Nimeipenda comment yako!
Kimsingi wapinzani hawana ubunifu, kamati kama hizi za kilimo, huduma za jamii ndizo walipaswa watu kuzigombania kwa maana mnakaa na kufikiri pamoja na serikali!
Haya ndiyo matatizo ya msingi ya watanzania, hapa ndipo maendeleo yanapolengwa, watanzania wanatamani kuona wanapata nafuu ktk maeneo haya lkn wabunge wanataka kuwepo ktk kamati moja tu! Yes usimamizi wa pesa za umma ni muhimu lkn ubunifu katika uzalishaji na kutatua matatizo ya msingi ya wananchi nalo lina umuhimu namba 1.
It's just watching expenditures, na wanainga'ang'ania PAC kwa ajili kick ya kisiasa, ila wanastahili kutuinyesha ubunifu zaidi kwenye hizo kamati za uzalishaji - kilimo, mifugo, uvuvi ambazo zinawahusu watu wengi zaidi. Naona kwa kulilia PAC ipo kibinafsi zaidi maana kamati zote za bunge zipo sawa na hakuna mbunge bora zaidi ya mwenzake.Majukumu ya PAC unayafahamu lakini?
Kwa namna wanavyokuwa na kuenenda wabunge wa CCM ni dhahiri kamati hii itakuwa butu na haitatimiza majukumu yake ipasavyo kama hawataweka ushabiki wao pembeni na kufanya kazi kwa maslahi ya Taifa
Kwenye hio kamati ya PAC huwa inakuwa na wajumbe wangapi? Je akidi inakuwaje?
Kilimo na mifugo ndio uti wa mgongo wa taifa - kupitia wapinzani tunataka kuona mifugo, kilimo na uvuvi vinatutoa, kamati zingine majungu na unafiki tu.
Wabongo Kwa ushabiki!wabunge walienda bungeni kwa ajili ya kamati au kuwakilisha wananchi hizo sababu ni za kijinga kama kila mbunge anajiamini anastahili kuwa bungeni sioni sababu ya kugomea kamati anayopangwa
tatizo ukawa na uchache wao wanafikiri wanaweza kumburuza spika wataisoma namba hadi 2020
Sisi wananchi tunachotaka kazi na maendeleo baassi. Mambo ya midomo. fijo, mahakamni hatutaki!!! Hapa ni Kazi tu sio ubabaishaji na visingizio kibao!K
Kama mlipanga kuwaburuza sasa mtakiona cha mtemakuni nyie ccccccccm, kama mlijipangia kivyenu na kuweka wadhaifu ili mambo yenu yasonge mbele kilaini huu si wakati wake. tunataka usawa na si vinginevyo. Bunge ni la wooote si lenu na marafiki zenu
Pole sana Movich boy. Wasingekuwa sawa Kubenea mwenye elimu ya hapa na pale asingepata Ubunge. My point tunachotaka wananchi si mbwembwe zozote abli na kazi tu na maendeleo endapo yataletwa na Kubenea mwenye elimu ya hapa na pale sawa , endapo yataletwa na Prof. sawa waht we want ni kazi na commitment ya wabunge period!Mwana, kwa comment hii siamini kama nawe ni great thinker na zaidi naona kabisa umevamia jukwaa ambalo sio saizi yako hivyo nakushauri kwa wembamba wa akili yako kama sindano na udogo wa fikra zako kama jina lako MWANA it is better urudi fasta facebook kwani naamini huko ndio kwako huku umepotea njia. Siamini kwa mtu mwenye kufikiri vizuri anaweza akasema wabunge wote ni sawa HAPANA wabunge wanatofautiana sana hasa kuanzia upatikanaji wa ubunge wao (MAJIMBO, VITI MAALUM na UTEUZI WA RAISI), wanatofautiana elimu na weledi (KUJUA KUSOMA NA KUANDIKA, DARASA LA SABA, ELIMU YA JUU PhD, Prof? wanatofautiana uzoefu wa shughuli za kibunge (Kipindi kimoja, viwili, vitatu NK), wanatofautiana uwezo wa kifra na kujenga hoja (Tundu Lissu + Deo Sanga, Mnyika +Lusinde, Zitto+Assumpter Mshama)
ku
kumbe kuna wabunge dhaifu upinzani tulikuwa hatujui. !! ni ajabu na kweli. sasa kwa nini wananchi waliwachagua? ? napendekeza wajiuzuru kama wanakubali wao ni dhaifu kwa hiyo ni mizigo
Najua tunataka maendeleo, maisha bora na mambo kama haya , Lakini si kwa staili ileile ya kihafidhina mkuu. Kila mtu anastahili kupata anachostahili mwingine. Sjui kama umenipata!!! wabunge wetu wanayo stahiki sawasawa na ile ya wale wa ccm, sasa kama umefuatilia kwa karibu kilichoanza pale mjengoni ni ama kuna mtoto wa tumboni na wa mgongoni wakati mama yetu ni mmoja.Sisi wananchi tunachotaka kazi na maendeleo baassi. Mambo ya midomo. fijo, mahakamni hatutaki!!! Hapa ni Kazi tu sio ubabaishaji na visingizio kibao!
Fani ya Mnyika ni nini kaka?Ni aina ya uandishi lakini nafikiri mleta mada umekosea sana! Hujui kwanini wamegomea lakini umejaribu kuingiza fikra zako za ufitini kati yao kwa muundo wa maswali "je wabunge wa ukawa walioteuliwa kwenye kamati hiyo ya PAC hawana akili na sio watendaji ? Athari ya muundo huu ni kuwafanya watu wajadili zaidi fikra zako ambazo kimsingi sio njema kuliko kutaka kupata uhalisia wa jambo lenyewe. Niungane nawe kuwashangaa wabunge wa UKAWA kama kweli wote walichagua kamati ya PAC!!! Hivi hata Lisu, Mdee au Mnyika waliomba kuwa katika kamati ya PAC??? Nimshangae pia spika kama amempanga Mnyika au Lisu kwa mfano kwenye kamati ya maendeleo ya jamii kwa kuwa wanafani zao; hivyo naungana na wabunge wa UKAWA kugomea uteuzi huo kwa sababu kukosea kwao kuchagua hakuhalalishi au mpa mamlaka spika ya kuwapangia wabunge kiholela bila kufuata taaluma zao au weledi wao.
Kwani unaanzeje kuwaamini ukawa?Toka lini uliwaamini ukawa???
Kama unavyoamini kwamba ukiwa gizani ili uone unahitaji mwangaKwani unaanzeje kuwaamini ukawa?