waliripotiwa kuzaliwa wakiwa na meno mawili waliozwa siku ya Jumatatu na kupatiwa nyumba ya kitamaduni ili waishi pamoja.
Chini ya Sheria za Uganda, ni makosa kwa watu walio chini ya umri wa miaka 18 kufunga ndoa ama hata kushiriki katika tendo la ngono. Serikali inaendelea kuchunguza utamaduni huo ambao unakiuka sheria za mtoto.
Inadaiwa watoto hao wawili walianza kuchumbiana wakati mvulana alipokuwa na umri wa miaka mitatu na msichana akiwa na umri wa miezi mitatu pekee. Hatua hiyo baadaye iliimarisha uhusiano kati ya familia zote mbili, huku Delifazi Mulame baba wa mvulana akimuita msichana huyo kama ‘mke wa mwanangu’. “Mwanangu alizaliwa na meno mawili na mkewe akazaliwa na meno mawili.
Kuzaliwa kwake kulileta baraka nyingi na jina lake linapaswa kuwaunganisha watu wa makabila ya Baganda na Basoga,” alisema Mulame.