Mtazamo wangu uchaguzi serikali za mitaa

Mtazamo wangu uchaguzi serikali za mitaa

johnmashilatu

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2010
Posts
1,213
Reaction score
1,620
Napendekeza kuanzishwe "uzi" (nakosa jina lake) maalum ambao utakuwa mahususi kwa ajili ya taarifa mbalimbali zinazohusu uchaguzi wa serikali z amitaa mbao utafanyika nchini kote Jumapili ya Desemba 14 mwaka huu.

pamoja na kurahisisha upatikaaji wa taarifa katika eneo moja, uzi huo utasaidia watu ambao watakuwa wakifanya marejeo ya uchaguzi wa serikal za mitaa katika siku za baadaye.

taarifa zote khusu uchaguzi huo zipatikane kwenye eneo moja ambako wenye nia ya kuzipata waende huko hasa tukiingatia kuwa uchaguzi huu unafanyika katika wakati ambako watanzania wengi hivi sasa wanatumia simu ambazo zinauwezo wa kutoa na kupkea taarifa za aina mbalimbali.

wadau wa jf jumapili kila mmoja akitahidi kila atakapo kuwa atujuze kinachoendelea ili kuwawezesha wadau kufahamu yanayojiri kwenye uchaguzi huo

hii haitatulazimu kusubiri "vyombo vya habari" vitupatie taarifa kwa kuchelewa au pangine baada ya kuhaririwa kutokana na sera ya chombo husika. Habari zipatikane hapa hapa

Nawasilisha
 
nadhani ni sahihi. JF wafanye ivyo maana hata wakati wa Bunge la ESCROW waliturushia LIVE!
 
Kama ndivyo tuanze kutupia vile tunavyofahamu, kama kinachoendelea hapa mwanza ambapo katika kata ya Kirumba UKAWA wameshindwa kukubaliana hivyo kila chama katika uchaguzi huu unaofanyika wakati kukiwa na urahisi wa kuwepo kwa vipaza sauti, kina mgombea wake.
 
Nyingine inaweza kuwa hii ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura katika uchaguzi huo: Home

Watanzania milioni 11,491,661 kati ya milioni 18,587,742 (asilimia 62) wamejiandikisha kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Jumapili ijayo.
Mikoa ya Katavi na Kagera imefanya vizuri kwa kuandikisha wapigakura wengi zaidi huku mikoa ya Dar es salam na Kilimanjaro ikiandikisha idadi ndogo.

Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa uchaguzi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Khalist Luanda, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Luanda alisema Watanzania hao ni sawa na asilimia 62 ya walioandikishwa wanatokana na taarifa za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ambayo yalionyesha kwamba asilimia 40 ya Watanzania wote wana umri kuanzia miaka 18 na kuendelea.

Akizungumzia kuhusu mikoa iliyofanya vizuri, alisema Katavi umeandikisha wapigakura asilimia 79 wakati Kagera ni asilimia 78.

Kwa mujibu wa Luanda, mikoa iliyoandikisha wapigakura wachache ni Dar es Salaam asilimia 43 na Kilimanjaro asilimia 50.

Luanda alibanisha kuwa Halmashauri zilizovuka lengo ni ya Mji wa Mpanda(107%) na Mji wa Babati (101%) wakati zilizoandikisha kwa asilimia ndogo ni Kilindi (21%) na Same (22%).

"Katika uchaguzi huo karatasi za kupigia kura zitaandaliwa na Halmashauri husika na ambayo itakuwa sifa ya jina la mgombea, jina la chama, nembo ya chama na Nembo ya halmashauri na ingizo jipya ni Nembo ya Chama ili kuwasaidia wale wasiojua kusoma," alisema Luanda.

Alivionya vyama vya siasa vinavyotoa vitisho kwa wagombea kuacha vitendo hivyo, badala yake viwahamasishe wapiga kura wao kujitokeza kwa wingi kupiga kura.

Alisema, vituo vya kupiga kura vitafunguliwa saa mbili asubuhi na kufungwa saa 10 jioni huku akiwaasa wapiga kura kufika Kwa wakati vituoni kwani wale watakaochelewa watapoteza fursa hiyo.

Kuhusu idadi ya wagombea waliopita bila kupingwa, Luanda alisema bado wanajumlisha na idadi hiyo na itatolewa wakati wa kutangaza matokeo ya ujumla baada ya uchaguzi huo.

Alisema pia bado wanakusanya taarifa za mapingamizi yaliyopita na yaliyokataliwa na yatatolewa katika matokeo ya ujumla
 
Back
Top Bottom