Source:Habari Leo,March 02, 2008http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?id=7381Mkuu huyo wa Mkoa amemwambia Makamu huyo wa Rais kuwa Mara kuna utajiri mkubwa wa madini aina ya dhahabu katika vijiji 19 vya Wilaya ya Musoma Vijijini, vijiji 7 vya Wilaya ya Serengeti na pia katika vijiji 11 vilivyopo wilayani Tarime, huku Wilaya ya Rorya kunafanyika utafiti ambako kuna dalili za kuwapo dhahabu.
Machibya alieleza kuwa madini ya dhahabu yamepata wawekezaji katika migodi ya Norh Mara ambako kuna kampuni ya uchimbaji ya Barrick Tanzania ambayo kwa mwaka jana ilizalisha kilo 10,052,488, zenye thamani ya dola za Marekani 163,938,056 na kwamba Serikali ilipata mrahaba wa dola 4,956,753.28. Huku ikichangia huduma za jamii dola 353,000.
Hayo maandishi niliyo yawekea rangi,yanaonyesha jinsi tulivyologwa(?)Kampuni ya madini inapata $163bn, serikali inaambulia $4ml na eti huduma za jamii za thamani ya $300elfu. Hapo mkuu wa mkoa anaona tumefaidi, kumbe ni zero kabisa. Jamani wana JF hii imekaakaaje lakini. Tuko makini na raslimali zetu!!!!