Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakuu
Je, Mbowe yupo nyuma ya yanayoendelea kati ya wagombea na watiania wa ubunge 55 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa 2020 na 2025 maarufu G55 wanaowakilisha zaidi ya watiania 200, wakiwemo viongozi wa juu wa chama hicho dhidi ya uongozi wa sasa chini ya mwenyekiti wao Tundu Lissu ambaye anaongoza harakati za kuzia uchaguzi kama hakutafanyika mabadiliko (no reforms, no election).
Soma, Pia: Waraka wa wagombea 2020 na watia nia wa ubunge 55 wa CHADEMA
Tangu kukubali kushindwa uchaguzi wa ndani wa chama hicho na kusema anaenda kusaka Mafekeche, Mbowe aliamua kukaa kimya na kutoshiriki wazi wazi shughuli za chama hali ambayo inazua maswali mengi kwani wengi wanaoonyesha kwenda tofauti na harakati za chama chini ya Lissu ni wale waliokuwa timu Mbowe.
Mbowe ni mjumbe wakudumu wa Kamati Kuu ya chama lakini hayaonekani kwenye vikao kazi vya chama wala kuzunguka mikoani kueneza ajenda ya kutaka mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi.
Kama Mbowe angekuwa bega kwa bega na Lissu, haya yanayoendelea hivi sasa ya Lembrus Mchome, John Mrema na wengine Je, tungeyashuhudia?
Je, Mbowe yupo nyuma ya yanayoendelea kati ya wagombea na watiania wa ubunge 55 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa 2020 na 2025 maarufu G55 wanaowakilisha zaidi ya watiania 200, wakiwemo viongozi wa juu wa chama hicho dhidi ya uongozi wa sasa chini ya mwenyekiti wao Tundu Lissu ambaye anaongoza harakati za kuzia uchaguzi kama hakutafanyika mabadiliko (no reforms, no election).
Soma, Pia: Waraka wa wagombea 2020 na watia nia wa ubunge 55 wa CHADEMA
Tangu kukubali kushindwa uchaguzi wa ndani wa chama hicho na kusema anaenda kusaka Mafekeche, Mbowe aliamua kukaa kimya na kutoshiriki wazi wazi shughuli za chama hali ambayo inazua maswali mengi kwani wengi wanaoonyesha kwenda tofauti na harakati za chama chini ya Lissu ni wale waliokuwa timu Mbowe.
Mbowe ni mjumbe wakudumu wa Kamati Kuu ya chama lakini hayaonekani kwenye vikao kazi vya chama wala kuzunguka mikoani kueneza ajenda ya kutaka mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi.
Kama Mbowe angekuwa bega kwa bega na Lissu, haya yanayoendelea hivi sasa ya Lembrus Mchome, John Mrema na wengine Je, tungeyashuhudia?