Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Ndugu Wananchi,

Mimi kama mdau wa siasa na mzalendo kwa nchi yangu naomba nitoe ushauri ufuatao kwa UKAWA pamoja na Lowassa. Najua kuna watu inaweza ikawa ngumu sana kuelewa point yangu, lakini wenye ufahamu na mambo ya siasa na mapinduzi wataona point yangu.

Huu ushauri wangu umezingatia hali ya uchumi wa watanzania ambayo imeendelea kuwa maskini huku viongozi wakizidi kutajirika sana (mfano familia ya Rais wa sasa). Naelewa pia kuna watu watakuja hapa na fikra ya ufisadi wa ndugu Lowassa na kwamba hafai kupokelewa UKAWA. Hivi hawa ukiwauliza waweze kuthibitisha huo ufisadi wa Lowassa wanao majibu? Na je ni nani ndai ya CCM ambaye ni msafi?

Je huyu Magufuli ni msafi kiasi gani? Ni kwa vipi tumesahau juzi taarifa za CAG jinsi alivyolidanganya Bunge na upotevu wa billions zaidi ya 500? na je si ni huyu huyu Magufuli ndiye aliyehusika kwenye sakata la uuzaji wa nyumba za serikali? akimuuzia girlfriend wake na kaka yake ambao hawakuwa watumishi wa serikali kinyume cha utaratibu?

Nauliza tena, je ni nani MSAFI ndani ya CCM? Jibu ni HAKUNA MSAFI CCM. Na kwa wale wanaotegemea kuona mabadiliko yoyote hasa ya kiuchumi chini ya kiongozi yeyote ndani ya CCM hao wanajidanganya. Kwa CCM hata uwe msafi kiasi gani ukishaingia utakuwa unafanya matakwa ya CCM ya kulindana hasa ya kulinda wenye pesa na si kwa ajili ya wananchi.

Kwa hakika CCM haipo kwa ajili ya wananchi, kwani chini ya CCM tangu Uhuru, hakika hatujapata nafuu yoyote japo tuna rasilimali nyingi kama madini, maziwa , mafuta na gesi sasa. Naomba wananchi wenzangu mfungue macho na kuona jinsi muswada wa gesi na mafuta ulivyopitishwa juzi kwa hati ya dharura ili kulinda maslahi ya watu na si wananchi.

Ni wakat sasa wananchi wajue kwamba ADUI yao mkubwa ni CCM na mfumo wake na si watu, kwani watu hata wawe wazuri kiasi gani, lkn akishaingia ndani ya CCM, huyo mtu kwisha habari yake.

Baada ya huo utangulizi, sasa naomba niongelee kilichonisukuma mimi kuchukua muda kuandika thread hii. Awali ya yote naomba niseme kwamba mimi sina chama lakini ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa. Na kwasababu natoka eneo moja na Magufuli, wengi wangetarajia mimi pia niwe kati ya watu wanaofurahia uteuzi wake.

Naomba niseme kwamba, kwanza Magufuli ni mtendaji mzuri pamoja na kwamba ana udhaifu wake lakini kwa ccm yeye kidogo ana nafuu. Hatahivyo, pamoja na utendaji wake kuwa na unafuu, lakini HATALETA MABADILIKO yoyote, kwani akishaingia kwenye uongozi, yeye naye ataishia kufanya kama chama kinavyohitaji.

Na kwa msingi huo, mabadiliko ya maana katika nyanja zote yataletwa na chama mbadala na si ndani ya CCM.

Hivyo basi, Ombi langu kwa UKAWA ni kwamba wampokee Lowassa kupitia CHADEMA na Lowassa apewe nafasi ya kugombea Urais kupitia UKAWA. Naomba nirudie tena, Lowassa apewe nafasi ya kugombea URAIS. Hii ndio njia pekee ya kuitoa CCM na kuleta mfumo mpya utakaoleta mabadiliko hapa Tanzania.

UKAWA, kama kuna mtu mwenye value added kwenye mchakato wa kumtoa mkoloni mweusi madarakani ni Edward Lowassa, na wakati ndio huu na mkiacha tu hii nafasi, basi mtaendelea kuwa wapinzani miaka nenda rudi na mbaya zaidi hata wabunge watapunguakwa kasi sana mwaka huu. Hakuna mtu yeyote anayeweza leta thamani kwenye UKAWA na kuipa Ushindi toka CCM mbali na Lowassa pekee.

Faida ni kwamba CHADEMA tayari kina msingi nchi nzima na wafuasi wengi sana. Lowassa naye ana back up ya watu wengi sana na hata baadhi ya viongozi wa CCM katika ngazi zote watakuja naye. Naomba ieleweke kwamba Lowassa anapoingia CHADEMA atakuta mfumo ambao nao uko tayari, kwahiyo atafanya kazi ndani ya huo mfumo, na hivzo mambo ya CCM hatakuwa na impact kwenye mfumo atakaoukuta CHADEMA na UKAWA.

Na ukizingatia mfumo wa CHADEMA unavyojali wananchi, hivyo watanzania tutafaidika sana hasa kiuchumi. Lowassa akiwa mgombea Urais wa UKAWA atasaidia sana hata majimbo mengi ya ubunge kwa Wana UKAWA.

Mapendekezo yangu kwa wagombea wa UKAWA ni huu hapa:

1. Lowassa agombee urais kupitia CHADEMA.

2. Prof. Lipumba agombee Umakamu wa Urais.

3. Dr. Slaa akagombee ubunge ili aje awe waziri mkuu.

NB1: Naomba ieleweke kwamba mpaka sasa majimbo ya CHADEMA hasa za maeneo wanakokaa wasukuma (Kanada ya Ziwa) kwa kiasi kikubwa yatarudi CCM kwasababu ya Magufuli kuwa msukuma. Asiyetaka kukubaliana na mimi asubiri October. Na kura za urais vivyo hivyo. Na kwa msingi huo, ni lazima CHADEMA na UKAWA wawe na target ya kura za nyanda za juu kusini, kusini, kati na kaskazini. Na watu wa kusaidia UKAWA kukusanya kura za kutosha katika maeneo hayo ni Lowassa (Kaskazini, Kusini, kati, na nyanda za juu kusini) na Lipumba hasa kanda za magharibi na Kusini.

Najua kuna watu watakuja na hoja hapa ya Muungano kuhusu nafasi ya urais na makamu wake. Hapa UKAWA walenge kuondoa mfumo wa CCM na hivyo wanatakiwa watu wenye ngu (influencial people). Na kwa kuzingatia hilo, kwa CUF ukiondoa Lipumba anakuja Hamad amabye anagombea Zanzibar. Na kwasababu hiyo, wana-UKAWA wa Zanzibar wakubali tu wagombea wote watokee Bara, kwani matunda ya mfumo wa UKAWA utawafaidisha wananchi wote.

NB2: Lowassa atasaidia pia urais wa Seif Hamad kwa upande wa Zanzibar, kwani kuna wtu kule ambao hawajakubaliana na maamuzi ya CCM ya kuwaondoa akina Bilal. Na pia Lowassa na Karume ni kitu kimoja.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba hii ndio nafasi pekee ya CCM kuondolewa madarakani. Na njia pekee ni kupitia kwa Lowassa na UKAWA. Chadema na UKawa kubalini huu ushauri na hakika watanzania tuko nyuma yenu, kwani tunaamini kwamba uchumi wa Tanzania utabailika kwa mfumo ulio nje ya CCM na CHADEMA na UKAWA wanaweza kutumia nafasi hii sasa ya kumkubali Lowassa ili tupate mabadiliko.

UKAWA mnatakiwa kuwa makini, acheneni na propaganda za watu wengi hapa JF na mkubaliane na hali halisi. Wakati ndio huu na mkiuachia basi watanzania wasahau mabadiliko kwa kipindi kirefu sana.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA.

Ahsanteni.
Ni mimi Mpenda nchi.
Lowassa aingie upinzani lakini awe Mbunge tu ili apewe uwaziri Mkuu achape kazi naomba Ukawa mchukue maoni ya wananchi
 
Naona huna nia njema na Lowasa.
Kwa maoni yangu UKAWA yatosha.
Ushauri wa bure kwa Lowasa: akapunzike, siasa kwake basi. Ya CCM ikimshinda kwenda kutangatanga uzeeni hakutamfikisha popote isipokuwa atajizolea aibu na kuporomoshwa zaidi.
Atapumzika either way, akiingia UKAWA au akibaki CCM. Bora apumzike baada ya kuwakwaza kidogo CCM!
 
Kwani Lowasa naye alitoka nje ya Bunge la Katiba?.... Kwa nini sasa asimame kwa tiketi ya Ukawa?

Sina hakika kama alitoka lakini jana kwenye mkutano wa CHADEMA,Monduli Ndg Bananga alisema anamkaribisha Lowassa ndani ya Chadema kwa kuwa mzee huyo anatafutiwa tuhuma ambazo sio za kweli na hata kwenye bunge la katiba, Mzee Lowassa hakuongea chochote maana hakubaliani na marekebisho ya kihuni yaliyofanywa na CCM.
 
Tafakarini upya tena kwa mapana yake.
Hizi ashki zenu zilizojitokeza sasa zitaisha mda si mrefu mtakapofungua macho yenu na kuangalia with High Definition eyes.
Luku Vere
 
wewe kwa kuwa ni ccm lazima useme hivyo kwa sababu unajua Lowasa ndio anaibeba ccm kwa yeye kuwa mwanachama wa ccm hata kama mnajifanya hafai kuwa rais lakini siku Lowasa atakapotangaza kuamia UKAWA ndio itakuwa mwisho wenu pamoja na Makufuli wenu kama unabisha mwambieni aame kama mtapona, CHADEMA lazima wamtake kwa sababu akiamia kwao ccm itakufa
Mkuu kwanza naomba nikuhakikishie mimi sio CCM!, ila kwa wengi humu usipokuwa CCM kwao lazima uwe Chadema, mimi sio CCM wala sio Chadema, sina chama.

Tatizo langu mimi ni kuwa mkweli too much!, baada ya CCM kumsimamisha JPM, then 2015 ni CCM tena na JPM ndiye rais wetu!. Upinzani hauna mtu wa kushindana na JPM!. Kama CCM ingemsimamisha Membe, then Lowassa akahamia UKAWA, upinzani ungeingia ikulu kama kumsukumiza mlevi!.

Pasco
 
Mimi sijui watakuja na sababu gani kwa uamuzi wa kumpokea Edward Lowassa. Lakini kwa vyovyote vile uamuzi huu ni lazima uchukuliwe with great precautions.

Hebu turudi nyuma kidogo mwaka 2000 kama sijakosea pale NCCR MAGEUZI kilipochukua maamuzi magumu kama haya ambayo CHADEMA inashuriwa kuchukua leo kumpokea mtu maarufu sana EL mithiri ya Agustino Lyatonga Mrema wa mwaka 2000 alipojiunga nao na wakampokea kwa mbwembwe nyingi.

Naogopa sana yasije yakakikuta CHADEMA kama kilivyoikuta NCCR Mageuzi kwani badala ya neema ilikuwa ni mwanzo wa kusambaratika kwa chama na kurudi nyuma hatua nyingi japo kilipata manufaa ya muda mfupi ya kuingiza wabunge wengi bungeni kwa sbb ya umaarufu wa mtu Huyo.

Natambua pia kuwa nyakati hazilingani na ni ukweli pia Mrema na Lowassa ni watu wawili tofauti na wenye hulka tofauti pia na hata umaarufu wao umejengwa ktk misingi tofauti, lakini muhimu sana upinzani ukajifunza tokana Na historia hii na ikumbukwe kuwa watu hawa wanafanana kwa kitu kimoja kikubwa kabisa, wote ni wana CCM wenye uchu wa madaraka!

Kiukweli binafsi sina tatizo na uamuzi wowote utakaochukuliwa na viongozi wetu juu ya aidha kumpokea EL au kutokumpokea ili mradi tu wajiridhishe pasipo hata chembe ya mashaka kuwa uamuzi huo utakuwa na manufaa kwa chama ya sasa na ya muda mrefu na baadae na si kuturudisha nyuma.

Aidha ni lazima kuwe na sababu rahisi kuelezeka na kueleweka kwa wanachama na wafuasi juu ya uamuzi huo wa kumpokea mtu aliye tayari alishajengewa taswira hasi mbele ya jamii kiasi ambacho japo ana ufuasi mkubwa lakini pia jamii kubwa inamwona kama ni mtu asiye msafi, asiye na maadili ya kiuongozi. Ni lazima hili liwe addressed kiukamilifu ili watu waelewe kisha watoe sapoti yao na kuvunja hoja za wapinzani wetu.

Tukumbuke pia kuwa CHADEMA hawa hawa waliwahi kumweka katika orodha ya watu wafisidi wa nchi hii kupitia "the list of shame" ya Dr W.P. Slaa ya viwanja vya Mwembeyanga mwaka 2007 km sijakosea. Sasa kwa hili ni sharti waje na maelezo ya kina Ku - reverse msimamo wao huo juu ya mtu huyu ili wanachama na wafuasi na jamii kwa ujumla ielewe na iwaunge mkono na kisha tusonge mbele kwa pamoja ili kuitoa CCM. Kwamba ni nini kimefanyika mtu huyu kawa msafi-tena hata kuwa mtu wa upande wao!!

Ipo kazi kwelikweli, lakini labda watafanikiwa na pia yeye mwenyewe EL kuuthibitishia umma kuwa,sivyo wapinzani wake wamfikiriavyo bali ukweli juu yake ni huu na huu na hivyo jamii ibadili mtazamo hasi juu yake!

Otherwise, tusisahau usemi huu, majuto ni mjukuu!
 
Lowassa aingie upinzani lakini awe Mbunge tu ili apewe uwaziri Mkuu achape kazi naomba Ukawa mchukue maoni ya wananchi

Naweza kukubaliana na wewe kwa kiwango kikubwa kwa sbb umaarufu wa Lowassa na wafuasi wake watakaoamua kumfuata ni wazi kuwa atakuwa msaada kiasi kikubwa kwa upinzani. Akifanya hivyo, kuna possibility ya 90% ya majimbo yote ya mkoa wa Arusha na Manyara na mikoa jirani ya hii kwenda upinzani.

Tatizo ni kuwa hakuna guarantee kuwa upinzani utashinda kiti cha urais japo akitumika kumnadi mgombea uraisi wa upinzani, kuna uwezekano mkubwa wa kushinda na hivyo assumption yako ya yeye kuja kuwa PM ika materialize.

However, ni lazima upinzani na bwana mwenyewe kwa pamoja wauthibitishie umma pasipo shaka kuwa hahusiki na tuhuma za ufisadi zinazomkabili ili kuondoa taswira hasi aliyojengewa na wapinzani wake mbele ya jamii ili sasa aaminike na apate sapoti pana na kubwa zaidi!!

Hiki ndicho kikwazo cha EL na ndicho kigugumizi cha upinzani kuchukua uamuzi wa moja kwa moja na wa mara moja kumpokea!!
 
Mkuu kwanza naomba nikuhakikishie mimi sio CCM!, ila kwa wengi humu usipokuwa CCM kwao lazima uwe Chadema, mimi sio CCM wala sio Chadema, sina chama.

Tatizo langu mimi ni kuwa mkweli too much!, baada ya CCM kumsimamisha JPM, then 2015 ni CCM tena na JPM ndiye rais wetu!. Upinzani hauna mtu wa kushindana na JPM!. Kama CCM ingemsimamisha Membe, then Lowassa akahamia UKAWA, upinzani ungeingia ikulu kama kumsukumiza mlevi!.

Pasco

Wewe ndo umeongea ukweli,CCM imeoza na CCM wenyewe walijua hilo na hapo ndipo wakazichanga karata na kumteua Maghufuli, kwanza kanda ya ziwa karbia wote wapo nyuma ya maghufuli kwenye issue ya uraisi, na kule ndo wapiga kura wengi walipo, robo tatu ya watanzania wapo kule, kuteuliwa kwa Maghufuli kumeshusha sana mvuto wa Lowasa (ila wengi humu JF hawajui hilo), sa hvi stori nyingi kule zimezagaa wakimuongelea Maghufuli kana kwamba ni Mungu wao, na leo atakuwa Furahisha yaani ni shiida, namshauri Lowasa atulie tu asije kufa kabla ya mda wake....!!!!
 
Aise nami naunga mkono...EL atatufaa kuangusha hili joka ccm,ijulikane kumpa nafasi si kwamba ukawa hakuna bright man.
 
Mkuu kwanza naomba nikuhakikishie mimi sio CCM!, ila kwa wengi humu usipokuwa CCM kwao lazima uwe Chadema, mimi sio CCM wala sio Chadema, sina chama.

Tatizo langu mimi ni kuwa mkweli too much!, baada ya CCM kumsimamisha JPM, then 2015 ni CCM tena na JPM ndiye rais wetu!. Upinzani hauna mtu wa kushindana na JPM!. Kama CCM ingemsimamisha Membe, then Lowassa akahamia UKAWA, upinzani ungeingia ikulu kama kumsukumiza mlevi!.

hata Makufuli kwa taarifa yako hana ubavu wa kushindana na Lowasa, kumbuka Makufuli amepata hiyo nafasi baada ya hasira za watu waliokuwa wanamtaka Lowasa kulipiza kisasi cha kumkataa Membe ambaye ndio lilikuwa chaguo la Kikwete. kama wewe ni mkweli lazima uone hivyo, haya tunayokuambia sisi ni habari ya ndani ya vikao sio ya barabarani wewe kwa kuwa huna chama huwezi kujua mambo ya ndani
 
mtoa mada una mapungufu kidogo ya kufikri na kujenga hoja, japo hujajipambanua kwa kina na umedai huna chama lakini andishi lako linaonyesha dhahiri kuwa wewe ni shabiki wa team wa LOWASA amabaye ana shutuma kibao za Rushwa na kashifa ya Richmond ndiyo inayo mutafuna popote pale atakapo enda lazima gamba la richmond litaendelea kumutafuna. Lowasa hafai kuiongoza nchi hii hata kama atapitia upinzani bado hafai na UKAWA hawapaswi kumupokea na kumupa nafasi hiyo.mimi ni mwana UKAWA damu damu niliye choshwa na mfumo wa ccm kwa kila kona hata asimamishwe nabii lakini akiwa ndani ya ccm atakuwa mwinzi.
KWA NINI LOWASA HAFAI KUWA KIONGOZI KWA CHAMA CHOCHOTE.
Loawasa hafai kwanza ana kashifa ya Richmond inamutafuna ambayo kashifa hiyo iliibuliwa na wapinzani ambao leo hii unamushauri Lowasa akajiunge nao wakati wapinzani kwa mda tofauti wamemtuhumu Lowasa.
pili mbinu alizo tumia Lowasa kutangaza nia ilikuwa imejaa ufisadi na Rushwa kwa kila kona na lengo la Lowasa ilikuwa ni kufanya kila awezalo kuingia ikulu, hili ni kosa kubwa ambalo Lowasa hafai kuwa kiongozi ndani na nje Ukawa
Team iliyokuwa imemuzunguka Lowasa wote wale wana kashifa mbali mbali za rushwa na ufisadi na walikuwa kwa pamoja kila kona wakati anatangaza nia je akija ukawa ataasafishika vipi?

UKAWA WAKIMPKEA BASI WATANZANIA WATAKOSA IMANI NAO.
UKAWA ndilo tumanini jipya la watanzania kwa ajiri ya ukombozi mpya na kumuondoa madarakani mkoloni mweusi ccm, itakuwa ni aibu kwa ukawa wamuchukue Lowasa na pia apewe nafasi ya juu ya kugombea uraisi, Lowasa ni mtu ambaye anafanya kila means kuhakikisha anashinda jambo ambalo linaweza ku coast ukawa na kuwapa nafasi nzuri ccm kuweza kuwachafua ukawa kwa kumupokea fisadi aliye tukuka, pili ukawa hawa hawa kwa nyakati tofauti wanasema ccm haifai na Lowasa ni mwa ccm je watatumia maji ya aina gani kumuosha Lowasa tatakate machoni mwa watanzania.
tatu UKAWA dhamila yetu kuu ni kumutoa ccm madarakani ambapo jambo hili linaneda kutimia mwezi wa kumi, hivyo lowasa hatufai

kama ccm imeoza tayari na lowasa ameoza maana na yeye ni zao la ccm tena la mda mrefu, ifike hatua tukumbuke historia inasemaje mwaka 1995 Nyerere alisema kuwa Lowasa hafai coz ni fisadi, je iweje leo hii lowasa apewe nafasi ndani ya UKAWA.
 
Naweza kukubaliana na wewe kwa kiwango kikubwa kwa sbb umaarufu wa Lowassa na wafuasi wake watakaoamua kumfuata ni wazi kuwa atakuwa msaada kiasi kikubwa kwa upinzani. Akifanya hivyo, kuna possibility ya 90% ya majimbo yote ya mkoa wa Arusha na Manyara na mikoa jirani ya hii kwenda upinzani.

Tatizo ni kuwa hakuna guarantee kuwa upinzani utashinda kiti cha urais japo akitumika kumnadi mgombea uraisi wa upinzani, kuna uwezekano mkubwa wa kushinda na hivyo assumption yako ya yeye kuja kuwa PM ika materialize.

However, ni lazima upinzani na bwana mwenyewe kwa pamoja wauthibitishie umma pasipo shaka kuwa hahusiki na tuhuma za ufisadi zinazomkabili ili kuondoa taswira hasi aliyojengewa na wapinzani wake mbele ya jamii ili sasa aaminike na apate sapoti pana na kubwa zaidi!!

Hiki ndicho kikwazo cha EL na ndicho kigugumizi cha upinzani kuchukua uamuzi wa moja kwa moja na wa mara moja kumpokea!!

SWALI

Lowasa ameomba kuingia Upinzani?
 
mawazo yako ni mazuri sana tunaungana na wewe kuwaomba viongozi wa UKAWA wafanye chini juu wampate Lowasa wakipuuza hayo mawazo hakutokuwa na njia nyingine ya kuitoa ccm madarakani, kwani kwa mikataba waliowekeana na nchi za nje hawatatupa hiyo nafasi tena
 
Point Muhimu hapa ni kumtoa kwanza nyoka ndani, vitu tutavipanga baada ya nyoka kuwa ametoka nje.

Angalia lakini huyo nyoka ni hatari akikuwahi umekufa. Chadema ni chama cha wezi hakutakuwa na ajabu kumpokea mliokuwa mkimuita mwizi,nia yenu sio kumkomboa Mtz bali kula kwa zamu. Kamwe hatudanyiki bora mwizi huyu mdokozi kuliko nyie majambazi mtaimaliza nchi kabisa na baadae kuanza kutuua
 
Angalia lakini huyo nyoka ni hatari akikuwahi umekufa. Chadema ni chama cha wezi hakutakuwa na ajabu kumpokea mliokuwa mkimuita mwizi,nia yenu sio kumkomboa Mtz bali kula kwa zamu. Kamwe hatudanyiki bora mwizi huyu mdokozi kuliko nyie majambazi mtaimaliza nchi kabisa na baadae kuanza kutuua. Hivi kwa akili yenu haswa ya bangi na viroba mnafikiria Lowassa anaweza kukubali kuwatumikia?
 
ACT acheni kupima upepo..kama mnamtaka Lowassa mchukueni tuu lakini hamna haja ya kumhusisha na chadema ili mpate feedback ya mawazo ya wananchi..makene alishaliweka hili suala wazi kabisa
 
Lowasa na UKAWA ni two immiscible solvents..Hawakai pamoja..Mmoja ni very polar na mwingine ni non polar

Lowasa ili ayeyuke kwenye UKAWA inabidi aloose polarity yake kwa kuitisha press na kueleza kinagaubaga nani mwenye Richmond na mchakato mzima ulivyokuwa.Aeleze ni deal ngapi amepiga akiwa serikalini na awataje wenzake na mbinu wanazozitumia.

Awataje wanasiasa walio nyuma ya wauza unga,wawindaji wa tembo,wauaji wa albino etc.Ataje mbinu wanazotumia CCM kuiba kura...Yani aseme kila kitu kwa ukweli wake ili waTZ waujue ukweli wa viongozi wao

Then aombe radhi kwa waTZ na kwa Mungu wake maana ufisadi walioufanya una uhusiano wa moja kwa moja/usio wa moja kwa moja na baadhi ya vifo vya watu hapa nchini na hapo ndio 'like will dissolve like'

Bila kufanya hivyo..UKAWA itakayompokea ijiandae kuanguka vibaya
 
Back
Top Bottom