MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,255
- 8,027
Kama mnafuatilia vizuri ni kwamba mkuu wetu mtukufu anafanya ziara zake mikoani kila siku,lakini awapo jukwaani hulitumia vizuri kwa dakika kadhaa kukinadi chama chake na hata kubishambulia na kuviponda vyama vya upinzani nchini. Hufikia hata kuwaita baadhi ya waliokua makada wa CCM na kuwaomba warudi kukijenga chama tena hadharani.Lakini kinyume kabisa na katiba kwa wale ambao hawakuchaguliwa hawaruhusiwi kufanya siasa hadi hapo 2020 wakati wa kutangaza wagombea wao.Sitaki kuuliza ni vipi wananchi watavifahamu hivyo vyama wakati wa kampeni tu maana sio swali tena ni mjadala uliopo wakati huu.
Sasa hapa kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida usiohitaji PhD atajua kua kuna siasa ya chini kwa chini kuhakikisha kua upinzani unafutika nchini ili chama utawala kiendelee kusalia madarakani pamoja na ukongwe wake. Mimi hua nafikiri kua sera nzuri na utendaji wa mtu ndio kivutio kikubwa kwa wananchi kukupenda chama chake na sio kuwashawishi kwa kuwaponda wapinzani.
Huu ni mtihani mkubwa na mgumu sana kwa UKAWA na vyama vingine vya upinzani katika ustawi wake nchini, Vinalazimishwa kua "Dormant" kwa lazima na ikizingatiwa msajili wa vyama anavitaka kisheria vyama vyote kupitia kwa wananchi kutafuta uungwaji mkono kwa kueneza itikadi na kunadi Sera zao.Hapa ndipo mtu unafikia mahali kutafuta nini lengo kuu hasa la chama cha siasa mahali popote.
Naufananisha utalatibu huu na bao la mkono ambapo mfungaji ameshaona hakuna namna ya kutumia mguu(Katiba) kuufunga mpira huo bali analazimisha kwa mikono ili mradi refa atangaze goli tu mwisho wa mchezo.
Sasa hapa kwa mtu mwenye uelewa wa kawaida usiohitaji PhD atajua kua kuna siasa ya chini kwa chini kuhakikisha kua upinzani unafutika nchini ili chama utawala kiendelee kusalia madarakani pamoja na ukongwe wake. Mimi hua nafikiri kua sera nzuri na utendaji wa mtu ndio kivutio kikubwa kwa wananchi kukupenda chama chake na sio kuwashawishi kwa kuwaponda wapinzani.
Huu ni mtihani mkubwa na mgumu sana kwa UKAWA na vyama vingine vya upinzani katika ustawi wake nchini, Vinalazimishwa kua "Dormant" kwa lazima na ikizingatiwa msajili wa vyama anavitaka kisheria vyama vyote kupitia kwa wananchi kutafuta uungwaji mkono kwa kueneza itikadi na kunadi Sera zao.Hapa ndipo mtu unafikia mahali kutafuta nini lengo kuu hasa la chama cha siasa mahali popote.
Naufananisha utalatibu huu na bao la mkono ambapo mfungaji ameshaona hakuna namna ya kutumia mguu(Katiba) kuufunga mpira huo bali analazimisha kwa mikono ili mradi refa atangaze goli tu mwisho wa mchezo.