Ukibanana na Mchafu, Hakika Utachafuka

Ukibanana na Mchafu, Hakika Utachafuka

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,940
Mara nyingi hata watu wazuri walichafuka kwaajili ya kujishikamana na watu wenye matendo machafu. Kuna misemo na mausia mengi kuanzia kwenye vitabu vya dini mpaka kwenye jamii juu ya wale tunaoshikamana na waovu:

Biblia inasema, jicho lako likikukosesha ling'oe maana ni aheri kuingia mbinguni na jicho moja kuliko kubakia nayo yote halafu ukaukosa ufalme wa mbinguni. Jicho hili la kukukosesha ndio hawa watu wanaotuzunguka na kukaribiana nao.

Kuna ule msemo kuwa ndege wafananao huruka pamoja. Nayo ni tahadhari, juu ya wale wanaoambatana au kushikamana na waovu. Ukiwa karibu na jambazi, jamii itakuchukulia nawe ni jambazi. Ukiwa umejishikamana na jambazi linaloua watu, linalopora mali za watu, na linalowapoteza watu, tambua nawe utachukuliwa kuwa ama unafurahia huo uchafu au nawe unashiriki kwenye huo uchafu.

Naambiwa kule Vatican wakiwa wanafanya uchaguzi wa kumpata Papa, mara akichaguliwa, ili kujua Papa huyu atakuwa ni mtu wa namna gani, wanangojea wasikie jina atakalolichagua. Ndiyo maana hata Papa wa sasa alipochaguliwa tu, na kisha kuchagua jina la Francis, ilimaanisha Papa huyu atafuata fadhila ya umaskini kama alivyokuwa Mt. Francis, atakuwa mtu wa msamaha na asiyependa kabisa kumhukumu yeyote. Na ndicho kilichotokea. Kwanza aligomea kuhamia nyumba iliyokuwa maalum kwaajili Papa kwa sababu aliiona ni ya kifahari. Akamsimamisha Askofu wa Ujerumani aliyekuwa ametengeneza kitanda chenye thamani zaidi ya dola 10,000. Alipoulizwa kuhusu mashoga, akajibu tu kuwa kanisa kazi yake ni kumfundisha mwanadamu nini kilicho sahihi kwa kadiri ya mpango wa Mungu, lakini ni nani yeye hata amhukumu mwanadamu mwingine? Kazi yake ni kufundisha, siyo kuhukumu.

Mambo mengi mabaya na ya kutisha wakati wa utawala wa Hayati Magufuli, ni Bashite aliyekuwa akiyasimamia. Akapewa uhuru mkubwa wa kutenda aliyoyataka bila kukemewa wala kuadhibiwa. Na aliweza kufikia hapo baada ya kufanikiwa kumtisha Hayati Magufuli, na kumwaminisha kuwa yeye ndiye pekee aliyempenda na kujitoa maisha yake yote kwaajili yake Rais. Matendo maovu yote aliyoyafanya Bashite kwa jina la wasiojulikana, kuwatisha wafanyabishara wakubwa na kuwabambikia kesi za biashara za madawa ya kulevya, mwishowe lawama zilimwangukia Magufuli. Bwana huyu alifanikiwa kupokonya sehemu ya madaraka ya Rais na kuyatumia katika uovu, kiasi cha kumkaripia hata waziri mkuu na IGP. Marehemu Maguguli alikuja kugundua wakati muda umepita.

Rais Samia, yupo kwenye njia ile ile aliyoipita Rais Magufuli, na kwa vile ndiyo aliyoichagua, pia naye atayavuna matunda yale yale. Ajue kuwa maovu yote atakayoyatenda Bashite, yeye ndiye atabeba gharama yake. Watakaouchukia uovu wa Bashite, watamchukia na yeye pia. Ni suala la muda tu, tutashuhudia mengi.

Rais ana machaguo mawili tu mbele yake. Aruke pamoja na watanzania wema au aruke na mtu mwovu, naye awe sehemu ya uovu wake.
 
Umechafua Uzi Kwa kumtaja pope aliyejitambulisha Rasmi kuwa ni .....wa kule chini.

Au ndio msimamo wenu wanademokrasia kuwa USHOGA ni HAKI za binadamu?
 
Naona umeandika blaa blaa za kutetea ujinga wa kubariki ndoa za jinsia moja. Hayo mengine ya uzushi naona umeamua tu kuchomekea lakini lengo lako lilikuwa ni kutaka kueneza habari za kishetani na ushetani zinazohubiriwa sana na mataifa ya magharibi na Marekani yenyewe.

Ndiyo akili yako inapoishia. Bakia hapo hapo, sioni kama kuna mwenye kukusaidia.

Sijawahi kusikia kuwa kuna kiongozi yeyote amewahi kuelekeza ushoga ubarikiwe. Baraka hutolewa na Mungu, na kamwe Mungu hawezi kubariki dhambi, japo anasamehe dhambi zote isipokuwa kumkufuru Roho Mtakatifu.
 
Umechafua Uzi Kwa kumtaja pope aliyejitambulisha Rasmi kuwa ni .....wa kule chini.

Au ndio msimamo wenu wanademokrasia kuwa USHOGA ni HAKI za binadamu?

Haitakuja kutokea ushoga ikawa ni haki ya mtu yeyote kwa sababu siyo mpango wa Mungu.

Mungu angetaka tuwe mashoga, angetufanya wote tuwe wanaume au wote tuwe wanawake.
 
Naona umeandika blaa blaa za kutetea ujinga wa kubariki ndoa za jinsia moja. Hayo mengine ya uzushi naona umeamua tu kuchomekea lakini lengo lako lilikuwa ni kutaka kueneza habari za kishetani na ushetani zinazohubiriwa sana na mataifa ya magharibi na Marekani yenyewe.
Mtoa mada yupo sahihi wewe Lucas chawa na huyo kichaa wenu makonda hawezi kudumu kwenye hiyo nafasi coz ameanza na mguu mbaya sana

Tayari graph ya mama samia imeshuka gafla baada ya kumteua bashite kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha.
 
Rais ana machaguo mawili tu mbele yake. Aruke pamoja na watanzania wema au aruke na mtu mwovu, naye awe sehemu ya uovu wake.
Inawezekana hukuukusudia mstari huu kama ulivyokaa hapa; kwani huko juu, ikiwa ni pamoja na kichwa cha mada ulivyo kiwasilisha vinapingana na mstari huo.

Msemo wa "ndege..." ndio sahihi unao elezea vizuri, uhusiano wa Bashite na Magufuli; na sasa na Samia.

Samia hakumrudisha Bashite kwa bahati mbaya baada ya kukaa nje ya uongozi baada ya kutemwa na Magufuli. Huyu mama atakuwa anamjua ndani na nje huyu mtu, kwani siyo mgeni kwake.
Kwa hiyo swali muhimu la kujiuliza katika mada yako hii ni kwa sababu zipi zilizo fanya iwe muhimu sana mtu kama Bashite kurudishwa katika uongozi. Mama alikosa kitu gani katika wengine wote, ambacho Bashite pekee ndiye aliye nacho?
 
Ndiyo akili yako inapoishia. Bakia hapo hapo, sioni kama kuna mwenye kukusaidia.

Sijawahi kusikia kuwa kuna kiongozi yeyote amewahi kuelekeza ushoga ubarikiwe. Baraka hutolewa na Mungu, na kamwe Mungu hawezi kubariki dhambi, japo anasamehe dhambi zote isipokuwa kumkufuru Roho Mtakatifu.
Dah.
Mkuu 'Bams', kumbuka hapa tupo JF; kuna kila aina ya watu humu. Haya ya kiimani yaweke pembeni, tunao mzigo mkubwa sana sasa hivi kuhusu hatma ya nchi yetu na hawa viongozi wabovu tunaoletewa na CCM. Tujikite huko huko, huenda kukawa na njia ya kuwabadili baadhi ya hawa machawa wanao tuvuruga sana siku hizi hapa JF.
Miaka mingine mitano au zaidi ya huyu mama itakuwa ni balaa kubwa sana kwa nchi hii.
 
It’s truly amazing!

Yaani mtu anaesemwa kuwa zero brain, jambazi, hasiyejua anachokifanya na hasiyetakiwa na jamii ndio anawafanya muandike kurasa baada ya kurasa humu ndani? Kwa maneno tu aliyosema, sasa akiyataja hayo majina na kuweka ukweli hadharani (Kama kweli anao na ni Ukweli halisi) itakuwaje??

Makonda, hebu malizia ulipoanzia na utoe evidence beyond any reasonable doubt.
 
Naona umeandika blaa blaa za kutetea ujinga wa kubariki ndoa za jinsia moja. Hayo mengine ya uzushi naona umeamua tu kuchomekea lakini lengo lako lilikuwa ni kutaka kueneza habari za kishetani na ushetani zinazohubiriwa sana na mataifa ya magharibi na Marekani yenyewe.
Wewe chawa Lucas, Makonda anasema Samia anatukanwa na Mawaziri aliowateuwa yeye mwenyewe. CCM kimekuwa chama cha walafi wa madaraka ili wapate nafasi ya kufyonze kilaini keki ya taifa. Ni chama ambacho hakifai tena kuongoza hili taifa.
 
Ndiyo akili yako inapoishia. Bakia hapo hapo, sioni kama kuna mwenye kukusaidia.

Sijawahi kusikia kuwa kuna kiongozi yeyote amewahi kuelekeza ushoga ubarikiwe. Baraka hutolewa na Mungu, na kamwe Mungu hawezi kubariki dhambi, japo anasamehe dhambi zote isipokuwa kumkufuru Roho Mtakatifu.
Huna haja ya kuangaika na huyu kiumbe, hajawai kumiliki akili hata siku moja. Amekuwa akitumika kueneza propaganda nyepesi za kukaririshwa bila kujiongoza. Ushoga anaoupigia upatu ni jambo la kukaririshwa kwasababu umekuwepo muda mrefu, ni janga bila kujali itikadi yoyote. Kutokana na propaganda mfilisi za baadhi ya wanakisiasa walitaka ionekane mbele ya jamii kwamba ni agenda ya baadhi ya vyama vya upinzani, upande mwingine dini fulanifulani walijitahidi kukaa pembeni na kurusha mpira Vatican. Wasiokuwa na akili wameingia kwenye hiyo mtego.
 
Makonda uwe waziri mkuu uwanyoshe watu.
Mwingine ni wewe hapo. Kipindi unatoa CV kuomba kazi kupitia hili jukwaa nilikuona wa maana. Kipi cha ziada alichonacho hadi awe Waziri mkuu. Au unafurahia pale anapowakomoa wale husiowapenda? Anatengeneza migogoro badala ya kuunganisha watu.
 
Naona umeandika blaa blaa za kutetea ujinga wa kubariki ndoa za jinsia moja. Hayo mengine ya uzushi naona umeamua tu kuchomekea lakini lengo lako lilikuwa ni kutaka kueneza habari za kishetani na ushetani zinazohubiriwa sana na mataifa ya magharibi na Marekani yenyewe.
Kwa vile huna akili ndiyo maana umemuelewa mwandishi ndivyo sivyo kwa vile tu amemtaja mumeo nyamitako.
 
Mara nyingi hata watu wazuri walichafuka kwaajili ya kujishikamana na watu wenye matendo machafu. Kuna misemo na mausia mengi kuanzia kwenye vitabu vya dini mpaka kwenye jamii juu ya wale tunaoshikamana na waovu:

Biblia inasema, jicho lako likikukosesha ling'oe maana ni aheri kuingia mbinguni na jicho moja kuliko kubakia nayo yote halafu ukaukosa ufalme wa mbinguni. Jicho hili la kukukosesha ndio hawa watu wanaotuzunguka na kukaribiana nao.

Kuna ule msemo kuwa ndege wafananao huruka pamoja. Nayo ni tahadhari, juu ya wale wanaoambatana au kushikamana na waovu. Ukiwa karibu na jambazi, jamii itakuchukulia nawe ni jambazi. Ukiwa umejishikamana na jambazi linaloua watu, linalopora mali za watu, na linalowapoteza watu, tambua nawe utachukuliwa kuwa ama unafurahia huo uchafu au nawe unashiriki kwenye huo uchafu.

Naambiwa kule Vatican wakiwa wanafanya uchaguzi wa kumpata Papa, mara akichaguliwa, ili kujua Papa huyu atakuwa ni mtu wa namna gani, wanangojea wasikie jina atakalolichagua. Ndiyo maana hata Papa wa sasa alipochaguliwa tu, na kisha kuchagua jina la Francis, ilimaanisha Papa huyu atafuata fadhila ya umaskini kama alivyokuwa Mt. Francis, atakuwa mtu wa msamaha na asiyependa kabisa kumhukumu yeyote. Na ndicho kilichotokea. Kwanza aligomea kuhamia nyumba iliyokuwa maalum kwaajili Papa kwa sababu aliiona ni ya kifahari. Akamsimamisha Askofu wa Ujerumani aliyekuwa ametengeneza kitanda chenye thamani zaidi ya dola 10,000. Alipoulizwa kuhusu mashoga, akajibu tu kuwa kanisa kazi yake ni kumfundisha mwanadamu nini kilicho sahihi kwa kadiri ya mpango wa Mungu, lakini ni nani yeye hata amhukumu mwanadamu mwingine? Kazi yake ni kufundisha, siyo kuhukumu.

Mambo mengi mabaya na ya kutisha wakati wa utawala wa Hayati Magufuli, ni Bashite aliyekuwa akiyasimamia. Akapewa uhuru mkubwa wa kutenda aliyoyataka bila kukemewa wala kuadhibiwa. Na aliweza kufikia hapo baada ya kufanikiwa kumtisha Hayati Magufuli, na kumwaminisha kuwa yeye ndiye pekee aliyempenda na kujitoa maisha yake yote kwaajili yake Rais. Matendo maovu yote aliyoyafanya Bashite kwa jina la wasiojulikana, kuwatisha wafanyabishara wakubwa na kuwabambikia kesi za biashara za madawa ya kulevya, mwishowe lawama zilimwangukia Magufuli. Bwana huyu alifanikiwa kupokonya sehemu ya madaraka ya Rais na kuyatumia katika uovu, kiasi cha kumkaripia hata waziri mkuu na IGP. Marehemu Maguguli alikuja kugundua wakati muda umepita.

Rais Samia, yupo kwenye njia ile ile aliyoipita Rais Magufuli, na kwa vile ndiyo aliyoichagua, pia naye atayavuna matunda yale yale. Ajue kuwa maovu yote atakayoyatenda Bashite, yeye ndiye atabeba gharama yake. Watakaouchukia uovu wa Bashite, watamchukia na yeye pia. Ni suala la muda tu, tutashuhudia mengi.

Rais ana machaguo mawili tu mbele yake. Aruke pamoja na watanzania wema au aruke na mtu mwovu, naye awe sehemu ya uovu wake.
Rubbish
 
Back
Top Bottom