Wahenga walisema UKISTAAJABU ya Mussa UTAYAONA ya FIrauni. KUMBE Huko Kuona ni zaidi ya kustaajabu maana ni sawa UPUMBAVU wa kuabudu Wachungaji. Sijui kama naeleweka?
Nikumbushe miaka ile ya uongozi wa JK, Chama cha Mapunduzi kilikuwa hatarini yaani kimekwisha kabisa katika ushawishi. Chama hakina sera wala mvuto ilikuwa swala la muda tu. Yaani ilikuwa aibu mtu kujinasibu na Chama na kila mtu alitegemea kuwa huo ndio mwisho wa Utawala wake. Hilo lilikuwa wazi kabisa isipokuwa kwa mbinu za dola.
Wapinzani nao wakaunda nguvu moja ya UKAWA kupambana na dola lakini kama wahenga wasemavyo. Katika Msafara wa Mamba, Kenge nao wamo! Dola ni zaidi ya Chama kimoja ni mtandao mkubwa unaohusu vyombo vyote vya serikali wao hawakuliona hilo.
Nilisema hapa kabla ya Uchaguzi mkuu kuwa Chadema wamefanya kosa kubwa sana kuchanganya nguvu na mahasimu wao, hoja hiyo ilipingwa kwa nguvu kubwa sana na wale wasojua tofauti ya Mamba na Kenge! Kwa sababu kwao hoja kubwa ilikuwa kufika penye maji mengi wakinadi - Mpaka kieleweke!
Nukuu zipo humu humu. Matokeo ya uchaguzi yalipitoka - Upinzani chali, ilikuwaje, Tukaanza kujiuliza funguo za gari kapewa nani?
Chuma akamamata nchi kinyume cha mategemeo ya wengi, hasira zote zikamgeukia Magufuli nsiye hasomu wao, wakati CCM jua linawawakia chama kikarudi kupata nuru! Leo hii imebakia hadithi hadithi..
Nasema hivi kama sio Magufuli kujitoa mhanga kwa chama hiki kuchukua Uongozi kuogmbea Urais mwaka 2015, hiki chama kilikuwa kimekufa kabisa! Ati leo hii kuna watu wanadiriki kabisa kujivunia Chama ilihali wakimnanga Mwendazake! Hawa ndio wale waitwao mitume wa uongo!
Kuna jamii sasa hivi wanaabudu Wachungaji kwa ilani za Utajiri. Hawa watu ni Wapumbavu kwa Marefu na Mapana na katu hutaweza waongoa katika imani zao hata kama wanapotea. Tatizo lake moja tu, Sii rahisi kujua tofauti yetu sisi sote..
Nikumbushe miaka ile ya uongozi wa JK, Chama cha Mapunduzi kilikuwa hatarini yaani kimekwisha kabisa katika ushawishi. Chama hakina sera wala mvuto ilikuwa swala la muda tu. Yaani ilikuwa aibu mtu kujinasibu na Chama na kila mtu alitegemea kuwa huo ndio mwisho wa Utawala wake. Hilo lilikuwa wazi kabisa isipokuwa kwa mbinu za dola.
Wapinzani nao wakaunda nguvu moja ya UKAWA kupambana na dola lakini kama wahenga wasemavyo. Katika Msafara wa Mamba, Kenge nao wamo! Dola ni zaidi ya Chama kimoja ni mtandao mkubwa unaohusu vyombo vyote vya serikali wao hawakuliona hilo.
Nilisema hapa kabla ya Uchaguzi mkuu kuwa Chadema wamefanya kosa kubwa sana kuchanganya nguvu na mahasimu wao, hoja hiyo ilipingwa kwa nguvu kubwa sana na wale wasojua tofauti ya Mamba na Kenge! Kwa sababu kwao hoja kubwa ilikuwa kufika penye maji mengi wakinadi - Mpaka kieleweke!
Nukuu zipo humu humu. Matokeo ya uchaguzi yalipitoka - Upinzani chali, ilikuwaje, Tukaanza kujiuliza funguo za gari kapewa nani?
Chuma akamamata nchi kinyume cha mategemeo ya wengi, hasira zote zikamgeukia Magufuli nsiye hasomu wao, wakati CCM jua linawawakia chama kikarudi kupata nuru! Leo hii imebakia hadithi hadithi..
Nasema hivi kama sio Magufuli kujitoa mhanga kwa chama hiki kuchukua Uongozi kuogmbea Urais mwaka 2015, hiki chama kilikuwa kimekufa kabisa! Ati leo hii kuna watu wanadiriki kabisa kujivunia Chama ilihali wakimnanga Mwendazake! Hawa ndio wale waitwao mitume wa uongo!
Kuna jamii sasa hivi wanaabudu Wachungaji kwa ilani za Utajiri. Hawa watu ni Wapumbavu kwa Marefu na Mapana na katu hutaweza waongoa katika imani zao hata kama wanapotea. Tatizo lake moja tu, Sii rahisi kujua tofauti yetu sisi sote..