UKAWA sasa IKAWA?

Hivi huyu ni Mwanakijiji yule yule ninayemfahamu au account yake imeingiliwa? Siamini kwani kwa sasa amekuwa mtu wa siasa nyepesi nyepesi sana. Hivi ni kweli Mwanakijiji hafahamu kilichopo nyuma ya hao viongozi wa NCCR?

Swali la msingi la kujiuliza ni hili, makubaliano ya mgawanyo wa majimbo haukufanyika leo, siku zote hao viongozi walikuwa wapi kupinga au kutoa maoni yao kuboresha makubaliano yaliyofikiwa na m/kiti na katibu wao mkuu?

Majimbo yamegawanywa kabla ya muda wa kurudisha form NEC tarehe 22/09/2015, watu wamechukua form zikajazwa na kurudishwa. Kampeni zinaelekea kumaliza mwezi sasa leo wao ndio watoke waseme kuwa hawaridhishwi na mgawanyo wa majimbo? Mtu mzima mwenye akili timamu unayekubaliana na mitazamo ya hovyo kama hii tukuelewe vipi?
 
Too low Mwanakijiji, kwani pilipili usioila yakuwashia nini?

Kura yangu ni mabadiliko.

mkuu ni kumbushe hivi mbatia ni msemaji wa chadema au ni mwanachama wa chama gani.
 
Mzee Mwanakijiji, kwa sasa habari ni moja tu kwanza. Kuing'oa CCM madarakani, jambo amblo limekuwa humu kwa miongo kadhaa.

Iking'oka badi hayo mengine yatakuwa mepesi kabisa. Kumbuka yalisemwa mengi kwamba wasingeweza kufika hapa waliko leo lakini ona wamefika.

Ikasemwa akiondoka fulani na fulani itakuwa na negative impact na UKAWA kusambaratika na wafuasi wake kugawanyika kwa kiasi kikubwa. Lakini ina wameonfoka wale lakini no one cares!

Maelezo yako hayatii watu moyo wakati wanakaribia au wanaelekea kupata ushindi bali yanavunja nguvu jambo ambalo linakuweka katika kundi la maadui.
 
Mafanikio ya CCM si kubadilisha maisha ya watanzania,ila kuvuruga muungano wa watanzania ili iwe rahisi kuwatawala...safari hii watashindwa tu...to hell CCM!
 
Ngamia anapokaribia kufa, huwa anarusha mateke ya hatari san. Hakuna cha ajabu sasa kuwaona hata ''makamanda'' wakisalimu amri. Too late though.
 
Mzee akishabikia ccm simshangai coz watu wagumu kubadilika kifikira duniani ni wazee.
 

Zee lingine hili apa.
 

Nilikata tamaa Mbatia aliposema mnao wazoefu akawataja kina Mungai, Mgana, Masha, Mahanga na mimi nakuongezea Sumaye na Lowasa walioshiriki kwa takribani miaka 40 kati ya hiyo 54 ya uhuru.
 

Ww sifa unayo!
 

Kinachowaponza hamtaki kuelezwa ukweli.subiri baada ya oktoba utamwelewa mwanakijiji ambaye baadhi yenu mnasema anaishi ughaibuni wakati tuko nae huku uswahili.shame on you
 

Huyu jamaa anayejiita mwanakijiji hata sura yake hajawahi kuionyesha asituhangaishe .
 
Hahaha...huyu MM wa 2005, 2010 na 2015... kweli binadamu hasa sisi wa Afrika hata uishi Marekani miaka 50 bado tu utabaki kuwa na ubongo wa KIafrika.

unachosahau MM ni kwamba kwa sasa UKAWA hawana mamlaka au hawajashikilia gia ya mabadiliko, wanaohitaji mabadiliko haya ya kidemokrasia tena bila vurugu ni WaTanzania masikini wanaopata shida za CCM directly, ni Vijana wa Taifa hili ambao kwa sasa wamejua umasikini hausababishwi na Mungu bali sera mbovu na wezi wa serikalini, na wanamjua adui yao ni CCM maana ndie anaekua responsible...

Hata LOWASA akishindwa uchaguzi huu, bado haitaondoa idea ya kuhitaji mabadiliko vichwani mwetu...na wewe utakua sehemu ya Political Dinosaur ambao wamepoteza influence na heshima... unajificha kwenye kivuli cha "Taasisi" hata kufikia kusema wewe ni Institution mate wa Nyerere? haya ni matusi na sijui ni Nyerere yupi unamzungumzia.

Zile zama za 2005 ulipokua unaiunga mkono CCM na Kikwete tulikuwepo, na hata ulipoiunga mkono CHADEMA na UKAWA tulikuwepo, na hata sasa unapoiita DUBWASHA bado tupo...hii inaakisi wewe ni mtu wa namna gani, unayejificha katika vichaka na vivuli vinavyowaka moto...

Kile kidogo ulichobaki nacho hifadhi, kwa maana si muda utakua sawa na Lizaboni
 
Last edited by a moderator:

TOO LATE, TOO DESPERATE ! Bahati mbaya unadhani hatukuewi..... Ulituaminisha CCJ is the best party - hata kabla haijapata usajili. Ulitumia vigezo gani? Unachohofia UKAWA hakipo CCM? CCM leo hii raisi akichagua kiongozi yeyote wa ngazi lazima aangalie dini na kabila. Akichagua Muislamu, basi makamu mkristo, akichagua mkristo, makamu muislamu..hii ndo dubwasha unalolipenda. Mzee Mwanakijiji, tuambie lini CCM imegeuka nzuri na isiyo na mifarakano? Leo hii Waziri Mkuu kanuna, Makamu wa Raisi kanuna, Mshauri mkuu wa raisi kanuna...bado unataka kutuaminisha CCM wana umoja? We vipi Mkuu, au umefikia umri wa Mkapa kutojua nini uongee mbele ya kadamnasi? Spare UKAWA man, talk a balanced talk. Mbona huisemi CCM, umeng'atwa na kunguni nini?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…