Wanabodi-
Naomba niandike machache na msingi sana juu ya wilaya ya Mwanga kisiasa na hali inayiendelea kwasasa kwenye Ukawa.
Kumezuka katabia kabaadhi ya vyama vilivyomo kwenye Ukawa kuanza kudandia majimbo ambayo hawajawahi kufanya kazi za kisiasa zozote zile. Kwasasa hapa Mwanga Nccr nao wanataka jimbo la Mwanga kisa nao wapo kwenye Ukawa, hii ni aibu na hatari sana kwakazi kubwa iliyofanywa na Chadema Wakiongozwa na Kamanda Kilewo tokea 2011 na hatimaye wapare wameelewa nini maana ya mabadiliko sasa wanataka kukatuzwa ndoto zao za chachu ya mabadiliko iliyokuwa imefutika siyo tu mwanga bali pare yote mpaka same.
Viongozi wetu wawe makini sana na jambo hili kwakuww litawarudisha watu wengi nyuma waliyoamua kujitolea na kufilisika na wengine hata kupelekea kufungwa na kuachana na wenza wao. Ukienda maeneo ya Lang'ata,Kirya,kileo,ngujini,kilomeni,kifula,shighatini,mwaniko,kighare,chomvu,kirongwe,tologha,kwakoa hawawezi kusikia hadithi nyingine isipokuwa Chadema pekee.
Sijui ni kauli ipi itatumika kuiweka Nccr pale Mwanga, kama kunawatu ambao angalau wangepaswa kunyanyua mdomo juu ya Mwanga ilikuwa ni Cuf not Nccr. Hawa hawana hata kiongozi wa wilaya,kata,kijiji ndiyo sasahivi wanapita kwenda kutafuta viongozi tena wanapita kwenye viongozi wa Chadema kuwalaghai kuwa jimbo hilo limeachiwa wao Nccr.
Kama Ukawa wanania ya kuongoza Tanzania yetu wasigawane majimbo kama pipi, ninauhakika kama Nccr wakipewa hilo jimbo ccm hawatafanya Kampeni na itakuwa furaha kwao huku wanachadema wakiachwa kwa majonzi makubwa kwani kazi waliyoifanya kwa muda mrefu waroho wachache wameamua ipotee.
Tutalaani sana vyama hivi vya Ukawa kwa kuipoteza Mwanga, wapiganaji wengi wataumia sana, sidhani kama itakuwa ni haki Kwa wanachadema wa Mwanga.
Viongozi wa Ukawa kuweni na huruma na Wananchi wa Mwanga msiwafanye waendelee kuwa mateja ya ccm wapeni chaguo lao.
Acheni biashara ya kutaka kufurahishana kama wanaukwa, msigawe majimbo kwa idadi ya namba mtapoteza majimbo mengi na mtashindwa kuongoza serikali.
Ushauri wangu:
Busara na weledi unahitaji kuhusu mwanga kuliko kufanya maamuzi ya kutaka kugawa mwanga kwakutumia kumuenzi Marehemu Dr.Mvungi. sidhani hata yeye kama angalikuwa hai angekubali Mwanga ipotee kwa kigezo hicho kisichokuwa na mbele wala nyuma.
Naomba niandike machache na msingi sana juu ya wilaya ya Mwanga kisiasa na hali inayiendelea kwasasa kwenye Ukawa.
Kumezuka katabia kabaadhi ya vyama vilivyomo kwenye Ukawa kuanza kudandia majimbo ambayo hawajawahi kufanya kazi za kisiasa zozote zile. Kwasasa hapa Mwanga Nccr nao wanataka jimbo la Mwanga kisa nao wapo kwenye Ukawa, hii ni aibu na hatari sana kwakazi kubwa iliyofanywa na Chadema Wakiongozwa na Kamanda Kilewo tokea 2011 na hatimaye wapare wameelewa nini maana ya mabadiliko sasa wanataka kukatuzwa ndoto zao za chachu ya mabadiliko iliyokuwa imefutika siyo tu mwanga bali pare yote mpaka same.
Viongozi wetu wawe makini sana na jambo hili kwakuww litawarudisha watu wengi nyuma waliyoamua kujitolea na kufilisika na wengine hata kupelekea kufungwa na kuachana na wenza wao. Ukienda maeneo ya Lang'ata,Kirya,kileo,ngujini,kilomeni,kifula,shighatini,mwaniko,kighare,chomvu,kirongwe,tologha,kwakoa hawawezi kusikia hadithi nyingine isipokuwa Chadema pekee.
Sijui ni kauli ipi itatumika kuiweka Nccr pale Mwanga, kama kunawatu ambao angalau wangepaswa kunyanyua mdomo juu ya Mwanga ilikuwa ni Cuf not Nccr. Hawa hawana hata kiongozi wa wilaya,kata,kijiji ndiyo sasahivi wanapita kwenda kutafuta viongozi tena wanapita kwenye viongozi wa Chadema kuwalaghai kuwa jimbo hilo limeachiwa wao Nccr.
Kama Ukawa wanania ya kuongoza Tanzania yetu wasigawane majimbo kama pipi, ninauhakika kama Nccr wakipewa hilo jimbo ccm hawatafanya Kampeni na itakuwa furaha kwao huku wanachadema wakiachwa kwa majonzi makubwa kwani kazi waliyoifanya kwa muda mrefu waroho wachache wameamua ipotee.
Tutalaani sana vyama hivi vya Ukawa kwa kuipoteza Mwanga, wapiganaji wengi wataumia sana, sidhani kama itakuwa ni haki Kwa wanachadema wa Mwanga.
Viongozi wa Ukawa kuweni na huruma na Wananchi wa Mwanga msiwafanye waendelee kuwa mateja ya ccm wapeni chaguo lao.
Acheni biashara ya kutaka kufurahishana kama wanaukwa, msigawe majimbo kwa idadi ya namba mtapoteza majimbo mengi na mtashindwa kuongoza serikali.
Ushauri wangu:
Busara na weledi unahitaji kuhusu mwanga kuliko kufanya maamuzi ya kutaka kugawa mwanga kwakutumia kumuenzi Marehemu Dr.Mvungi. sidhani hata yeye kama angalikuwa hai angekubali Mwanga ipotee kwa kigezo hicho kisichokuwa na mbele wala nyuma.