Ukiona una hivi vitabia ujue una element za "uchawi"

Ukiona una hivi vitabia ujue una element za "uchawi"

Kingmairo

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2012
Posts
4,936
Reaction score
3,548
Ukiona una hivi vijitabia au alama ujue una element za kichawi chawi, na utakuwa mtu wa shida tu milele- "Not personal and no Offence intended pls"
  1. Ukiona rafiki, jirani au mfanyakazi mwenzio kapata kadeal kadogo roho inakuuma- wivu wa kinyongo
  2. Ukiona mtu ana mafanikio hata kama humjui unasema -" hawa si ndo mafisadi, wezi, wauza unga etc"
  3. Ukiwa na vijisenti unaona hakuna mwingine kama wewe, in fact wewe ndo mtu wengine wote nyani tu.
  4. Upo radhi kufanya kila lililo ndani ya uwezo wako ili rafiki, jirani au jamaa yako akose fursa inayompa kwende msalani
  5. Ukisikia deal la hela unataka ni wewe tu ulikamue hata kama halikuhusu na unatengeneza zengwe ili aliyekusudiwa asilipate.
  6. Ukiamka asubuhi kitu cha kwanza unawaza nani umpige mzinga halafu utamdhulumu
  7. Una mashaka mashaka kila wakati na unamuona kila mtu anayekukaribia ni mmbaya na anataka kukudhuru
  8. Ukimuona mke/mume/boyfriend/girlfriend wa mshakaji wako unamvua nguo kwa fikra. Yaan hadi unalala naye kimawazo
  9. Kama una chale za aina yoyote mgongoni, tumboni, kifuani, kiunoni, kwenye makalio au sehemu zozote za mwili zinazofunikwa
  10. Una kipato (japo cha wastani) lakini watu wako wa karibu kama mke/watoto/baba/mama/ndugu etc wana shida hakuna maelezo
  11. Unapenda kumpongeza mtu kwa mafanikio yake, yaani kila siku wa kwanza kutoa pongezi lakini kimoyo moyo unaumia hadi moyo umepondeka.
  12. Unapenda sana kukopa lakini kulipa ni issue mpaka unapelekwa kwa mjumbe au polisi
  13. Unapenda sana stori za waganga, mitishamba na unaamini ramli ndo njia nzuri ya kumjua mmbaya wako
  14. Unapenda kutembelea na kujipumzisha karibu na makaruburi au miti mikubwa kama mbuyu
Hii ni part I kwa sasa, part II ipo njiani na wazinzi wengi wapo humo.
 
Daah bro umenichekesha sana hapo namba 13 na 14' we noma aise
 
15. Ukiwa unaongea sana na kwa sauti ya juu kwenye Dalala,Bar,darasan na sehem zote za mikusanyiko ya kistaarabu.

16.Kuwa wa kwanza kutoka na wa mwisho kurudi nyumbani kwako kuliko watu wote mtaan kwako.

17.Ukiingia chooni unakuwa na wasiwasi sana juu ya utupu wako na una hisi kama kuna mtu ana kuchungulia,nakuficha kwa bidii sehemu zako nyeti kwa bidii.

18.Kwa matajiri, Nje ni msafi kweli kweli ila ndani uko very mess



Sent from my BlackBerry 9780using JamiiForums
 
unapenda sana ufaulu mtihani lakini kusoma hutaki
 
15. Ukiwa unaongea sana na kwa sauti ya juu kwenye Dalala,Bar,darasan na sehem zote za mikusanyiko ya kistaarabu.

16.Kuwa wa kwanza kutoka na wa mwisho kurudi nyumbani kwako kuliko watu wote mtaan kwako.

17.Ukiingia chooni unakuwa na wasiwasi sana juu ya utupu wako na una hisi kama kuna mtu ana kuchungulia,nakuficha kwa bidii sehemu zako nyeti kwa bidii.

18.Kwa matajiri, Nje ni msafi kweli kweli ila ndani uko very mess



Sent from my BlackBerry 9780using JamiiForums

Mkuu hii 17 na 18 umetisha. Ila nimeiapprove. List imeongezeka
 
Mtoa MADA Kingmairo inaonekana vigezo vyote hivyo unavyo, maana aisifiaye mvua imenyesheshea. Mtu anajijua mwenyewe aisee. Hongera!

Mkuu...umenichekesha kiasi ila sio lazma atoaye neno lazma hilo leno awe analiishi. Unaweza ukawa una ufahamu wa jambo kupitia kujifunza na kuona toka kwa watu na mazingira ya kijamii. Hii tunaita social learning
 
Back
Top Bottom