UKAWA mtusaidie hili kabla ya tarehe 14

UKAWA mtusaidie hili kabla ya tarehe 14

Ufafanuzi mwingine...
Nyingine inaweza kuwa hii ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura katika uchaguzi huo: Home

Watanzania milioni 11,491,661 kati ya milioni 18,587,742 (asilimia 62) wamejiandikisha kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Jumapili ijayo.
Mikoa ya Katavi na Kagera imefanya vizuri kwa kuandikisha wapigakura wengi zaidi huku mikoa ya Dar es salam na Kilimanjaro ikiandikisha idadi ndogo.

Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa uchaguzi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Khalist Luanda, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Luanda alisema Watanzania hao ni sawa na asilimia 62 ya walioandikishwa wanatokana na taarifa za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ambayo yalionyesha kwamba asilimia 40 ya Watanzania wote wana umri kuanzia miaka 18 na kuendelea.

Akizungumzia kuhusu mikoa iliyofanya vizuri, alisema Katavi umeandikisha wapigakura asilimia 79 wakati Kagera ni asilimia 78.

Kwa mujibu wa Luanda, mikoa iliyoandikisha wapigakura wachache ni Dar es Salaam asilimia 43 na Kilimanjaro asilimia 50.

Luanda alibanisha kuwa Halmashauri zilizovuka lengo ni ya Mji wa Mpanda(107%) na Mji wa Babati (101%) wakati zilizoandikisha kwa asilimia ndogo ni Kilindi (21%) na Same (22%).

"Katika uchaguzi huo karatasi za kupigia kura zitaandaliwa na Halmashauri husika na ambayo itakuwa sifa ya jina la mgombea, jina la chama, nembo ya chama na Nembo ya halmashauri na ingizo jipya ni Nembo ya Chama ili kuwasaidia wale wasiojua kusoma," alisema Luanda.

.....................




https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-uchaguzi-serikali-za-mitaa.html#post11378108
 
Umekuja mzima mzima hujifichi hahahaha!! Ukawa wamewashika pabaya hamchomoki.


Ngoja nikuelimishe Nuru.

UKAWA sio chama. Wanachokifanya ni kukubaliana ni mgombea kutoka chama gani anayekubarika sana eneo husika. Then huyo ndio anagombea nafasi tajwa, akikiwakilisha chama chake na wanachama wa Vyama vingine (isipokuwa CCM) wanahamasishwa wampigie kura huyo. Kwa kifupi inakuwa mpambano kati ya CCM na ''UKAWA'' ili kuepusha kura za Upinzani kugawanywa endapo kila chama kingesimamisha mgombea wake.

Pole kwa kutokujua hili. Now you know. Mambo ya ''umekuja mzima mzima'' sijui yanatoka wapi
 
suala hili iko iv ni kumnyima kura mgombea wa ccm. mgombea chadema, nccr, nld na cuf ruksa kuwapigia kura kwa sababu maeneo mengine chadema na cuf wana nguvu na wakati mwingine nccr basi wachuane apatikane mkali wa ukawa hapo nadhan nimeeleweka
 
Good! Naona umeamua kuwa neutral. Umeepusha mengi ahsante kura yako piga kwa ukawa.
 
Pamoja na hayo ccm hamzimalizi dakika90 lazima muombe pooo
 
Wewe ni darasa la ngapi kama mwanao wa darasa la tano anakuzidi kufikiri?
 
Tunaomba mtusaidie tuwaambie ndugu zetu ili wasibabaike siku ya kupiga kura uchaguzi wa mitaa ..Iko hivi, mmeungana sawa lakini watu wanauliza inamaana hata kwenye makaratasi ya kura vitaonekana vyama vyote vya ukawa ama kitakuwepo chama kimoja na mgombea mliyempitisha kama wa CUF ama CHADEMA ?

Mmeliwekaje hili ili tujue mapema siku tunaenda tusianze kuhangaika.

Ni kwamba kila wilaya na halmashauri imeandaa ballot paper zenye nembo ya vyama vyote.vyenye usajili na wewe kama ni mwa:thumbup::thumbup:na ukawa unachotakiwa kufanya ni kuangalia nembo ya chama cha mwanaukawa anayegombea katika eneo lako na kupiga kura yako kumchagua.
 
Weka salama ya (v) kwa mgombea wa chadema au cut au nccr mageuzi au nrd chakuzingatia ni usiweke salama ya (x) kwa usiempenda acha kama palivyo.kumbuka kumbuka kumuwekea salama ngombe aliyeomba nafasi kama m/kiti au mjumbe
 
Back
Top Bottom