UKAWA watakapotoka tena mwezi ujao!

UKAWA watakapotoka tena mwezi ujao!

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,539
Wadau,

Mtaalam mmoja wa kijeshi anasema, tabia fulani inapopandikizwa vya kutosha ndani ya kicha cha mtu, tabia pandikizi hugeuka na kuwa kama "Second nature" kwa mhusika. Kwa mfano anasema, mtu wa kawaida kabisa anavyojiunga na jeshi, hupandikiziwa tabia ya upiganaji na uvaaji wa magwanda katika kiwango ambacho tabia hiyo huwa ni kama "Second nature" kwa muhusika na huifurahia hali hiyo.

Kwa kuwa UKAWA wamepandikiziwa tabia ya kukimbia mijadala kwa kiwango ambacho tabia hiyo imekuwa kama "second nature" kwao, na kwa kuwa hivi karibuni inatarajiwa kwamba bunge litakutana tena kwa ajili ya kubadilisha sheria kadhaa kuhusu mchakato wa katiba mpya na kuboresha baadhi ya vifungu katika katiba ya 1977, Inatarajiwa kwamba watagoma tena na kuondoka zao.

Sasa kama watagoma kama kawaida; unashauri nini Kifanyike kati ya machaguo matatu ambayo yamekuwepo wakati wote.
1. Rais kuwaita ikulu?
2. Wabunge wanaotaka kuendelea (coalition of the willing ) kuendelea?
3. Mchakato wa marekebisho ya katiba 1977, usitishwe na tuendelee na yo kama ilivyo hadi hapo mpya itakapopitishwa?
 
Mkuu Betlehem, sidhani kama ni sahihi kusema UKAWA walikimbia mjadala, labda wajuvi wa kiswahili watuambie tofauti kati ya kususa na kukimbia! Ukirejea yale maneno ya mwenyekiti mwenza wa UKAWA Prof. Lipumba kuhusu bunge la katiba ilikuwa ni kususa, siyo kukimbia.
Na mimi niungane na wewe kwa hawa ndugu kwamba kususa bila mkakati madhubuti dhidi ya kile walichokisusia haisaidii. Kuondoka na kumuacha mwizi aendelee kuiba, utamfanya mwizi aibe ki-ustadi zaidi na hadi wapita njia watajua kuwa haibi, bali anahamisha, ila ukipiga kelele wapita njia watakusaidia pia.
 
Nafikiri unakosea kitu.Hukumbuki issue ya Sugu kutolewa na maaskari?
Wanaweza kuamua kutokususa,wakamua kupambana humohumo
 
Mkuu santuri ya act haiuuziki bila kuimba ukawa poor betlehem
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri unakosea kitu.Hukumbuki issue ya Sugu kutolewa na maaskari?
Kweli, itabidi watoke tena maana wakibaki wanaweza kutolewa na maaskari kama sugu.swali langu liko kwamba wakishatoka hatua ya kuchukua itakuwa ipi kati ya hizo hapo juu?
 
Kweli, itabidi watoke tena maana wakibaki wanaweza kutolewa na maaskari kama sugu.swali langu liko kwamba wakishatoka hatua ya kuchukua itakuwa ipi kati ya hizo hapo juu?

Kwa nini hili swali usiende kumuuliza baba yako?
 
huyu jamaa ni useless kabisa. hana hoja nyingine zaidi ya chadema na ukawa. hivi ulisha wahi pewa mimba na mwana ukawa nini?
 
Hili swali kwa nini usimuulize bosi wako zana za kilimo ambaye naye alisusa?
 
Wadau,


Sasa kama watagoma kama kawaida; unashauri nini Kifanyike kati ya machaguo matatu ambayo yamekuwepo wakati wote.
1. Rais kuwaita ikulu?
2. Wabunge wanaotaka kuendelea (coalition of the willing ) kuendelea?
3. Mchakato wa marekebisho ya katiba 1977, usitishwe na tuendelee na yo kama ilivyo hadi hapo mpya itakapopitishwa?


CCM muendelee na mchakato maana watakuwa mwamewarahisishia upigaji wa Kura ya ndiyoooooooooooooooooooooo!Si hakuna akidi inayohitaji siyo!

Madam spika ''Nadhani waliosema ndiyooo wamshinda"
Hapo upo? Big up sana.
 
Mbona CCM walikimbia debate na Upinzani wakati wa uchaguzi wa 2010?? Hadi mkamfukuza kazi Tido muhando??

Hehehe watu wanaoongea vikao vya maamuzi ya taifa wewe unaoongea taarab za siasa
 
We mbona huelewi? au unatulazimisha tukubaliane kwamba the only option is to match out?
Nimekuambia sio lazima,wanaweza kushinikiza kwa kufanya fujo kama ilivyowahi kutokea.
 
Nimekuambia sio lazima,wanaweza kushinikiza kwa kufanya fujo kama ilivyowahi kutokea.
Lakini ni vizuri fujo hiyo wakaifanyia nje ili waje huku rumande tule bata maana kuna bata wamebaki.
 
Wadau,

Mtaalam mmoja wa kijeshi anasema, tabia fulani inapopandikizwa vya kutosha ndani ya kicha cha mtu, tabia pandikizi hugeuka na kuwa kama "Second nature" kwa mhusika. Kwa mfano anasema, mtu wa kawaida kabisa anavyojiunga na jeshi, hupandikiziwa tabia ya upiganaji na uvaaji wa magwanda katika kiwango ambacho tabia hiyo huwa ni kama "Second nature" kwa muhusika na huifurahia hali hiyo.

Kwa kuwa UKAWA wamepandikiziwa tabia ya kukimbia mijadala kwa kiwango ambacho tabia hiyo imekuwa kama "second nature" kwao, na kwa kuwa hivi karibuni inatarajiwa kwamba bunge litakutana tena kwa ajili ya kubadilisha sheria kadhaa kuhusu mchakato wa katiba mpya na kuboresha baadhi ya vifungu katika katiba ya 1977, Inatarajiwa kwamba watagoma tena na kuondoka zao.

Sasa kama watagoma kama kawaida; unashauri nini Kifanyike kati ya machaguo matatu ambayo yamekuwepo wakati wote.
1. Rais kuwaita ikulu?
2. Wabunge wanaotaka kuendelea (coalition of the willing ) kuendelea?
3. Mchakato wa marekebisho ya katiba 1977, usitishwe na tuendelee na yo kama ilivyo hadi hapo mpya itakapopitishwa?
Hawa ndio viongozi wa lile Tawi jipya la CCM linaitwa ACt
 
Back
Top Bottom