Hivi hii jeuri miaka hii inatokea wapi mbona kipindi hicho mama zetu hawakuwa nayo !?!
Unajua nini, sio tu zama zimebadilika ulimwengu unakwenda kwa kasi sana na mambo yake yamekuwa vululu vululu. Ni jamii chache sana sasa hivi duniani ambazo bado zinaishi kwa misingi ya kuheshimu familia. Namaanisha kuna kizazi kiliacha kuafanya majukumu yake ndio maana unayaona haya yanayotokea kipindi hiki tunachoishi sasa hivi.
Kwanza turudi nyuma kizazi ambacho harusi ilikuwa inaishia kwenye kiwango cha familia na majirani hapo hata makwaruzano ya hiyo ndoa wataojua ni familia tena watu wa karibu na majirani. Siku hizi unaweza ukaenda kwenye harusi au ukajikuta unashiriki harusi ila bibi harusi humjui hujawahi kumuona, wazazi wake huwajui wala hujawahi kuwaona ila unajikuta na wewe ni mwanakamati kisa mtu unayejuana nae ni binamu wa wazazi wa bibi harusi na ndie aliyekuomba mchango na ukajikuta ni mwanakamati.
Sasa mtu ambaye sio ndugu wa karibu na maharusi mkijikuta familia wanamuachia huyo mwanakamati kuleta mapendekezo bila kujali baadae yataleta athari kwa wanandoa hao. Ndo mtu utasikia jamani bibi harusi asiende kunyanyasika huko anakoolewa akingie kwenye familia wajue kuwa binti ametoka familia ambayo iko vizuri, tuhakikishe kamati tutoe michango ya kutosha bibi harusi aende kwake na zawadi kibao ili mumewe na ndugu zake wamuheshimu..... hapo ndo makosa huanza.
Simemi binti au vijana wasipewe zawadi siku ya harusi ila kila kitu kiwe na kiasi, mkiwanunulia maharusi kila kitu kwenye nyumba yao wao watafanya juhudi gani kwwnye maisha?? ni sawa na mtoto unampeleka shule unamlipia ada unamlipia tuition na bado ikifika mtihani wa taifa unamnunulia feki ili afaulu......( huyu mzazi wa hivi unajiuliza akili yake iko sawa..... kama na yeye huyo mzazi alifanyiowa hivyo na wazazi wake basi kosa lilianzia huko nyuma).
Malezi yamebadilika sana na yanaleta athari nyingi sana kwenye familia / ndoa za leo....
Ni mambo mengi sana ambayo yamesababisha wasichana au wamama wa leo kuwa na kiburi hiko ambacho mama zatu / bibi zetu wa zamani hawakuwa navyo.
Swali nini kifanyike??!!...... suluhisho ni nini?
Je ile elimu iliyokuwa inatolewa kipindi kile tunasoma middle school na baadae ikaja elimu ya ujamaa na kujitegemea ilisaidia kuweka familia imara na kila mmoja kutimiza wajibu wake? kwanini ile elimu imeachwa? au bado inafundishwa? je watu wanafundishwa na kukuzwa kujitegemea an kuwa na ujamaa?
Je wanajua ujamaa ni nini? wanajua kujitegemea ni nini?
Watoto wa leo hadi wako na miaka 40 bado wanategemea support za wazazi wao, mzazi alipwe pension ndo amsaidie mwane wa kiume kujenga nyumba au kusomesha wanae.....
Kila mahali vurugu vululu na tunaona huko mitaani...
Eeeehh nimeandika mengi sana acha niishie hapa.