UKAWA na Operation "Hakuna tume huru hakuna uchaguzi".

UKAWA na Operation "Hakuna tume huru hakuna uchaguzi".

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
24,150
Reaction score
56,463
Hapo zamani nilikuwa na mawazo ya kuwa chama kikisusia uchaguzi kinawanyima wanachama haki ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa, unafanya mpinzani wako kupita bila kupingwa, na yeye anafurahi kuwa peke yake, wengine wakawa wanasema "ukisusa wenzako wala" au "hakuna kususia shamba nguruwe".

Lakini baada ya kufanyika kwa chaguzi mbalimbali awamu hii mawazo yamegeuka kabisa nimebadili msimamo, sioni haki wanayopata wapiga kura kama maoni yao kwenye sanduku la kura hayaheshimiwi. Leo naungana na wale wenye mawazo ya kususia sijui kama nitakuwa sahihi ama la, nitaeleza.

Ni ukweli usiopingika kuwa chaguzi za awamu hii ni kiini macho tu, tofauti na chaguzi za awamu zilizopita, ingawa kulikuwa na wizi lkn angalau walijua kula na kipofu. Wizi wa kura wa awamu hii ni wa wazi kabisa wa nguvu, si rais, jeshi la polisi, NEC, viongozi mbalimbali wanaoona aibu kuiba, kwa matamshi na vitendo.

Pamoja na hayo yote CCM wanachukulia advantage kuona vyama vya upinzani kama CHADEMA na CUF bado vinaendelea kushiriki kwa lengo la kuwasindikiza na kuuhadaa ulimwengu kuwa Tanzania kuna demokrasia ya vyama vingi, kumbe chama ni kimoja tu na vingine ni wasindikizaji.

Hebu tujiulize, niwaulize wabunge niwaulize madiwani unashiriki uchaguzi ili iweje wakati unajua kabisa hautatangazwa mshindi, na rais ameshawaelekeza wakurugenzi hataki kuona mpinzani akitangazwa mshindi.

Hapo zamani (Jecha effect) nilijua kuwa tunashiriki uchaguzi na NEC hii hii mbovu ili baadaye tuionyeshe dunia kuwa Tanzania hatuna demokrasia ya kweli lkn sioni matokeo chanya au labda dunia haijali kinachoendelea nchini, sasa kama mbinu hiyo haisaidii kwanini tuendelee kuitegemea.

Hoja yangu ni kuwa, kama hakutakuwa na tume huru, wanachama wa upinzani hasa vyama vikubwa vya CHADEMA na CUF wasusie chaguzi zote zinazofuata ukiwemo ule wa 2020. No pain no gain.

Ianzishwe kampeni kubwa mapema kuwaelimisha wananchi kwa slogan ya "HAKUNA TUME HURU HAKUNA UCHAGUZI", "NO FREE ELECTORAL COMMISSION NO ELECTION".

Kuingia kwenye uchaguzi na tume hii, ni kuwapotezea wananchi muda wao bure, chama kupoteza resources bure kwa vile hakuna Mbunge wala Diwani yeyote atakayetangazwa kashinda hata kama atapata kura zote 100%.

Nina hakika once mkiamua kususia serikali haitapuuza, tumeona NEC walivyolalamika turnout ndogo kwenye uchaguzi uliopita, najua mwanzo CCM watakuja na kejeli lkn mkibaki firm impact yake kijamii siyo ndogo, (rejea NASA ya Odinga).

Kwa tume hii ninawahakikishia kuwa uchaguzi wa 2020 si CHADEMA wala CUF watakaokuwa na Mbunge hata mmoja bungeni.

Kwenye utawala huu wa Magufuli na NEC hii na polisi hii na wakuu wa mikoa hawa wanaoshangilia ushindi hadharani bila woga na aibu, mshiriki uchaguzi hamtaingia bungeni msishiriki uchaguzi hamtaingia bungeni, ni kunyoa au kusuka.

Waacheni CCM waandae uchaguzi wao wateue wagombea wao wajitangaze washindi wao waingie bungeni wao peke yao, liwe bunge la CCM perse, waingie mikataba wao, watunge sheria wao, najua kwa muda mfupi hawatabaki salama.

Tuanze na uchaguzi mdogo wa jimbo la Liwale - Lindi UKAWA wajitoe wasiweke mgombea pesa zake zikajenge ofisi ya chama hapo hapo Liwale, wakiweka watueleze ni kwa sababu zipi.

==========​
Mawazo huru ya mwanaJF Quinine
==========​
cc: #freemanmbowe
cc: #mashinji
cc: #maalimuseif
cc: #prof abdallahsafari
cc: #edwardlowassa
 
Naunga mkono hoja, kifo cha taasisi zetu kimetimia, hakuna taasisi inayoaminika tena. Watu wanafanya cheating bila woga wowote, kituo kina waliojiandikisha 40 wanatangaza 700!!, kuendelea kushiriki upuuzi huu ni kupoteza muda. Wasusie tutapata shida kwa muda lakini nina imani tutavuka salama.
 
Bila tume huru na katiba inayokubalika kwa wananchi hatutakuwa na sababu ya kuingia kwenye uchaguzi
Hapo zamani nilikuwa na mawazo ya kuwa chama kikisusia uchaguzi kinawanyima wanachama haki ya msingi ya kuchagua na kuchaguliwa, unafanya mpinzani wako kupita bila kupingwa, na yeye anafurahi kuwa peke yake, wengine wakawa wanasema "ukisusa wenzako wala" au "hakuna kususia shamba nguruwe".

Lakini baada ya kufanyika kwa chaguzi mbalimbali awamu hii mawazo yamegeuka kabisa nimebadili msimamo, sioni haki wanayopata wapiga kura kama maoni yao kwenye sanduku la kura hayaheshimiwi. Leo naungana na wale wenye mawazo ya kususia sijui kama nitakuwa sahihi ama la, nitaeleza.

Ni ukweli usiopingika kuwa chaguzi za awamu hii ni kiini macho tu, tofauti na chaguzi za awamu zilizopita, ingawa kulikuwa na wizi lkn angalau walijua kila na kipofu. Wizi wa kura wa awamu hii ni wa wazi kabisa wa nguvu, si rais, jeshi la polisi, NEC, viongozi mbalimbali wanaoona aibu kuiba, kwa matamshi na vitendo.

Pamoja na hayo yote CCM wanachukulia advantage kuona vyama vya upinzani kama CHADEMA na CUF bado vinaendelea kushiriki kwa lengo la kuwasindikiza na kuuhadaa ulimwengu kuwa Tanzania kuna demokrasia ya vyama vingi, kumbe chama ni kimoja tu na vingine ni wasindikizaji.

Hebu tujiulize, niwaulize wabunge niwaulize madiwani unashiriki uchaguzi ili iweje wakati unajua kabisa hautatangazwa mshindi, na rais ameshawaelekeza wakurugenzi hataki kuona mpinzani akitangazwa mshindi.

Hapo zamani (Jecha effect) nilijua kuwa tunashiriki uchaguzi na NEC hii hii mbovu ili baadaye tuionyeshe dunia kuwa Tanzania hatuna demokrasia ya kweli lkn sioni matokeo chanya au labda dunia haijali kinachoendelea nchini, sasa kama mbinu hiyo haisaidii kwanini tuendelee kuitegemea.

Hoja yangu ni kuwa, kama hakutakuwa na tume huru, wanachama wa upinzani hasa vyama vikubwa vya CHADEMA na CUF wasusie chaguzi zote zinazofuata ukiwemo ule wa 2020. No pain no gain.

Ianzishwe kampeni kubwa mapema kuwaelimisha wananchi kwa slogan ya "HAKUNA TUME HURU HAKUNA UCHAGUZI", "NO FREE ELECTORAL COMMISSION NO ELECTION".

Kuingia kwenye uchaguzi na tume hii, ni kuwapotezea wananchi muda wao bure, chama kupoteza resources bure kwa vile hakuna Mbunge wala Diwani yeyote atakayetangazwa kashinda hata kama atapata kura zote 100%.

Nina hakika once mkiamua kususia serikali haitapuuza, tumeona NEC walivyolalamika turnout ndogo kwenye uchaguzi uliopita, najua mwanzo CCM watakuja na kejeli lkn mkibaki firm impact yake kijamii siyo ndogo, (rejea NASA ya Odinga).

Kwa tume hii ninawahakikishia kuwa uchaguzi wa 2020 si CHADEMA wala CUF watakaokuwa na Mbunge hata mmoja bungeni.

Kwa utawala huu wa Magufuli na NEC hii na polisi hii na wakuu wa mikoa hawa wanaoshangilia ushindi hadharani bila woga na aibu, mshiriki uchaguzi hamtaingia bungeni msishiriki uchaguzi hamtaingia bungeni, ni kunyoa au kusuka.

Waacheni CCM waandae uchaguzi wao wateue wagombea wao wajitangaze washindi wao waingie bungeni wao peke yao, liwe bunge la CCM perse, waingie mikataba wao, watunge sheria wao, najua kwa muda mfupi hawatabaki salama.

Mawazo huru ya mwanaJF Quinine

cc: #freemanmbowe
cc: #mashinji
cc: #maalimuseif
cc: #prof abdallahsafari
 
Usemayo ni ya msingi na tunayaunga mkono hakuna haja ya kuingia kwenye uchaguzi wa kiini macho huu
Naunga mkono hoja, kifo cha taasisi zetu kimetimia, hakuna taasisi inayoaminika tena. Watu wanafanya cheating bila woga wowote, kituo kina waliojiandikisha 40 wanatangaza 700!!, kuendelea kushiriki upuuzi huu ni kupoteza muda. Wasusie tutapata shida kwa muda lakini nina imani tutavuka salama.
 
Bila tume huru na katiba inayokubalika kwa wananchi hatutakuwa na sababu ya kuingia kwenye uchaguzi
Tuanze na tume huru katiba itafuata, wapinzani wakiendelea kuingia kwenye uchaguzi huu wa kiini macho wanainufaisha CCM kwa siasa za ndani na kimataifa.

Wabunge wa upinzani ni msaada mkubwa kwa maendeleo ni kama jicho la pili la serikali, hebu turudi kwenye Bunge la chama kimoja tuone kama CCM itasalimika.
 
Tuanze na tume huru katiba itafuata, wapinzani wakiendelea kuingia kwenye uchaguzi huu wa kiini macho wanainufaisha CCM kwa siasa za ndani na kimataifa.

Wabunge wa upinzani ni msaada mkubwa kwa maendeleo ni kama jicho la pili la serikali, hebu turudi kwenye Bunge la chama kimoja tuone kama CCM itasalimika.
Nakuunga mkono kwa 100% hakuna sababu ya kuingia kwenye chaguzi za kuitengenezea ccm uhalali wa kutawala
 
Tume huru na katiba kwa sasa kuwezekana ni vigumu maana huyu jamaa hawezi kutoa gogo ambalo linamkata aweke panga lililonolewa sawasawa hawezi na wala hata weza kukubali icho na mbowe na chadema hawawezi kupambana peke yao bila sisi kuonyesha tunataka nn tutoke tudai mambo yanayotukera dada mange alijaribu tukamwacha kwe mataa,kama sisi hatuwezi kuwa wakali kupigania nchi yetu sasa tunawapa mzigo mkubwa sana vizazi vyetu na vitatushangaa sana
 
"Neno (Tume) yaani imetumwa, sasa kwanini useme iwe Huru"
Hebu tuacheni tusherehekee ushindi wetu acheni kutuzingua.
5741-1.gif

Mwita hebu testi huu mmea wa Kiabakari.
 
Mkuu umeongea point sana, huo ndio ukweli pamoja na kuwa hata hiyo kampeni ikianzishwa haitasaidia sana kwa sababu sa hivi ni marufuku kufanya mkutano wa kisiasa nje ya jimbo lako, na kama wewe sio mbunge/diwani huruhusiwi kufanya mkutano sehemu yoyote ile ndani ya Jamuhuri, ukianza kuhamasisha kupitia mitandao utashitakiwa kwa kosa la matumizi mabaya ya mtandao, kiufupi sa hivi hakuna njia yoyote ya busara inayoweza kutumika zaidi ya ubabe ubabe.
Viongozi wetu wa dini baada ya waraka zao za kuikosoa serikali sa hivi sijui wamefanywa nini, hatuwasikii tena wakikosoa au kusifia, ni kama wamesusa kushauri chochote kile.
 
Huyu mtu anastahili kuondolewa madarakani na Bunge hatufai hata kidogo.Ni bahati mbaya tu hatuna Bunge imara.
Nafikiri baada ya Chadema kujitoa kwenye chaguzi zilizokuwa zinawapotezea muda wajikite kuangalia namna ya kumuondoa huyu kwa kutumia jumuiya za kimataifa kama wanavyotaka kumuondoa Museveni wa uganda.
 
Back
Top Bottom