UKAWA wagomea mwaliko wa CCM

UKAWA wagomea mwaliko wa CCM

Mkuu si vema kufukua makaburi , ukiwekewa matokeo ya uchaguzi humu utakimbia mjomba , ccm ina watu wachache mno .
Wapinzani mnapuuza zoezi la kuongeza wanachama/wapenzi wenu kwasababu ya hiyo akili ya kudhani mna wapenzi wengi na kila chaguzi mnaibiwa kura. Shauri yenu mkuu.
 
Mbowe hataki kushuhudia Jakaya Kikwete akikabidhi Madaraka kwa Magufuli

Mbowe ni Mwenyekiti Chadema Kabla Jakaya hajawa Chairman lakini kamkuta na kamuacha sasa atakosaje kuona aibu
This is Very Pathetic
 
Msimamo ni jambo zuri sana wangeenda isingeleta maana yoyote
 
Siasa ni mchezo mzuri na ni Maisha ila kukiwa na usawa tu
 
Mbowe hataki kushuhudia Jakaya Kikwete akikabidhi Madaraka kwa Magufuli

Mbowe ni Mwenyekiti Chadema Kabla Jakaya hajawa Chairman lakini kamkuta na kamuacha sasa atakosaje kuona aibu

kwa hiyo unataka kusema nn labda?
 
Vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi vimesema havitahudhuria mkutano mkuu wa ccm utakaofanyika July 23 mjini dodoma licha ya kupata mwaliko .

Msimamo Huo imara ni muendelezo wa UKAWA kususia shughuli za viongozi na wabunge wa ccm tangu walipoanza kususia vikao vya bunge vilivyokuwa chini ya Naibu Spika ambaye ni Mwanasheria msaidizi wa serikali wa zamani na mbunge wa ccm wa mtelezo wa kuteuliwa na Rais Dk Tulia Ackson.

Chanzo - Mwananchi

MyTake - naunga mkono msimamo huu wa kishujaa , ccm walioko bungeni ni walewale watakaokuwemo kwenye mkutano huo , nyeusi haijawahi kuwa nyekundu .

CCM na polisi , UKAWA na wananchi .
Haaa haaa siasa sio uadui,
 
Kwani SHIBUDA hajaalikwa kipindi hiki.?

Au hana deal tena?
 
Endeleeni kususa nafikiri mwaka 2020 kwenye uchaguzi mtawaeleza wananchi kwa kipindi cha miaka 5 tumesusa mara kadhaa tunaombeni Kura zenu wananchi. Kazi ya UKAWA iliyobaki ni kutoa matamko yasiyotekelezeka na kususa
 
ukawa lazima wanaona aibu toka mfumo wa vyama vingi uanze CCM imeshabadilisha wenyeviti wanne pamoja anafuatia sasa.
lakini wenyeviti wa ukawa toka wameanzisha vyama wenyeviti walewale
 
Mlisusia vikao na futari ya waziri mkuu kisa yupo Dr Tulia. Lakini kwenye hafla ya kugawa Madawati mlihudhulia na Dr. Tulia akiwepo. Kuweni na misimamo msiwe kama k
 
Vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi vimesema havitahudhuria mkutano mkuu wa ccm utakaofanyika July 23 mjini dodoma licha ya kupata mwaliko .

Msimamo Huo imara ni muendelezo wa UKAWA kususia shughuli za viongozi na wabunge wa ccm tangu walipoanza kususia vikao vya bunge vilivyokuwa chini ya Naibu Spika ambaye ni Mwanasheria msaidizi wa serikali wa zamani na mbunge wa ccm wa mtelezo wa kuteuliwa na Rais Dk Tulia Ackson.

Chanzo - Mwananchi

MyTake - naunga mkono msimamo huu wa kishujaa , ccm walioko bungeni ni walewale watakaokuwemo kwenye mkutano huo , nyeusi haijawahi kuwa nyekundu .

CCM na polisi , UKAWA na wananchi .
Nimesikia Lowassa kajifungia analia akiona Magufuli akikabidhiwa chama ila Mbowe kaona aibu kwa kuminya demokrasia ndani ya chama huku akishuhudia ndani ya ccm demokrasia ikitamalaki km maji ya bahari ya Hindi
 
Mbowe hataki kushuhudia Jakaya Kikwete akikabidhi Madaraka kwa Magufuli

Mbowe ni Mwenyekiti Chadema Kabla Jakaya hajawa Chairman lakini kamkuta na kamuacha sasa atakosaje kuona aibu
Jamani, huwa napata taabu sana kutamka, 'Mwenyekiti Mbowe.' Huyu kwa jinsi alivyong'ang'ania uongozi wa cdm, ingefaa aitwe Sultani Mbowe, mwaonaje? Kila nikimwangalia jamaa, naona ukimwambia aachie kiti aweza dondosha machozi.
 
Mbowe hataki kushuhudia Jakaya Kikwete akikabidhi Madaraka kwa Magufuli

Mbowe ni Mwenyekiti Chadema Kabla Jakaya hajawa Chairman lakini kamkuta na kamuacha sasa atakosaje kuona aibu



Kweli hili sikuliwaza, asante kwa kunifungua
 
Nimesikia Lowassa kajifungia analia akiona Magufuli akikabidhiwa chama ila Mbowe kaona aibu kwa kuminya demokrasia ndani ya chama huku akishuhudia ndani ya ccm demokrasia ikitamalaki km maji ya bahari ya Hindi
Fomu za kugombea uenyekiti wa ccm taifa zishaanza kutolewa ?
 
Wananchi tuko bize na Magufuli,
Ameshusha kodi za korosho kutoka 20 hadi kodi tano tu.

Viva Magufuli.

Machadema na maukawa yakafie mbali huko


Mkuu akili umeweka mfukoni kwani hizo kodi 20 ziliwekwa na ukawa au ccm?
 
CCM na polisi, UKAWA na wananchi? Acha ndoto za asubuhi, CCM ina wapenzi wengi zaidi ya UKAWA. Ubaya wao siyo wapiga kelele kama wa Ukawa. Hamjifunzi na matokeo ya chaguzi zilizopita.


Chaguzi zenyewe zile za jecha kufuta matokeo au unazungumzia chaguzi zipi?
 
Back
Top Bottom