Tukubaliane tu Lowassa alikuwa Mwanasiasa wa Pekee Sana, aligombea Urais akiungwa mkono na UKAWA na CCM!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,997
142,018
Ni vema kuyaangalia mazuri ya mtu, hayati Lowassa alikuwa Mwanasiasa wa Pekee Sana nchini Tanzania.

2015 aliwaunganisha watanzania kwenye Uchaguzi Mkuu kupitia UKAWA na kama angeshinda sasa tungekuwa na Siasa bora kabisa na Katiba Mpya tungeshaipata.

Rip Edward Lowassa
 
Kinachonishangaza ni CHADEMA kuchukua credits za Upepo wa Lowasa !!!.
Kudhani kuwa Idadi ya Kura zilizopatikana 2015 ni uwezo wao.
 
Ukishafariki hamna Baya Lako litasemwa kila ulilofanya utaonekana Shujaaa,Mwamba.

Binafsi namkubali lowassa sijui baya lake lolote, zaidi ya mazuri ikiwemo la Kulisha Monduli nzima Hasa sisi wanafunzi tuliokua tukienda kwake kujichotea maubwabwa siku ya birthday yake kila mwaka.

Tuliosoma MORINGE SOKOINE na shule jirani ndani ya MONDULI tunajua mazuri tu ya MZEE WETU hayo mengine tunayasikia kwenu tu ila hatuna ushahidi nayo.
 
Ni vema kuyaangalia mazuri ya mtu, hayati Lowasa alikuwa Mwanasiasa wa Pekee Sana nchini Tanzania

2015 aliwaunganisha Watanzania Kwenye Uchaguzi Mkuu kupitia UKAWA na kama angeshinda sasa tungekuwa na Siasa bora kabisa na Katiba Mpya tungeshaipata

Rip Edward Lowasa
Kama angeshinda. ………
Kwani Tibaijuka alimwambiaje 😅😅🙏
Ila naunga mkono mawazo yako!
🙏🙏
 
Edward Ngoyai Lowassa ni mwanasiasa wa Tanzania ambaye amehudumu katika siasa kwa muda mrefu. Ni kweli kwamba Lowassa amekuwa na historia ya kushiriki katika vyama mbalimbali vya kisiasa na alikuwa mgombea wa urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na baadaye kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Hapa ni muhtasari wa mchango wake wa kisiasa:

1. CCM:
- Lowassa alikuwa mwanachama wa CCM na aliwahi kushikilia nyadhifa mbalimbali serikalini, ikiwa ni pamoja na kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuanzia mwaka 2005 hadi 2008. Hata hivyo, alijiuzulu kama Waziri Mkuu baada ya kuhusishwa na kashfa ya Richmond.

2. Gombea wa UKAWA:
- Baada ya kujiuzulu kutoka CCM, Lowassa aliungana na vyama vya upinzani vilivyounda UKAWA (Umoja wa Katiba ya Wananchi). Alichaguliwa kama mgombea urais wa UKAWA katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

3. Mgawanyiko wa Maoni:
- Ugombea wake wa Urais kupitia UKAWA ulileta mgawanyiko wa maoni miongoni mwa wapiga kura na wanasiasa. Baadhi walimuona kama mwanasiasa mwenye uzoefu na uwezo wa kuunganisha upinzani, wakati wengine walikuwa na wasiwasi kuhusu historia yake na vyama vya zamani.

4. Historia ya Ushirikiano:
- Ushirikiano wa Lowassa na vyama tofauti na mifumo ya kisiasa unaweza kuonekana kama kipengele chake cha pekee. Hata hivyo, hii ilisababisha kutoelewana na hata kuvunjika kwa umoja wa UKAWA baada ya uchaguzi wa 2015.

Ni muhimu kuzingatia kwamba maoni kuhusu Lowassa yanaweza kutofautiana kulingana na mitazamo ya kisiasa na uzoefu wa kila mtu. Mchango wake wa kisiasa unaweza kuchambuliwa kwa namna mbalimbali, na tathmini yake inaweza kutegemea pia matukio ya kisiasa yaliyotokea katika nyakati tofauti.
 
Ni vema kuyaangalia mazuri ya mtu, hayati Lowasa alikuwa Mwanasiasa wa Pekee Sana nchini Tanzania

2015 aliwaunganisha Watanzania Kwenye Uchaguzi Mkuu kupitia UKAWA na kama angeshinda sasa tungekuwa na Siasa bora kabisa na Katiba Mpya tungeshaipata

Rip Edward Lowasa
Kwanini mnapenda kusifia wezi wa mali za umma?

Nyie ndio mnafanya mafisadi wajione ni watu muhimu kwenye jamii
 
Ukishafariki hamna Baya Lako litasemwa kila ulilofanya utaonekana Shujaaa,Mwamba.

Binafsi namkubali lowassa sijui baya lake lolote, zaidi ya mazuri ikiwemo la Kulisha Monduli nzima Hasa sisi wanafunzi tuliokua tukienda kwake kujichotea maubwabwa siku ya birthday yake kila mwaka.

Tuliosoma MORINGE SOKOINE na shule jirani ndani ya MONDULI tunajua mazuri tu ya MZEE WETU hayo mengine tunayasikia kwenu tu ila hatuna ushahidi nayo.
Ubwabwa ndo umekufanya umuone Lowasa ni shujaa?

Ndo maana vijana wetu siku hizi wamekuwa BWABWA
 
Ukishafariki hamna Baya Lako litasemwa kila ulilofanya utaonekana Shujaaa,Mwamba.

Binafsi namkubali lowassa sijui baya lake lolote, zaidi ya mazuri ikiwemo la Kulisha Monduli nzima Hasa sisi wanafunzi tuliokua tukienda kwake kujichotea maubwabwa siku ya birthday yake kila mwaka.

Tuliosoma MORINGE SOKOINE na shule jirani ndani ya MONDULI tunajua mazuri tu ya MZEE WETU hayo mengine tunayasikia kwenu tu ila hatuna ushahidi nayo.
Alikuwa ana bayaa mkuuu hata cc wa shulee ya msingi manyara ranch tulikulaa sana nyamaa za ng'ombe wakeee.

Rip lowasaa
 
Edward Ngoyai Lowassa ni mwanasiasa wa Tanzania ambaye amehudumu katika siasa kwa muda mrefu. Ni kweli kwamba Lowassa amekuwa na historia ya kushiriki katika vyama mbalimbali vya kisiasa na alikuwa mgombea wa urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na baadaye kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Hapa ni muhtasari wa mchango wake wa kisiasa:

1. CCM:
- Lowassa alikuwa mwanachama wa CCM na aliwahi kushikilia nyadhifa mbalimbali serikalini, ikiwa ni pamoja na kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuanzia mwaka 2005 hadi 2008. Hata hivyo, alijiuzulu kama Waziri Mkuu baada ya kuhusishwa na kashfa ya Richmond.

2. Gombea wa UKAWA:
- Baada ya kujiuzulu kutoka CCM, Lowassa aliungana na vyama vya upinzani vilivyounda UKAWA (Umoja wa Katiba ya Wananchi). Alichaguliwa kama mgombea urais wa UKAWA katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

3. Mgawanyiko wa Maoni:
- Ugombea wake wa Urais kupitia UKAWA ulileta mgawanyiko wa maoni miongoni mwa wapiga kura na wanasiasa. Baadhi walimuona kama mwanasiasa mwenye uzoefu na uwezo wa kuunganisha upinzani, wakati wengine walikuwa na wasiwasi kuhusu historia yake na vyama vya zamani.

4. Historia ya Ushirikiano:
- Ushirikiano wa Lowassa na vyama tofauti na mifumo ya kisiasa unaweza kuonekana kama kipengele chake cha pekee. Hata hivyo, hii ilisababisha kutoelewana na hata kuvunjika kwa umoja wa UKAWA baada ya uchaguzi wa 2015.

Ni muhimu kuzingatia kwamba maoni kuhusu Lowassa yanaweza kutofautiana kulingana na mitazamo ya kisiasa na uzoefu wa kila mtu. Mchango wake wa kisiasa unaweza kuchambuliwa kwa namna mbalimbali, na tathmini yake inaweza kutegemea pia matukio ya kisiasa yaliyotokea katika nyakati tofauti.
Hoi ni Chatgpt. Tell me an wrong
 
Hivi kumbe huyu fisadi naye ni hayati? Kwahiyo mwendazake ni mmoja tu!
 
Back
Top Bottom