Mtatunga kila aina ya mifano mwaka huu.
Mtatunga kila aina ya mifano mwaka huu.
Book 7 at work. Mlipumzika na sasa mmerudi kwa ari mpya na kasi mpya kuleta propaganda JF. Niliishawaambia nendeni mkawaambie wananchi mmtekeleza vipi ilani yenu ya uchaguzi badala ya kushinda kwenye mitandao mkipiga propaganda ambazo ki ukweli haziwasaidii.
Zitto aliishatoswa tayari, tafuta lingine la kuzumgumzia.
Tiba
Tatizo la Mbowe hana elimu lakini anakumbatia madaraka makubwa
mbowe akikuona kiti chake unakiviza anakuita MHAINI,maana halisi ya mhaini ni mtu anayetaka kupindua DOLA sasa chama chetu CDM kimekua lini DOLA?
Kwa muda mrefu nilikuwa najaribu kuutafakari mgogoro uliopelekea vita nchini Sudan ya kusini na kupelekea watu zaidi ya 1200 kufa na mamia kwa maelfu kuyahama makazi na kupata shida ikiwa ni magonjwa ya milipuko na njaa kwa watotot na akina mama.
Nimejaribu kufikiria nini chanzo cha yote hayo nchini s.sudan na watu kufariki wasio na hatia nikagundua kuwa chanzo cha yote hayo ni HOFU , WASIWASI NA KUTOJIAMINI kwa Kiongozi wa nchi hiyo SALVA KIIe wa rais.
Huyu jamaa hajiamini na kumuhofia makamu wake wa rais na kuja na visingizio kuwa ana mpango wa kumpindua kumbe ni woga na kutokana na kujua kwamba makamu huyo wa rais anayajua madudu mengi sana ya salva kiir akaona ni vyema am "fix" mapema pasi kujua kuwa makamu huyo wa rais ana ushawishi mkubwa sana kwa wananchi na pia katika jeshi.
Baada ya kumtimua kazi kwa kisingizio cha UASI leo ndo tunaona madhara makubwa yanayoendelea kutokea s.sudan na yeye mwenyewe anahaha namna ya kuutatua mgogoro huo..kwa kuwa amelikoroga HANA BUDI KULINYWA.
kama viongozi wa chadema wangekuwa na akili timamu wangeweza kujifunza kupitia suala la sudani ya kusini na madhara yanayoendela kujitokeza hivi sasa ambayo yanagharimu maisha ya raia wasio na hatia.
FREEMAN MBOWE hana tofauti kabisa na salva kiir rais wa s.sudan kwan kwa WOGA WAKE, KUTOJIAMINI KWAKE NA WASIWASI WAKE anamuogopa na kumuhofia sana kijana mdogo ZITTO ZUBER KABWE na kufanya kama alivofanya SALVA KIIR wa s.sudan kwa kumsingizia UASI na USALITI ili wam "fix" kama alivyofixiwa makamu wa rais wa s.sudan
MY TAKE:kama chadema na freeman mbowe mtaendelea na mpango dhaifu wa kumfukuza ZZK hakika chama chenu hakiwezi kukwepa ya sudan kusin kwa namna yoyote.
Wenye akili timamu watanielewa vizuri sana lakini misukule haiwezi kunielewa hata kidogo zaidi ya kuja na matusi na kashfa pasipo kusoma vizuri na kuelewa na kutafakari ki great thinker.
..... wenye akili timamu watanielewa vizuri sana lakini misukule haiwezi kunielewa hata kidogo zaidi ya kuja na matusi na kashfa pasipo kusoma vizuri na kuelewa na kutafakari ki great thinker. lakini hata ivo nawakaribisha wote MISUKULE na GREAT THINKERS tujadili.
SIJUI ......
Hivi CHADEMA imefikia hatua hiyo ya kuongoza nchi!!! SIJUI..... Serikali iliyoko madarakani inafanya nini? kweli ni dhaifu kiasi hicho? Kuna haja gani ya kusoma na kutafakari kama wewe ni GT na unayaona haya yanaweza kutokea kwanini usiyaseme bayana ili na sisi MISUKULE tuweze tujua mapema kabla hayajatufika maana sisi uwezo wa kufikiri ni mdogo na kama huwezi kusema bayana basi wewe ni MSUKULE na utetezi wako kwa ZZK hauna maana ni mapenzi yako binafsi..
Sure Mkuu. Hiki chama kikifa nitawahurumia sana akina Yeriko Nyerere na Ben Saanane
Mtatunga kila aina ya mifano mwaka huu.
Inahitaji uwe MSUKULE kweli kweli kuamini eti CHADEMA watashinda Uchaguzi 2015.Wakati akina Kinana wako busy kuimarisha mitandao hai ya Chama chao katika ngazi za chini kabisa,Kwa mfano hivi sasa wameanzisha VICOBA lengo likiwa kukamata kada zote za Watanzania wawe wapiga kura wao.Tujiulize CHADEMA ya Mbowe wanafanya nini kuimarisha mitandao yao ya Wapiga kura zaidi ya Makao Makuu kuzitafuna fedha huko bila ya kuwakumbuka wale wa chini.Uongozi huu una madhaifu mengi mno.Kwanza Uongozi wake hauna uwakilishi mzuri wa Watanzania wa kutoka makundi yote ya kijamii.Uongozi wa Kitaifa unaundwa kwa asilimia kubwa na watu wa dini moja na wa kanda moja.Hii ni kasoro kubwa itakayoinyima Chadema ushindi 2015 na ni kasoro ambayo Uongozi wa Mbowe umeonekana kupuuzia na hawataki kabisa kulifanyia kazi labda Mbowe hataki Chadema iingie Ikulu.
What's your point? Kwahiyo zzk abaki chadema hata kama Ñî msaliti, mhujumu na mamluk ili kukwepa ya Sudan ya kusini?
Wangapi wamefukuzwa/ kuvuliwa uanachama kwenye vyama vyao bila kutokea ya sudani ya kusini. WAPO akina mansoor himid, Maalim serif na engine wengi.
Jamaa hakawii kuja na press release ya kumsafisha huyu Mbowe mmwagaji damu kwa jina la Demokrasia.