UKAWA kufungua kesi mahakamani leo

UKAWA kufungua kesi mahakamani leo

Hawatafanikiwa na wanafahamu hawatafanikiwa!.

Bunge Maalum la Katiba lina kinga kisheria za kuzuia kuhojiwa na chombo chochote kuhusu lolote linalofanyika/lililofanyika ndani ya bunge.

Hawa wanatafuta sifa ambazo hazipo.
Nahisi unachanganya kati ya bunge la Jamhuri ya muungano na bunge maalumu la katiba (BMK).

BMK limeundwa kutokana na sheria ya mabadiliko ya katiba, ni tofauti kabisa ki mamlaka naki wajibu na bunge la Jamhuri ya muungano, tunachotaka ni mahakama ifafanue mamlaka lililonayo juu ya rasimu iliyowasilishwa na tume,

Tunataka tujue, Je, bunge hili lina mamlaka, kulingana na sheria iliyoliunda, kuondoa hata misingi mikuu ya rasimu na kuweka mingine?, Je, lina mamlaka hata ya kuitupilia mbali rasimu iliyowasilishwa na tume na kuibuka na rasimu nyingine kabisa?
 
Ha ha ha! Hiyo ni kweli tupu mdau! Kamishna polepole anajua aisee! Kwa maneno yake mwenyewe Kamishna Polepole anadai yeye ni mara yake ya kwanza kuandika katiba na amepata uekewa mkubwa sana, kwa kuwa walifanyakazi ile kama team, wakafafanuliwa pale walipokosa kuelewa, mwishowe kila Mjumbe akatoka na Elimu kubwa ya Uandikaji wa katiba, tafsiri pana ya kila kifungu ndani ya Rasimu na mambo mengi ya Kikatiba!

Unaona mkuu halafu anakuja mtu from no where maadamu kavimbishwa vitumbua sijui, na maccm basi yeye ni kubwabwaja tu mwanzo mwisho hajali anachokiongea kinaukweli kiasi gani yeye ni kuropoka kwakeli ukiangalia sana matatizo mengi katika nchi yetu yamejengwa ktk msingi wa njaa.
Ni kutokana na njaa mtu anafanya kitu ambacho katu dhamira yake haimtumi maadam aujue MSALANI ulipo nitatizo sana.

BACK TANGANYIKA
 
Mimi sio mwanasheria lakini nimesikia kua Bunge la katiba la haki ya kujadili, kubadilisha, kurekebisha, kuongeza au kuondaa kifungu chochote cha rasimu ya katiba. Kama ni kweli haki hiyo ipo, basi wanaofungua kesi wanapoteza muda wao na wanachelewesha upatikanaji wa katiba mpya. Tumeshuhudia matatizo mengi na tuhuma nyingi dhidi ya tume ya uchaguzi kwamba ndio wanawachelewesha wapinza kuingia Ikulu, mi naona wangezingatia mfumo wa tume ili wachukue nchi kisha watuletee hiyo katiba mpya ndani ya siku 100.
 
Naunga mkono maboresho ya kutoka tatu kwenda mbili maana mbili ndiyo zinafaa
 
Taarifa toka katika gazeti moja la leo la mtanzania 29/4/2014 lime ripoti kuwa ukawa wanajiandaa kumfungulia kesi mwanasheria mkuu wa serikali juu ya wa mjadala wa rasimu bungeni;mashtaka yake yatakua ni kutosimamia sheria inayo wataka wajumbe wa bunge maalum kujadili rasimu iliyo wasilishwa bungeni kwa mujibu wa sheria kinyume chake wajumbe wamejikita kujadili mambo ambayo hayamo katika rasimu iliyo letwa bungeni;sheria ya mchakato wa katiba namba 25(2) inasema wajumbe wataboresha rasimu na sikubadilisha ama kufuta yaliyomo ndani ya rasimu;mantiki ya kuboresha mfano wake ni kuwa nyumba ina madirisha 3 umeambiwa uyaboreshe maana yake sio kuongeza madirisha yawe 4 ama kupunguza yawe 2 ila mantiki yake kuya boresha maana yake ni kama yalikua ya mbao unaweka ya viyoo lakini yale yale 3,kama yalikua hayana nondo za ulinzi unayawekea nondo lakini yatabakia yale yale 3 na sio kuongeza yawe 4 au kupunguza yawe 2,huko si kuboresha;
inayoboreshwa ni nyumba sio madirisha,huwezi kuboresha dirisha pekee kama nyumba haipo.
 
Tunaona kila Siku na kusikia wajumbe waliobaki bungeni na wale wanaojiita tanzania kwanza wakiwapiga vijembe ukawa. Eti ooh! Sijui wanataka kuvunja muungano! Mara oh! Ni wanafiki! Mara hawaitakii mema Tanzania ! Mara kuwakejeli eti hata wasiporudi bungeni wao watapitisha katiba inayokubalika na wananchi. Hapa najiuliza' hivi ukawa na Hawa wengine nani anatetea maoni ya wananchi? Tuwe Wa kweli hapa! Tuache porojo hapa. Nauliza tu tuache itikadi tuache upenzi Wa mire go yetu
 
  • Thanks
Reactions: jme
Ni hatua nzuri! Sasa hivi wamebadilisha baadhi ya vifungu katika Kanuni zao ili wachache wasipate nafasi ya kuzungumzia misimamo yao. Baadaye wanaweza kuleta Mswada wa kubadilisha vipengere vya 2/3 visitumike katika upigaji wa kura na kuamua tu wengi wape!
 
Tunaona kila Siku na kusikia wajumbe waliobaki bungeni na wale wanaojiita tanzania kwanza wakiwapiga vijembe ukawa. Eti ooh! Sijui wanataka kuvunja muungano! Mara oh! Ni wanafiki! Mara hawaitakii mema Tanzania ! Mara kuwakejeli eti hata wasiporudi bungeni wao watapitisha katiba inayokubalika na wananchi. Hapa najiuliza' hivi ukawa na Hawa wengine nani anatetea maoni ya wananchi? Tuwe Wa kweli hapa! Tuache porojo hapa. Nauliza tu tuache itikadi tuache upenzi Wa mire go yetu

mkuu hata hao tanzania kwanza wanajua UKAWA wanatetea maoni ya wananchi ila ni kutoweka mbele maslai ya taifa
 
Tofauti ya mtu ukilazimishwa kufikiri kama mkuu wako wa kazi unakuwa huwajibiki kikamilifu sababu unajua kitakachotokea wakwanza kujibu ni mkuu wa kazi.

UKAWA wanahitajika kuishtaki serikali na kusimamisha kabisa huo mchakato,baadhi ya watanzania tumechoka na Zecomedy zenye matusi na mipasho,na hizo pesa zisaidie kupeleka panadol kwa hospitali.
 
Taarifa toka katika gazeti moja la leo la mtanzania 29/4/2014 limeripoti kuwa UKAWA wanajiandaa kumfungulia kesi mwanasheria mkuu wa serikali juu ya wa mjadala wa rasimu bungeni.

Mashtaka yake yatakuwa ni kutosimamia sheria inayowataka wajumbe wa bunge maalum kujadili rasimu iliyowasilishwa bungeni kwa mujibu wa sheria kinyume chake wajumbe wamejikita kujadili mambo ambayo hayamo katika rasimu iliyoletwa bungeni.

Sheria ya mchakato wa katiba namba 25(2) inasema wajumbe wataboresha rasimu na sikubadilisha ama kufuta yaliyomo ndani ya rasimu.

Mantiki ya kuboresha mfano wake ni kuwa nyumba ina madirisha 3 umeambiwa uyaboreshe maana yake sio kuongeza madirisha yawe 4 ama kupunguza yawe 2 ila mantiki yake kuyaboresha maana yake ni kama yalikuwa ya mbao unaweka ya viyoo lakini yale yale 3,kama yalikua hayana nondo za ulinzi unayawekea nondo lakini yatabakia yale yale 3 na sio kuongeza yawe 4 au kupunguza yawe 2,huko si kuboresha.

Hii kesi UKAWA wameisha shindwa hata kabla haija anza. Hakuna kesi hapo, nadhani ghiliba za kisiasa na yaonyesha UKAWA wameisha kubali kushindwa.
 
UKAWA wakishindwa hii kesi,sijui tutakimbilia wapi maana ma-CCM yatapata nguvu balaa na yatachonga sana.
 
Lakini sio kuondoa msingi mkuu uliojenga rasimu nzima, ambayo ni muundo wa serikali..

Mkuu nahitaji kuelimishwa zaidi, kama hutojali tafadhali saidia kunifafanulia mambo ya fuatayo:- Katiba ya China imejengwa katika Misingi Mikuu mitatu/ 3 principles of the people ambayo ni Nationalism, Democracy and Socialism. kwa kiasi kikubwa sana katiba yao imeweza kuwasaidia na sasa wanatarajiwa kuiengua USA kileleni kwa nguvu kubwa za kijeshi baada ya kufanikiwa kiuchumi! NATIONALISM, DEMOKRACY and SOCIALISM ndiyo Misingi ya Kuzaliwa kwa Azimio la Arusha kwa uelewa wangu. SWALI:- Kama Muundo wa Serikali ndiyo msingi Mkuu unaojenga rasimu nzima, Je? Rasimu Katiba Tarajiwa itakidhi Mahitaji ya Nchi katika nyakati hizi za Ushindani Mkali wa Kiuchumi? Kuweka kwenye KATIBA mpya kipengele cha KUWAVUTIA WAWEKEZAJI WA NJE huku sikuuza nchi?...Mkuu fikiria kabla ya kuandika kwanza ili nipate majibu yanayosadifiana na maswali yangu... Danken!
 
Umezungumzia katiba ya China, baadae ukagusia kidogo kuhusu kipengele kilichomo kwenye rasimu ambacho kinazungumzia kuwavutia wawekezaji na umedai kuwa ni sawa na kuuza nchi.....

Kama sijasahau, nadhani tunazungumzia mamlaka lililonayo BMK juu ya rasimu ya katiba iliwasilishwa tume...
Mkuu nahitaji kuelimishwa zaidi, kama hutojali tafadhali saidia kunifafanulia mambo ya fuatayo:- Katiba ya China imejengwa katika Misingi Mikuu mitatu/ 3 principles of the people ambayo ni Nationalism, Democracy and Socialism. kwa kiasi kikubwa sana katiba yao imeweza kuwasaidia na sasa wanatarajiwa kuiengua USA kileleni kwa nguvu kubwa za kijeshi baada ya kufanikiwa kiuchumi! NATIONALISM, DEMOKRACY and SOCIALISM ndiyo Misingi ya Kuzaliwa kwa Azimio la Arusha kwa uelewa wangu. SWALI:- Kama Muundo wa Serikali ndiyo msingi Mkuu unaojenga rasimu nzima, Je? Rasimu Katiba Tarajiwa itakidhi Mahitaji ya Nchi katika nyakati hizi za Ushindani Mkali wa Kiuchumi? Kuweka kwenye KATIBA mpya kipengele cha KUWAVUTIA WAWEKEZAJI WA NJE huku sikuuza nchi?...Mkuu fikiria kabla ya kuandika kwanza ili nipate majibu yanayosadifiana na maswali yangu... Danken!
 
Hii kesi ni muhimu sana kufunguliwa, kinyume na hapo ni kama Wananchi wamekubaliana kwa 100% na watu waliodharau maoni yao. Imefunguliwa na nani, itaendeshwaje na hukumu itakuwaje, hilo tusiliangalie sasa. Ni wachache waliwaelewa Wazanzibar waliofungua kesi ya katiba na japo haikutolewa hukumu lakini imebakia kuwa mwongozo muhimu wa Muungano.
 
Back
Top Bottom