2025 vigogo hawa watatoana jasho jimbo la Mwanga

Jun 25, 2022
12
8
Mwaka 2025 siyo mbali kama Mwenyezi Mungu anakuweka hai,ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa kumpata Rais, wabunge na madiwani na kuna majimbo ya uchaguzi ambayo hakika makada watatoana jasho kweli kweli.

Jimbo la Mwanga ni moja ya majimbo nane ya uchaguzi mkoani Kilimanjaro ambalo kwa sasa mbunge wake ni wakili msomi Joseph Thadayo aliyerithi mikoba hiyo kutoka kwa profesa Jumanne Maghembe ambaye zama zake za kisiasa zinaelekea ukingoni.

Za chini chini zinatonya kuwa mchuano utakuwa mkali kwa makada watatu akiwamo Thadayo mwenye ,profesa maghembe ambaye anatajwa kuwa ameanza harakati za kujijenga ndani ya chama ili kupambania kombe huku mmoja wa wafanyakabiashara wakubwa na mjumbe wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC), Seleman Mfinanga naye akitajwa kuja kwa kasi ya kutisha.

Wote watatu wanatajwa kuwa na nguvu kiuchumi na kisiasa lakini yote kwa yote mwamuzi ni kura ya maoni ndani ya chama na atakayechanga karata zake vizuri ndiye atayeibuka kidedea japo mwamuzi wa mwisho ni Kamati Kuu ya CCM.

"Thadayo lazima akaze kweli kweli maana kwa mwenendo uliopo kwa sasa asipokuwa makini anaweza asitetee kiti chake japo bado wana mwanga wanamkubali sana kutokana na kushughulikia changamoto nyingi za wananchi",anasema mmoja wa wananchi wa Shighatini.

Pamoja na huyo wapo wanaomtaja Mfinanga naye kuwa na nguvu kutokana na nafasi yake ya MNEC ambayo inamwezesha kuwa na mtandao mkubwa ndani ya chama katika wilaya ya Mwanga huku wengi wakimtaka maghembe apumzike wakidai hana jipya.

Wacha tusubiri,muda utaongea
 
Jimbo linalogombaniwa sasa halina maendeleo na miaka yote iyo walio ongoza nenda mkinzingo kule Kuna chuo kikubwa lakini wanafunzi 47 kwasababu hakuna mazingira mazur fika lembeni ndio kuzid
 
Mume wa zamani wa Joyce Kiria na Twaha Abadallah Mwaipaya wa Chadema usiwasahau kwenye orodha
 
Jimbo linalogombaniwa sasa halina maendeleo na miaka yote iyo walio ongoza nenda mkinzingo kule Kuna chuo kikubwa lakini wanafunzi 47 kwasababu hakuna mazingira mazur fika lembeni ndio kuzid
Kama hiyo wilaya ya Mwanga tangu tupate Uhuru mpaka leo HAINA STAND KABISA, zaidi ya parking pale jirani na Highway
 
Tupo wengi hapo, aungurumaye ni papa kumbe na wengine tupo! Wee subiri muda ufike utatuona tutakapofurumkia huko!
 
Jimbo linalogombaniwa sasa halina maendeleo na miaka yote iyo walio ongoza nenda mkinzingo kule Kuna chuo kikubwa lakini wanafunzi 47 kwasababu hakuna mazingira mazur fika lembeni ndio kuzid
mapema sana mambo haya tiaa kapuni fanya kazi
 
Wilaya isiyo na Kilimo, Ufugaji, Biashara za maana nk nk. Zaidi wanauziana Perege tu
 
2025 hatutafanya makosa tuliyofanya 2020. 2020 Tulikuwa loyal sana kwa chama kimoja. Ila 2025, inatakiwa mtu uwe na kadi ya vyama angalau vitatu!
Ukiliwa kichwa huku, unaponea kule.
2025 ni mwaka wa fursa... Hapana kucheza mbali na unga 1/4!
 
Back
Top Bottom