Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 24,940
- 26,796
Najaribu kutafuta hayo uliyosema kwamba mahakama iliyatamka:Wakuu,
Mahakama Kuu katika kesi ya kihistoria ya Saed Kubenea v. Attorney General, Misc. Civil Cause No. 28 of 2014 ilitamka wazi kwamba Bunge Maalum la Katiba halikufungwa na RASIMU YA WARIOBA na wala hawakulazimika kufuata yaliyokuwa ndani ya RASIMU hiyo, ...
1.Kuna mgongano mkubwa kati ya toleo la Kiswahili na Toleo la Kiingereza la kifungu cha 25 (2) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
2. Kwamba pamoja na mgongano huo, Sheria imekusudia kwamba Madaraka ya Bunge Maalum la Katiba yatatekelezwa kupitia Rasimu ya Tume ya M.y.K kama ilivyowasilishwa kwake.
3. Kwamba mamlaka ya BMK yana mipaka, na kwamba madaraka yake yanaongozwa na na kutekelezwa kupitia Rasimu. BMK linaweza kubadili na kuboresha mapendekezo yaliyomo katika Rasimu mradi tu maboresho yasiende kinyume na misingi iliyowekwa na kifungu cha 9 (2) cha Sheria ya M.y.K, kama ilivyokuwa pia kwa Tume.
4.Mahakama Kuu haina Mamlaka ya kuamua ni kiwango gani BMK inaweza kuboresha Rasimu kwani hilo ni suala la kisiasa, ingawa BMK inafungwa na kifungu cha 9 (2) cha Sheria ya M.y.K.