Ukimchagua kiongozi asiyefaa, umechagua maisha mabaya kwa miaka 5

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,116
Kufanya maamuzi mabaya wakati wa uchaguzi kunawagharimu watu wengi sana, wengi hukubali kurubuniwa kwa rushwa au ahadi za madaraka, upendeleo au kumchagua mtu kisa ni wa chama chake hata kama hafai. Huuza haki yao ya msingi ya kufanya maamuzi yao binafsi na sahihi kwenye boksi la kura.

Wakati unapokuwa umeshindwa kufika kwenye shughuli zako kwa wakati kutokana na ubovu wa barabara, unateseka na kukosekana kwa huduma muhimu za kijamii au kupanda kwa gharama za maisha ile rushwa uliopewa ushakula imeisha au kile kitenge na tisheti vishachakaa na havifai tena ila una miaka 5 ya tabu kwa kumchagua kiongozi asiyefaa.

Wahenga walisema ningejua huja mwisho wa safari na majuto ni mjukuu, unaposema ningejua ushachelewa inabidi ujipange upyaaaa! Usikubali kuishi kwa majuto miaka 5 fanya maamuzi sahihi kumpata kiongozi bora.
 
Katiba imara ndiyo mlinzi wa kura yako, hakuna njia mbadala na ya mkato huku watawala wanalichezea sanduku la kura kama kasha la manyangarakasha.
 
Hata hivyo kupanga ni kuchagua 🐒

kila raia ana uhuru wa kupima na kuamua kuchagua atakavyo bila kushurutushwa wala kuburuzwa kwa namna yeyote ile na mawazo au mtazamo wa wengine kuhusu kumchagua nani wakati wa uchaguzi 🐒

vinginevyo ni kujipanga tu, kulaumiana na kujipa umuhimu kwamba wewe ndie hodari zaidi, unajua viongozi wa zuri zaidi na kwamba ushawishi wako ndio makini zaidi ya wengine.

Fursa ipo, jitokeze bayana bila hiyana wala haya eleza kinagaubaga kiongozi nzuri ni yupi wa chama gani na ana sera gani na wananchi watakuskiza na kuamua kukupa maua yako kwenye debe siku ya uchaguzi 🐒

R.I.P Laigwanan comrade ENL
 
hata hivyo kupanga ni kuchagua 🐒

kila raia ana uhuru wa kupima na kuamua kuchagua atakavyo bila kushurutushwa wala kuburuzwa kwa namna yeyote ile na mawazo au mtazamo wa wengine kuhusu kumchagua nani wakati wa uchaguzi 🐒

vinginevyo ni kujipanga tu, kulaumiana na kujipa umuhimu kwamba wewe ndie hodari zaidi, unajua viongozi wa zuri zaidi na kwamba ushawishi wako ndio makini zaidi ya wengine.

Fursa ipo, jitokeze bayana bila hiyana wala haya eleza kinagaubaga kiongozi nzuri ni yupi wa chama gani na ana sera gani na wananchi watakuskiza na kuamua kukupa maua yako kwenye debe siku ya uchaguzi 🐒

R.I.P Laigwanan comrade ENL
Muache wizi wa kura.Mkikaa kwenye vikao vyenu vya kichawi/CCM muambiane.
 
Labda muwaondoe hawa wazee wa mitaani na wamama maana wenyewe wakishapewa vitenge na elfu kumikumi za chai huwaambii kitu.
 
Muache wizi wa kura.Mkikaa kwenye vikao vyenu vya kichawi/CCM muambiane.
Wanaoibiwa kila siku, sikuzote si huwa ni washamba tu.

Unaibiwa unashangaa tu, unaibiwa tena unacheka cheka tu. Huo si uzwazwa sasa....

kwanza, unaibiwaje kitu ambacho hata huna 🤣

Hapana kujificha nyuma ya kisingizio cha kuibiwa kura hutasaidika kamwe, Lazima muwe wabuni sera makini na wapanga mikakati mahiri ili kuvutia wananchi na kupata uungwaji mkono wa wananchi walio wengi nyakati za uchaguzi 🐒

Kuzira na kususa ni none sense, hakuna atakae waonea huruma. Vyama vilivyo jipanga kushinda uchaguzi na kushika Dola huwekeza kila rasilimali waliyonayo kwa wananchi, hawategemei huruma wala muujiza kushinda uchaguzi 🐒

kura ni yakutafuta kwa udi na uvumba my friend 🐒

R.I.P Laigwanan comrade ENL
 
Back
Top Bottom