Ukeketaji

miss strong

JF-Expert Member
Jul 4, 2012
7,012
3,694
Habari wana MMU

Tuna binti wetu wa kazi ambae sasa ni kama miezi 6 tangia tumeanza kuishi nae.Ni mwenyeji wa mkoa wa Dodoma.

Huyu binti historia yake hakuwahi kupelekwa shule na kwa maana hiyo hawezi kusoma wala kuandika.Alifanyiwa mpango hapa nyumbani akapelekwa sehemu ili ajifunze kusoma na kuandika then utaratibu mwingine ufuate.

Amekuwa ni rafiki kwangu ingawa me nimempita kiumri ila ananiambia vitu vingi sana.Na huwa na mshauri pale inapobidi...

Juzi mama yake alipiga cm kwa wazazi wangu wakiomba tumrudishe binti yao.Home walikubali na baadae wakampigia tena aongee na binti yao....
Waliongea nae kwa kilugha na hatukujua walichoongea

Sasa leo huyu binti amenifuata chumbani na kuniambia kuwa mama yake atakuwa anamuitia kumkeketa tu maana kabla yakuja huku dar alimwambia akamsalimie bibi yake kijijini (mvumi) akahisi zoez hilo lingekamilishwa lakin hakwenda.

Namuonea huruma sana na nimemwambia kuwa akirudi nyumbani asikubali lakin sasa kaniambia haiwezekani kwani huwa wanawakamatia ndani.

Roho inauma sijajua jinsi yakumsaidia jamani.....nisaidieni ushauri!!!
 
Atakuwa anapenda, kwa jamii zinazokeketa hiyo ni heshima.

Kama anajua hilo asiende.

Hajaanza kupigwa kitu?
 
Atakuwa anapenda, kwa jamii zinazokeketa hiyo ni heshima.

Kama anajua hilo asiende.

Hajaanza kupigwa kitu?
Yaa huwa wana feel proud kuketwa na Wao ni Kama heshima na huyo lazima aende maana wana karirishwa kabisa kuwa mwanamke bora lazima akeketwe!

Huyo hawezi kuacha kwenda maana anaona ufahari na ana hamu kabisa ya kufanyiwa hivyo!
 
Atakuwa anapenda, kwa jamii zinazokeketa hiyo ni heshima.

Kama anajua hilo asiende.

Hajaanza kupigwa kitu?

Bado inavyoonekana.....nilifikiri labda anaweza kushtaki kuwa tumemkatalia mwanae kwenda.
 
Yaa huwa wana feel proud kuketwa na Wao ni Kama heshima na huyo lazima aende maana wana karirishwa kabisa kuwa mwanamke bora lazima akeketwe!

Huyo hawezi kuacha kwenda maana anaona ufahari na ana hamu kabisa ya kufanyiwa hivyo!

Huyu kaanza kuelimika baada yakuona baadhi ya vipind kwenye tv vinavyopinga ukeketaji na kusema madhara yake.

Kuhusu kukaririshwa ni kweli coz kasema wanaotoka kukeketwa ukiwauliza habari za huko wanasema yaani huko ni raha sana.
 
Habari wana MMU

Tuna binti wetu wa kazi ambae sasa ni kama miezi 6 tangia tumeanza kuishi nae.Ni mwenyeji wa mkoa wa Dodoma.

Huyu binti historia yake hakuwahi kupelekwa shule na kwa maana hiyo hawezi kusoma wala kuandika.Alifanyiwa mpango hapa nyumbani akapelekwa sehemu ili ajifunze kusoma na kuandika then utaratibu mwingine ufuate.

Amekuwa ni rafiki kwangu ingawa me nimempita kiumri ila ananiambia vitu vingi sana.Na huwa na mshauri pale inapobidi...

Juzi mama yake alipiga cm kwa wazazi wangu wakiomba tumrudishe binti yao.Home walikubali na baadae wakampigia tena aongee na binti yao....
Waliongea nae kwa kilugha na hatukujua walichoongea

Sasa leo huyu binti amenifuata chumbani na kuniambia kuwa mama yake atakuwa anamuitia kumkeketa tu maana kabla yakuja huku dar alimwambia akamsalimie bibi yake kijijini (mvumi) akahisi zoez hilo lingekamilishwa lakin hakwenda.

Namuonea huruma sana na nimemwambia kuwa akirudi nyumbani asikubali lakin sasa kaniambia haiwezekani kwani huwa wanawakamatia ndani.

Roho inauma sijajua jinsi yakumsaidia jamani.....nisaidieni ushauri!!!

Muache mwenzio akakate antenna,atatumia dish
 
Duh.i feel sorry to her.akatoe taarfa pols kabla ya kwenda kwao...
 
Eti eeeehh??acha tu tumzuie
hiyo ni moja ya kazi ngumu kwako maana Hapo ataoneka hana heshima kwa wazazi wake! Mentality waliokuwa jengewa jamii hizi ni ya ajabu sana tena sana!

Jaribu kumzuia pengine unaweza kumuokoa na uanze kumpa elimu kwanza!
 
hiyo ni moja ya kazi ngumu kwako maana Hapo ataoneka hana heshima kwa wazazi wake! Mentality waliokuwa jengewa jamii hizi ni ya ajabu sana tena sana!

Jaribu kumzuia pengine unaweza kumuokoa na uanze kumpa elimu kwanza!

Duuuhh yaani mpaka nasisimka mwili kama nakatwa mie vile.....namuonea huruma maana sijui nitamsaidiaje jamani.
 
Leo binti kakwambia kuwa anahisi kuitwa huko ni kwa ajili ya kumkeketa tuu. Wewe umemshauri kuwa akirudi nyumbani asikubali lakini yeye kadai kuwa haiwezekani kwani huwa wanawakamatia ndani na kuwakeketa. Sheria inasemaje? Kifungu cha 169A(1) cha Sheria ya Tanzania ya Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 kinasema:

169A.-(1) Mtu yeyote ambaye, ni muangalizi, anawajibu au usimamizi wa mtu yeyote mwenye umri wa chini ya miaka kumi na nane akimtesa au akimtelekeza mtu huyo au akisababisha tohara kwa mwanamke au akimtahiri au kusababisha tohara hiyo ifanyike au kusababisha mtu huyo adhalilishwe, ateswe, au atelekezwe kwa namna ambayo itamsababishia maumivu au madhara kwa afya yake, pamoja na maumivu au kuharibu uwezo wake wa kuona, kusikia au kiungo chochote cha mwili au akili, atakuwa ametenda kosa la ukatili kwa mtoto.

Kwa kisoma hicho kifungu, mtakuwa mmetenda kosa la jina kama mtamruhusu kwenda kukeketwa, kama kweli ameambiwa aende kukeketwa bila ridhaa yake? Kwa maana nyingine, hiki kifungu cha sheria kinawahusu nyie? Ana umri gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom