Ukeketaji

Ukeketaji

Habari wana MMU

Tuna binti wetu wa kazi ambae sasa ni kama miezi 6 tangia tumeanza kuishi nae.Ni mwenyeji wa mkoa wa Dodoma.

Huyu binti historia yake hakuwahi kupelekwa shule na kwa maana hiyo hawezi kusoma wala kuandika.Alifanyiwa mpango hapa nyumbani akapelekwa sehemu ili ajifunze kusoma na kuandika then utaratibu mwingine ufuate.

Amekuwa ni rafiki kwangu ingawa me nimempita kiumri ila ananiambia vitu vingi sana.Na huwa na mshauri pale inapobidi...

Juzi mama yake alipiga cm kwa wazazi wangu wakiomba tumrudishe binti yao.Home walikubali na baadae wakampigia tena aongee na binti yao....
Waliongea nae kwa kilugha na hatukujua walichoongea

Sasa leo huyu binti amenifuata chumbani na kuniambia kuwa mama yake atakuwa anamuitia kumkeketa tu maana kabla yakuja huku dar alimwambia akamsalimie bibi yake kijijini (mvumi) akahisi zoez hilo lingekamilishwa lakin hakwenda.

Namuonea huruma sana na nimemwambia kuwa akirudi nyumbani asikubali lakin sasa kaniambia haiwezekani kwani huwa wanawakamatia ndani.

Roho inauma sijajua jinsi yakumsaidia jamani.....nisaidieni ushauri!!!

Mkuu, mshauri asiende---ukeketaji ni mbaya sana kwa watoto wa kike. Ikibidi waelimishe wazazi wake kuhusu madhara ya ukeketaji kama wasipoelewa waripoti dawati la kijinsia--hatuwezi kuona binti anaharibiwa utamu hivi hivi tukakaa kimya! Lakini sijakupata vizuri hapo kwenye red mkuu.
 
Yeah kes coz watamfanyia ktu ambacho hayupo willing nacho.ts violation of human rights

Duuuhh huyu mama yake anatafuta matatizo maana hata shule mtoto hakumpeleka na bado analeta balaa lingine.
 
Mkuu, mahsuri asiende---ukeketaji ni mbaya sana kwa watoto wa kike. Lakini sijakupata vizuri hapo kwenye red mkuu.

Yaani anasema wakiwa wamepanga kukufanyia tohara....mfano upo nje na shughuli zako unatumwa ukachukue kitu ndani basi wanakukamatia humo kukushughulikia.
 
mila na tamaduni ni ubombo(bone marrow), elimu ni vinyweleo tu.

Hakuna elimu inaweza.badilisha fahari yako ya kitsmaduni. Mie bora nilale chini ila ng'ombe niwe nao walau 1000.

Huyu kaanza kuelimika baada yakuona baadhi ya vipind kwenye tv vinavyopinga ukeketaji na kusema madhara yake.

Kuhusu kukaririshwa ni kweli coz kasema wanaotoka kukeketwa ukiwauliza habari za huko wanasema yaani huko ni raha sana.
 
mwambie tuhuyo binti asijaribu kwenda serikali imepiga marufuku.....atakamatwa atafungwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom