UKAWA kugomea Kamati za Bunge

UKAWA kugomea Kamati za Bunge

Watanzania sasa tupunguze UBINAFSI mimi nauona umeenea kwa kila mtu, watu hatuaminiani kabisaaaaa!

Asanteni
hivi unaanzaje kuwaamini wanaccm ? utakuwa na roho ngumu sana !
 
Wewe mtoa mada unaonekana umeandika tu kihisia ili upate popularity ya wanalumumba wenzio hapa jamvini. Ni hivii:

-Kwanza hujaweka exact source ya mada hii,lakini pia hujasema ni kwasababu zipi hao wabunge wazipinge nafasi hizo. Mtu mwenye weledi na utaalamu na zaidi uzoefu katika field flan anastahili aelekezwe huko huko ili ashuhulike vizuri ipasavyo kwa maslahi ya taifa.

Viongozi wa CCM wamewaplace wabunge wao ktk nafasi hizo kwa maslahi yao na hilo halina ubishi. Ukitaka kugundua hilo angalia maeneo ya utaalam na uzoefu wao then linganisha na nafasi walizopewa.
 
wabunge walienda bungeni kwa ajili ya kamati au kuwakilisha wananchi hizo sababu ni za kijinga kama kila mbunge anajiamini anastahili kuwa bungeni sioni sababu ya kugomea kamati anayopangwa
tatizo ukawa na uchache wao wanafikiri wanaweza kumburuza spika wataisoma namba hadi 2020
 
Ati nini? Waliweka mpira kwapani? Mbona juzi mbowe aliwashangaa wabunge wa CCM walipoweka mpira kwapani wakati wa uchaguzi wa Meya wa Kinondoni?
 
Ni aina ya uandishi lakini nafikiri mleta mada umekosea sana! Hujui kwanini wamegomea lakini umejaribu kuingiza fikra zako za ufitini kati yao kwa muundo wa maswali "je wabunge wa ukawa walioteuliwa kwenye kamati hiyo ya PAC hawana akili na sio watendaji ? Athari ya muundo huu ni kuwafanya watu wajadili zaidi fikra zako ambazo kimsingi sio njema kuliko kutaka kupata uhalisia wa jambo lenyewe. Niungane nawe kuwashangaa wabunge wa UKAWA kama kweli wote walichagua kamati ya PAC!!! Hivi hata Lisu, Mdee au Mnyika waliomba kuwa katika kamati ya PAC??? Nimshangae pia spika kama amempanga Mnyika au Lisu kwa mfano kwenye kamati ya maendeleo ya jamii kwa kuwa wanafani zao; hivyo naungana na wabunge wa UKAWA kugomea uteuzi huo kwa sababu kukosea kwao kuchagua hakuhalalishi au mpa mamlaka spika ya kuwapangia wabunge kiholela bila kufuata taaluma zao au weledi wao.
Kama wana fani zao watoke bungeni warudi kwenye fani zao....hivi Mnyika,Kubenea,lema na Profesa J wana fani gani?
 
Inashangaza sana kuona wabunge wetu tunaowaamini wa ukawa Jana kugoma kuingia ktk kamati walizoteuliwa kwa kudai kuwa sizo walizozitaraji,cha kuchekesha zaidi Mh kubenea baada ya kuona amepangwa ktk huduma za jamii akakasirika na kusikika akisema haiwezekani apangwe huko,kubenea alitarajia atapangwa PAC kitu ambacho kimemkasirisha sana hiyo jana,cha kujiuliza tu kwanini ukawa wagome?

Walijipangia nini ktk nia zao?kwa sheria za bunge PAC lazima iongozwe na mpinzani,je wabunge wa ukawa walioteuliwa kwenye kamati hiyo ya PAC hawana akili na sio watendaji?kwanini kina kubenea na wenzao wasiwaamini wabunge wao?

Sio bure ukawa walikuwa na nia ovu,hakuna hata mbunge mmoja aliejaza kamati alioitaka kisha akapangwa huko,safari hii ni tafauti kabisa,na ukawa takriban wote hakuna aliejaza kamati nyengine zaidi ya PAC na maliasili na utalii,nishati na madini.

Poleni sana kwa kukosa ulaji mlioutarajia pigeni kazi tumewachagua mkatuwakilishe,na mwaka huu mkigoma mara tatu tu unafutiwa ubunge.
wanataka kamati za kutaka kupewa rushwa kwa vizingizio vya kuopoa eti uozo katika taasisi hizo
 
Nawaunga mkono wabunge wote wa UKAWA kwa hatua hiyo.

Haiwezekani kamati ya PAC kwa mfano spika amejaza wabunge wa CCM kibao.
Kama sio makusudi ni nini??

Wakati huo huo kamati ya kilimo, mifugo na uvuvi ndo amejaza wabunge wa upinzani.

Tatizo nini sasa hapo?
 
#Kule kwetu, nakupongeza kwa uchambuzi wako dhidi ya mleta mada kwenye comment yako na 23. Mwandishi hakuqeka source, hakuweka sababu kwa nn wasusie, hakuwahoji wala hakuhoji spika wala katibu. Habari haiandikwi vile, rudi shule ya msingi ujifunze kk!
 
Wabunge wa kawa wasingefanya hivyo tusinge chukua muda kufikiri zaidi! Wametutafakarisha zaidi kuhusu uteuzi huu.
 
.....wana hoja ya msingi spika anataka kuwapangia wenyeviti wa PAC na kamati ya serikali za mitaa
 
Nawaunga mkono wabunge wote wa UKAWA kwa hatua hiyo.

Haiwezekani kamati ya PAC kwa mfano spika amejaza wabunge wa CCM kibao.
Kama sio makusudi ni nini??

Wakati huo huo kamati ya kilimo, mifugo na uvuvi ndo amejaza wabunge wa upinzani.

Kwenye hio kamati ya PAC huwa inakuwa na wajumbe wangapi? Je akidi inakuwaje?

Kilimo na mifugo ndio uti wa mgongo wa taifa - kupitia wapinzani tunataka kuona mifugo, kilimo na uvuvi vinatutoa, kamati zingine majungu na unafiki tu.
 
Ndicho walichobakiza kugoma kugoma kugoma , itachukua muda mrefu sana wapinzani kuaminiwa na kupewa nchi. Wamekubuhu kwa Unafiki pumbavu sana[/QUOTE

U]
[QUOTE="bdo, post: 15154951, member: umenielewa.e hio kamati ya PAC huwa inakuwa na wajumbe wangapi? Je akidi inakuwaje?

Kilimo na mifugo ndio uti wa mgongo wa taifa - kupitia wapinzani tunataka kuona mifugo, kilimo na uvuvi vinatutoa, kamati zingine majungu na unafiki tu.[/QUOTE]

Kama unafahamu majukumu ya PAC,utakuwa umenielewa
 
Tatizo nini sasa hapo?

Majukumu ya PAC unayafahamu lakini?

Kwa namna wanavyokuwa na kuenenda wabunge wa CCM ni dhahiri kamati hii itakuwa butu na haitatimiza majukumu yake ipasavyo kama hawataweka ushabiki wao pembeni na kufanya kazi kwa maslahi ya Taifa
 
ku
K


Kama mlipanga kuwaburuza sasa mtakiona cha mtemakuni nyie ccccccccm, kama mlijipangia kivyenu na kuweka wadhaifu ili mambo yenu yasonge mbele kilaini huu si wakati wake. tunataka usawa na si vinginevyo. Bunge ni la wooote si lenu na marafiki zenu
kumbe kuna wabunge dhaifu upinzani tulikuwa hatujui. !! ni ajabu na kweli. sasa kwa nini wananchi waliwachagua? ? napendekeza wajiuzuru kama wanakubali wao ni dhaifu kwa hiyo ni mizigo
 
Hivi huko PAC sijui maliasili na utalii, nishati na madini kuna nini hadi kila mbunge atake kupangwa huko?
kuna ulaji mzee kwani hujui ? jamaa wanataka wapige hela mpaka kieleweke
 
Kwenye hio kamati ya PAC huwa inakuwa na wajumbe wangapi? Je akidi inakuwaje?

Kilimo na mifugo ndio uti wa mgongo wa taifa - kupitia wapinzani tunataka kuona mifugo, kilimo na uvuvi vinatutoa, kamati zingine majungu na unafiki tu.
Nimeipenda comment yako!
Kimsingi wapinzani hawana ubunifu, kamati kama hizi za kilimo, huduma za jamii ndizo walipaswa watu kuzigombania kwa maana mnakaa na kufikiri pamoja na serikali!
Haya ndiyo matatizo ya msingi ya watanzania, hapa ndipo maendeleo yanapolengwa, watanzania wanatamani kuona wanapata nafuu ktk maeneo haya lkn wabunge wanataka kuwepo ktk kamati moja tu! Yes usimamizi wa pesa za umma ni muhimu lkn ubunifu katika uzalishaji na kutatua matatizo ya msingi ya wananchi nalo lina umuhimu namba 1.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom