Huyo jamaa mwenye pikipiki macho yametafsiri yaliyokiona ikapeleka kwenye ubongo ubongo ukashusha Mwanza-Nyegezi. Mathalani angejua historia ya huyo dada udenda usingemtoka kiasi hicho. Hayo ndio yanatukuta wanaume nyumbani tunaacha mke mwema mzuri mcha Mungu anakuheshimu, umebarikiwa vitoto vizuri vinasoma english medium hawajui baba kumbe akisafiri anakuwa firauni, akifika safarini siku hiyo hiyo anakwenda bar ama club anakuta lidada jeupe pee limejinenepea limeacha mapaja nje yenye michirizi ili likutege vizuri, unafika bei kumbe ni unene wa ARV unabeba matatizo, unampelekea mke wako aliyetulia nyumbani, maskini vitoto vinakuita dad , kumbe tayari mambo yakianza unaanza kusingizia magojwa ya wasomi mara kisukari , mara pressure, mara umelogwa... Tuache tamaa....hata kama ni mchepuko umeupata chukua muda kupata ABC zake... wewe unamkuta bar eti na namba ya simu umechukua unadhani wamwona mwenyewe hapo?