Ukifa unazaliwa tena

Ukifa unazaliwa tena

Duh na ungekuwa una kufa unazaliwa mnyama ungeta uwe mnyama gani? 😂
Unanijaribu unatak niseme kuwa nitachagua kuwa papa huko Baharini?

Lion, Tiger, Fisi, Mbwa, Chris nk

Kifup mnyama anayekula nyama ( carnivores)
 
Napenda kula nyama san 🤣 mboga za majani kwani nimekuwa ng'ombe

halafu kuna wanyama kama mbuzi, swala, kondoo nk hawa wanaliwa ujue 😬
Duh kweli wewe mchaga
 
Children who had lived before
Nimesoma sana Habari hizi na zimetokea sehemu nyingi duniani

Kuna mtoto alikuwa miaka 4 aliwakana wazazi wake hapa
Alisema hao sio wazazi wake bali alizaliwa kwenye nyumba iliyopo karibu na bahari na alitaja nyumba mpaka wazazi wake

Na walifuatitia ikawa ni kweli hiyo nyumba ipo na alipofika kuiona tu alifurahi sana
Wenye nyumba (sio wazazi) waliombwa na waandishi na mtoto aliingia mbio bila kukosea akasema chumba Changu hiki hapa na anakimbia kama wewe ukiwa kwenu unavyopajua

Mwingine ni Syria/Israel border huko Golan heights
Alizaliwa mtoto na alipokuwa miaka 3 akasema aliuwawa na hii birthmark ya kichwa ni shoka alilopigwa
Aliwapeleka mpaka kwa aliemuuwa na pia kaburi alilozikwa na wakafukua wakakuta mtu kazikwa na kichwani kapigwa na kitu kizito

Muuwaji wake alipooulizwa alikana mwanzo lakini shoka lilipatikana na akakubali kosa
Locals walisema huyo mtu alipotea 4 years ago

Hivi visa vipo ila nasoma kama hadithi ingawa wengi huwa wanashirikishwa kama professors na doctors na wataalamu kibao
 
Ww una amini nini?
Ni naamini na kwa Mungu waenda kuchomwa. Haiwezekani uishi maisha ya kifedhuli duniani uwe shoga, muuaji, mchawi halafu uishie tu kwenda kuzaliwa tena. Tusiwape moyo washenzi wafikiri ufirauni wao wanaoufanya mwishowe ni kwenda tu kuzaliwa tena nchi nyingine halafu yaishe.
 
Shanti Devi = Shanti Devil AU Shanti Shetani, walitoa "l" kwenye neno Devi ili isijulikane kuwa huyo Binti ni wakala wa shetani katika kuuhadaa ulimwengu juu ya maisha baada ya kifo.
 
Kuhusu mtu anaenda wapi baada ya kifo imebaki kuwa fumbo kwa sababu sayansi inasema mengine na dini mbalimbali zinasema mengine.

Kwa msichana Shanti Devi ilikua tofauti kidogo, baada ya kifo chake alizaliwa sehemu nyingine akiwa na kumbukumbu za zamani

Tushuke nayo


Shanti Devi alikuwa msichana mdogo aliyezaliwa Delhi, India mwaka wa 1926. Akiwa na umri wa miaka minne, alianza kudai kwamba alikuwa na kumbukumbu za maisha ya zamani kama mwanamke aitwaye Lugdi Devi, ambaye aliishi katika mji uitwao Muttra (kama maili 90 kutoka Delhi).

Shanti angezungumza na wazazi wake kuhusu maisha yake ya zamani, akieleza mji alioishi, watu aliowajua, na matukio yaliyotokea. Alidai kwamba alikufa wakati wa kujifungua na kwamba jina la mumewe lilikuwa Kedar Nath

Wazazi wa Shanti hapo awali walitupilia mbali madai yake, lakini kadiri alivyokuwa mkubwa, alisisitiza zaidi, na kumbukumbu zake zikawa nyingi zaidi. Mara nyingi alikuwa akichora picha za mji aliokua akiishi zamani na alama zak

ambazo wazazi wake walifanya uchunguzi na kuthibitisha baadaye kuwa sahihi.

Mnamo 1935, Shanti alipokuwa na umri wa miaka tisa, hadithi yake ilivutia fikira za mwalimu wake, ambaye alimwandikia barua profesa wa falsafa katika Chuo Kikuu cha Delhi. Profesa, aitwaye Dk

Ian Stevenson, alikuwa na nia ya kuchunguza madai ya kuzaliwa upya na aliamua kukutana na Shanti.

Walivyokutana, Stevenson alimwomba Shanti kutoa maelezo zaidi kuhusu maisha yake ya zamani. Aliweza kueleza mpangilio wa mji, majina ya mitaa, na maeneo ya majengo mbalimbali.

Pia alimtambua mwanamume anayeitwa Pandit Kanjimal, ambaye alidai kuwa alikuwa mshirika wa biashara wa mumewe.

Stevenson aliamua kuchunguza madai ya Shanti zaidi na akasafiri hadi Muttra ili kuona kama angeweza kuthibitisha kumbukumbu zake.

Aliweza kuipata nyumba aliyokuwa akiishi Lugdi Devi na kugundua kwamba maelezo mengi ambayo Shanti alikuwa ameeleza yalilingana na nyumba hiyo na mazingira yake.



Pia alimpata mwanamume anayeitwa Pandit Kanjimal, ambaye alithibitisha kuwa Lugdi Devi alikuwa mke wa mshirika wake wa kibiashara na alikufa wakati wa kujifungua.

Uchunguzi wa Stevenson ulienea kwenye vichwa vya habari duniani kote, na Shanti akawa maarufu katika jambo kuzaliwa upya. Hadithi yake baadaye iliandikwa katika kitabu kinachoitwa "Kesi Ishirini Zinazopendekeza Kuzaliwa Upya," ambacho Stevenson alichapisha mnamo 1966.

Mbali na Shanti Devi, watu wengine ambao wamewahi kuzaliwa na kuwa na kumbukumbu za kuishi zamani sawa na Shanti Devi ni kama James Leininger, Ryan Hammons pamoja Bridey Murphy
Huenda hata wewe mtoa mada ulishawahi kuishi huko New York miaka ya zamani Sana kabla ya kuzaliwa tena huku Tanzania.
 
Ni naamini na kwa Mungu waenda kuchomwa. Haiwezekani uishi maisha ya kifedhuli duniani uwe shoga, muuaji, mchawi halafu uishie tu kwenda kuzaliwa tena. Tusiwape moyo washenzi wafikiri ufirauni wao wanaoufanya mwishowe ni kwenda tu kuzaliwa tena nchi nyingine halafu yaishe.
Ukijua dunian tunaishi kwa probability uwezi kuwaza sana how have sure kuna moto uko
 
Huenda hata wewe mtoa mada ulishawahi kuishi huko New York miaka ya zamani Sana kabla ya kuzaliwa tena huku Tanzania.
Naomba niludishwe huko New york uku bongo mambo magumu sana 😂😂
 
M
Shanti Devi = Shanti Devil AU Shanti Shetani, walitoa l kwenye neno Devi ili isijulikane kuwa huyo Binti ni wakala wa shetani katika kuuhadaa ulimwengu juu ya maisha baada ya kifo.
h ya kweli haya?
 
Children who had lived before
Nimesoma sana Habari hizi na zimetokea sehemu nyingi duniani

Kuna mtoto alikuwa miaka 4 aliwakana wazazi wake hapa
Alisema hao sio wazazi wake bali alizaliwa kwenye nyumba iliyopo karibu na bahari na alitaja nyumba mpaka wazazi wake

Na walifuatitia ikawa ni kweli hiyo nyumba ipo na alipofika kuiona tu alifurahi sana
Wenye nyumba (sio wazazi) waliombwa na waandishi na mtoto aliingia mbio bila kukosea akasema chumba Changu hiki hapa na anakimbia kama wewe ukiwa kwenu unavyopajua

Mwingine ni Syria/Israel border huko Golan heights
Alizaliwa mtoto na alipokuwa miaka 3 akasema aliuwawa na hii birthmark ya kichwa ni shoka alilopigwa
Aliwapeleka mpaka kwa aliemuuwa na pia kaburi alilozikwa na wakafukua wakakuta mtu kazikwa na kichwani kapigwa na kitu kizito

Muuwaji wake alipooulizwa alikana mwanzo lakini shoka lilipatikana na akakubali kosa
Locals walisema huyo mtu alipotea 4 years ago

Hivi visa vipo ila nasoma kama hadithi ingawa wengi huwa wanashirikishwa kama professors na doctors na wataalamu kibao
Mimi nipo njia panda
 
Back
Top Bottom