Ukiona mtu anajikinga sana na elimu aliyonayo ujue ni mjinga wa kupindukia

Mghaka

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
320
127
Mawazo mazuri, busara, hekima na upeo wa kunyambulisha mambo si matokeo ya shule kubwa bali ni kipaji tuu. shule inaongezea kidogo tu. Mfalme Suleimani alisoma wapi kuwa social psychologist kiasi cha kutoa hukuma ya kesi ya akinamama wawili waliogombania mtoto, kwa wasiofahamu niwaklumbushe! ("nyie akina mama kwa kuwa mnagombania huyu mtoto na sasa nimeshindwa kuwaamua naagiza kisu ili mgawane, mama mmoja akasema sawa! na mwingine mimi namwachia mtoto mwezangu Mungu ndiye ataamua kwani hata akiwa kwake nitaendelea kumwona mtoto yu hai, ndipo Mfalme Suleimani akatambua mama mwenye mtoto ni yule aliyekataa asichingwe")


Wako watu wameishi na kukua katika elimu ya kukariri na ni maprofessor leo lakini ni mbumbumbu katika uhalisia wa dunia ya kijamii. Wako watu humu jamii forum wanavyeti vya shule ambavyo si vyao, na namna walivyopata wanajua wao! Dunia ya kitanzania vyeti ni bora kuliko busara na hekima ya mtu? Mbona tumepotea jamani. Steve Biko alifukuzwa shule na udaktari hakuhitimu lakini busara iliyopo katika maandishi yake inadumu na tunamkumbuka kuliko maprofessor wa siasa wengi hapa duniani. Professor anayetengeneza shirika ili lishiriki udanganyifu wa kura za maoni kwa kuwapa ujiko wasiostahili naye ni msomi na anapaswa kusikilizwa? yoyoyoyo! Nelson Mandela amesoma shule gani mnaeijua ninyi wenzangu? Samora? Newton na mvumbuzi wa umeme wote walikimbia shule ya darasani?

Marehemu Moringe Sokoine alikuwa na shule gani lakini sote tunajua alichoifanyia nchi hii katika kuondoa ufisadi wa kibiashara na rushwa.Msomeni Wilson Churchill, Gadhi Mahatma, Msomeni George Washngton Wote hawa walikuwa na elimu ya kawaida sana Hata wakina Nuhu na gharika na ujenzi wa safina, Mapharaoh nk

Kama maajabu ya hawa watu mnayakubali kwa nini mnayakataa ya akina Lema, sugu, nyerere na wengine, Usiangalie wana nini angalia wanasema nini, Vipaji walivyonavyo katika kuwasilisha yale wanayoyafahamu na ujasiri wa namna ya kuyatatua ndiyo yamewauza na kuwafanya wakubalike kwa umma na ndio wanaoichachafya na kuinyima usingizi CCM. CCM kaeni na vyeti vyenu waacheni CDM wakae na mawazo yao ambayo wanayatoa kichwani mwao na wananchi wanayakubali

Kalaga baho! tukwiwona lulu! itang'asa imilau! chewililye chechako, We jamaa mawazo uliyonayo kichwani ni bora kuliko kiburi cha vyeti vyako
 
Mawazo mazuri, busara, hekima na upeo wa kunyambulisha mambo si matokeo ya shule kubwa bali ni kipaji tuu. shule inaongezea kidogo tu. Mfalme Suleimani alisoma wapi kuwa social psychologist kgiasi cha kutoa hukuma ya kesi ya akinamama wawili waliogombania mtoto, kwa wasiofahamu niwaklumbushe! ("nyie akina mama kwa kuwa mnagombania huyu mtoto na sasa nimeshindwa kuwaamua naagiza kisu ili mgawane, mama mmoja akasema sawa! na mwingine mimi namwachia mtoto mwezangu Mungu ndiye ataamua kwani hata akiwa kwake nitaendelea kumwona mtoto yu hai, ndipo Mfalme Suleimani akatambua mama mwenye mtoto ni yule aliyekataa asichingwe")


Wako watu wameishi na kukua katika elimu ya kukariri na ni maprofessor leo lakini ni mbumbumbu katika uhalisia wa dunia ya kijamii. Wako watu humu jamii forum wanavyeti vya shule ambavyo si vyao, na namna walivyopata wanajua wao! Dunia ya kitanzania vyeti ni bora kuliko busara na hekima ya mtu? Mbona tumepotea jamani. Steve Biko alifukuzwa shule na udaktari hakuhitimu lakini busara iliyopo katika maandishi yake inadumu na tunamkumbuka kuliko maprofessor wa siasa wengi hapa duniani. Professor anayetengeneza shirika ili lishiriki udanganyifu wa kura za maoni kwa kuwapa ujiko wasiostahili naye ni msomi na anapaswa kusikilizwa? yoyoyoyo! Nelson Mandela amesoma shule gani mnaeijua ninyi wenzangu? Samora? Newton na mvumbuzi wa umeme wote walikimbia shule ya darasani?

Marehemu Moringe Sokoine alikuwa na shule gani lakini sote tunajua alichoifanyia nchi hii katika kuondoa ufisadi wa kibiashara na rushwa.Msomeni Wilson Churchill, Gadhi Mahatma, Msomeni George Washngton Wote hawa walikuwa na elimu ya kawaida sana Hata wakina Nuhu na gharika na ujenzi wa safina, Mapharaoh nk

Kama maajabu ya hawa watu mnayakubali kwa nini mnayakataa ya akina Lema, sugu, nyerere na wengine, Usiangalie wana nini angalia wanasema nini, Vipaji walivyonavyo katika kuwasilisha yale wanayoyafahamu na ujasiri wa namna ya kuyatatua ndiyo yamewauza na kuwafanya wakubalike kwa umma na ndio wanaoichachafya na kuinyima usingizi CCM. CCM kaeni na vyeti vyenu waacheni CDM wakae na mawazo yao ambayo wanayatoa kichwani mwao na wananchi wanayakubali

Kalaga baho! tukwiwona lulu! itang'asa imilau! chewililye chechako, We jamaa mawazo uliyonayo kichwani ni bora kuliko kiburi cha vyeti vyako

Umezunguka sana kiongozi kiasi kwamba uzi utatutesa waliowengi kuelewa lengo na mlengwa. Sijui labda aje Prof.Mkandala na Dr. Bana wana REDET watusaidie.
 
Umezunguka sana kiongozi kiasi kwamba uzi utatutesa waliowengi kuelewa lengo na mlengwa. Sijui labda aje Prof.Mkandala na Dr. Bana wana REDET watusaidie.

mkuu mbona stare decisis(kiini cha uzi) kimeeleweka poa tu. labda rudia tena kuusoma.
 
Back
Top Bottom