UKAWA Wanadharau Mahakama

UKAWA Wanadharau Mahakama

Buchanan

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2009
Posts
13,192
Reaction score
1,976
Wakuu.

Mahakama Kuu katika kesi ya kihistoria ya Saed Kubenea v. Attorney General, Misc. Civil Cause No. 28 of 2014 ilitamka wazi kwamba Bunge Maalum la Katiba halikufungwa na RASIMU YA WARIOBA na wala hawakulazimika kufuata yaliyokuwa ndani ya RASIMU hiyo, lakini ndugu zetu wa UKAWA bado hilo hawalioni! Wamekuwa wanatoa comments (hata humu JF) as if Bunge Maalum la Katiba lilifungwa na RASIMU YA WARIOBA! Hiyo si sahihi hata kidogo.

Sisemi kwamba Bunge Maalum la Katiba halipaswi kukosolewa lakini pale ambapo chombo pekee cha utoaji haki kinapotoa tafsiri ya kisheria lazima tafsiri hiyo iheshimiwe hadi hapo chombo hicho hicho kitakapotoa tafsiri nyingineyo! Ni vizuri hata namna upigaji kura ulivyofanyika na hata kura zilivyopatikana vikahojiwe Mahakamani na Mahakama hiyo ikitoa tafsiri basi tuiheshimu, hata kama itakuwa ni kinyume na maoni yetu.

Kinyume chake ni kudharau (contempt) chombo hicho hicho ambacho wao wenyewe walikimbilia kwenda kuwasilisha malalamiko yao.

Nawasilisha kwa mjadala zaidi.
 
Kweli ni vizuri akaweka wazi umri wake maana miropoko mingine inashangaza sana
 
si rahisi kwa binadamu aliyejidharau nafsi yake kuheshimu mamlaka zilizopo, UKAWA wameshadharau utu wao kama watanzania, hawaoni faida ya kuheshimu mamlaka zilizopo, hawa watu ni wa kupuuzwa toka mwanzo
 
Kilichofanyika na sita na vijisent ni sawa sawa dr upewe kazi ya kupunguza uzito mtu mwenye kilo nyingi badala ya kumfanyisha mazoezi apungue wewe unamkata kichwa alafu unasema ameshapungua kilo kumi ndicho alichofanya vijisent na sita
 
Kilichofanyika na sita na vijisent ni sawa sawa dr upewe kazi ya kupunguza uzito mtu mwenye kilo nyingi badala ya kumfanyisha mazoezi apungue wewe unamkata kichwa alafu unasema ameshapungua kilo kumi ndicho alichofanya vijisent na sita

Issue hapa ni dharau ya UKAWA dhidi ya maamuzi ya Mahakama!
 
Nadhani ndiyo maana wamekuuliza umri wako maana hoja yako haipo husemi nikwanjia IPI wamedharau mahakama

Pole sana kwa kutokuelewa au kutokutaka kuielewa mada!
 
Mahakama mbona ilishamaliza kazi siku nyingi sana na kuweka bayana kuwa bunge kazi yake inatakiwa ijadili rasimu peke yake na si vinginevyo
 
si rahisi kwa binadamu aliyejidharau nafsi yake kuheshimu mamlaka zilizopo, UKAWA wameshadharau utu wao kama watanzania, hawaoni faida ya kuheshimu mamlaka zilizopo, hawa watu ni wa kupuuzwa toka mwanzo

Walianza na Waasisi wa Taifa hili wakawaona sio kitu, wakawakejeli, wakawatukana, kisha wasivyokuwa na aibu wakakimbilia kwenye kaburi la Mwl kule Butiama...!
 
Mahakama mbona ilishamaliza kazi siku nyingi sana na kuweka bayana kuwa bunge kazi yake inatakiwa ijadili rasimu peke yake na si vinginevyo

Haaaa haaaaa, kumbe Kibatala na Marando ndivyo walivyowadanganya baada ya kupata aibu ya mwaka?
 
Back
Top Bottom