Ukaribu wa Mwalimu Nyerere na familia ya Freeman Mbowe

Ukaribu wa Mwalimu Nyerere na familia ya Freeman Mbowe

brownjosephati

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2024
Posts
615
Reaction score
758
Kama ulikuwa hujui kuwa FREEMAN MBOWE jina lake alipewa na MWALIMU NYERERE, basi wacha nikufahamishe.
Watu wengi hudhani kuwa familia ya MBOWE na ile ya MWALIMU NYERERE ni maadui kwa sababu FREEMAN MBOWE ni mpinzani wa kisiasa.

Hili si kweli. Ukweli ni kwamba familia hizi mbili ni marafiki wa karibu sana—urafiki ambao ulianzia enzi za MWALIMU NYERERE na unaendelea hadi leo ninavyokuandikia makala hii.

Zimekuwa familia zinazoheshimiana sana. Na la kushangaza kwa wengi ni kwamba FREEMAN MBOWE humchukulia MWALIMU NYERERE kama baba yake.

Siyo tu kwa sababu MWALIMU ni BABA WA TAIFA, bali ni kutokana na urafiki wa karibu sana uliokuwepo kati ya baba yake FREEMAN MBOWE na MWALIMU NYERERE.

Mtu unayemuona kwenye picha akipeana mkono na MWALIMU NYERERE ni baba mzazi wa FREEMAN MBOWE. Anaitwa AIKAEL ALFAYO MBOWE. Picha hiyo ilipigwa mkoani Kilimanjaro wakati MWALIMU alikuwa ziarani huko.

Mzee AIKAEL alikuwa tajiri mkubwa mkoani Kilimanjaro na mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa kwa chama cha TANU.

Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE alihamasisha wananchi wa Arusha na Kilimanjaro wakiwemo machifu kujiunga na TANU. Kwa kifupi, alikuwa mmoja wa wapigania uhuru wakubwa hapa nchini. Kutokana na mchango huo, MWALIMU NYERERE alimpenda sana na hatimaye wakawa marafiki wa karibu sana.

Urafiki wao ulikuwa wa dhati kiasi kwamba mzee AIKAEL aliweza kufika IKULU muda wowote aliotaka, kumuona na kuzungumza na MWALIMU NYERERE.

Mzee huyu ndiye mtu aliyekwenda IKULU mara nyingi zaidi ya wazee wengine enzi za utawala wa NYERERE. Na mara nyingi aliambatana na mwanawe, FREEMAN MBOWE.

Hapo ndipo dhana ilipozaliwa kuwa FREEMAN MBOWE amelewa IKULU kwa sababu alizoea kuingia IKULU tangu akiwa mtoto mdogo. Urafiki huo mkubwa pia ulipelekea familia hizi mbili kuwa karibu hata zaidi.

Ukaribu huu unaonekana pia katika maisha ya MAKONGORO NYERERE na FREEMAN MBOWE, waliocheza pamoja mara nyingi wakiwa watoto. Mwaka 1983, MAKONGORO NYERERE alipoamua kuoa, alimkabidhi barua ya posa kwa mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE rafiki wa karibu wa baba yake.

Hivyo basi, mzee MBOWE akawa mshenga katika ndoa hiyo, kwa ombi maalum la MWALIMU NYERERE.

Ndoa hiyo ya MAKONGORO NYERERE na AISHA ilifungwa rasmi, na leo hii mkewe ni Jaji kitaaluma.

Na jambo lingine la kuvutia: wakati FREEMAN MBOWE anabatizwa tarehe 9 Desemba 1961—siku ambayo Tanzania ilipata uhuru baba wa ubatizo wake hakuwa mwingine bali ni MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE. Na jina "FREEMAN" alipewa na MWALIMU mwenyewe.

Makala hii imeletwa kwenu ✍️✍️
 
Mbowe ni mwanaccm kamili na alikuwa chadema kusukuma ajenda za ccm. Zile 4R ulikuwa mkataba baina yake na mwenyekiti wa chama cha kijani ndio maana npaka leo Lissu analalamika kuwa hawajui ni nini Mbowe alijadili ikulu.

Hamuwezi kujiita Chama cha Demokrasia huku mtu akishindwa uchaguzi anahama chama. Wanatuhibiria tuache dhambi angali wao hawazitii amri kumi
Mbowe ana Roho mbaya sana tokea Lisu apelekwe jela hujawahi kwenda kumuona jela au hata kwenda mahakamani kinafiki
 
LISIVYO NA AIBU LINAFANYA TIMMING YA LINI LIJIUNGE CHAUMA!!!
 
Kama ulikua hujui kuwa FREEMAN MBOWE jina lake alipewa na MWALIMU NYERERE wacha nikufahamishe:-
Watu wengi hudhani familia ya MBOWE na familia ya MWALIMU NYERERE ni maadui,
Kwasababu tu kuwa FREEMAN MBOWE ni mpinzani sio kweli,
Familia hizi ni familia marafiki sana tokea enzi za MWALIMU NYERERE mpaka leo ninavyokuletea makala hii,
Na zina heshimiana sana lakini pia usichokijua ni kwamba,
FREEMAN MBOWE humchukulia MWALIMU NYERERE kama baba yake,
Siyo kwamba humchukulia kama baba kwasababu,
MWALIMU NYERERE ni BABA YETU WA TAIFA tu hapana,
Humchukulia kama baba yake kwasasababu ya urafiki mkubwa,
Uliokuwepo kati ya baba yake mzazi na MWALIMU NYERERE,
Unae muona hapo chini anae peana mikono na mwalimu NYERERE,
Ni baba yake mzazi na FREEMAN MBOWE,
Kwa wale musiomjua huyu ndio baba yake mzazi kabisa FREEMAN MBOWE,
Kwa jina anaitwa AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Picha hii ilipigwa huko mkoani KILIMANJARO,
Wakati MWALIMU NYERERE alipokuwa anafanya ziara mkoani humo,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE alikuwa ni tajiri mkubwa mkoani KILIMANJARO,
Aliyetoa mchango wa kipekee kwa chama cha TANU,
Ikiwemo kuwashawishi na kuwaingiza wananchi wa ARUSHA na KILIMANJARO,
Kwenye chama cha TANU wakiwemo machifu,
Kiufupi mzee MBOWE ni moja ya wapigania uhuru wakubwa hapa nchini,
Kutokana na kitendo hicho MWALIMU NYERERE,
Alimpenda sana mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Hatimae wakawa marafiki wakubwa wakati wa uhai wao,
Na ilifika hatua mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Akawa akitaka kwenda IKULU anaenda muda wowote,
Kumuona NWALIMU NYERERE na kuzungumza nae,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE ndio mzee aliekwenda IKULU,
Mara nyingi zaidi kuliko mzee yoyote enzi za mwalimu NYERERE akiwa IKULU,
Na mara nyingi alipokua akienda alikua anaenda na mwanawe aitwae FREEMAN MBOWE,
Na hapo ndipo ilipozuka dhana kuwa FREEMAN MBOWE amelelewa IKULU,
Kwasababu FREEMAN MBOWE hajaanza juzi kwenda IKULU,
Ameanza kwenda IKULU tangu akiwa mdogo,
Na urafiki wa mwalimu NYERERE na mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Ulisababisha hata familia zao ziwe na urafiki wakubwa,
Kama ulikua hujui ni kwamba FREEMAN MBOWE na MAKONGORO NYERERE,
Wamecheza pamoja mara nyingi sana wakiwa wadogo,
Kwasababu mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE kama nilivyosema hapo juu kuwa alikua rafiki mkubwa wa NYERERE,
Na kwa kuthibitisha hilo kuwa familia hizi zina urafiki mkubwa,
Mwezi Octoba mwaka 1983 mtoto wa mwalimu NYERERE aitwae MAKONGORO NYERERE alipotaka kuoa,
Aliempelekea barua ya posa MAKONGORO NYERERE ni mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Huyu ndie alikua mshenga katika ndoa yake,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE alifanya hivyo,
Baada ya kuombwa na MWALIMU NYERERE kufanya hivyo kama rafiki yake,
Hatimae ndoa kati ya MAKONGORO NYERERE na mkewe aitwae AISHA ikafungwa,
Mke wa MAKONGORO NYERERE kitaaluma,
Yeye ni mwanasheria na kwasasa mkewe ni JAJI,
Na kitu chengine usicho kijua ni kwamba,
Wakati FREEMAN MBOWE anabatizwa tarehe 9/12/1961,
Siku ambayo uhuru wa nchi hii ulipatikana,
Aliekuwa baba wa ubatizo wa FREEMAN MBOWE siku hiyo,
Alikua ni MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,
Na jina la FREEMAN mtu aliechagua jina hilo,
Siyo mwengine ni MWALIMU NYERERE.

Makala hii imeletwa kwenu ✍️✍️

KURA ZOTE-TWENDE NA MAMA 2025-30
ubongo wako uko hivi kama vifuu vya nazi
1749696554179.jpeg
 
Kama ulikua hujui kuwa FREEMAN MBOWE jina lake alipewa na MWALIMU NYERERE wacha nikufahamishe:-
Watu wengi hudhani familia ya MBOWE na familia ya MWALIMU NYERERE ni maadui,
Kwasababu tu kuwa FREEMAN MBOWE ni mpinzani sio kweli,
Familia hizi ni familia marafiki sana tokea enzi za MWALIMU NYERERE mpaka leo ninavyokuletea makala hii,
Na zina heshimiana sana lakini pia usichokijua ni kwamba,
FREEMAN MBOWE humchukulia MWALIMU NYERERE kama baba yake,
Siyo kwamba humchukulia kama baba kwasababu,
MWALIMU NYERERE ni BABA YETU WA TAIFA tu hapana,
Humchukulia kama baba yake kwasasababu ya urafiki mkubwa,
Uliokuwepo kati ya baba yake mzazi na MWALIMU NYERERE,
Unae muona hapo chini anae peana mikono na mwalimu NYERERE,
Ni baba yake mzazi na FREEMAN MBOWE,
Kwa wale musiomjua huyu ndio baba yake mzazi kabisa FREEMAN MBOWE,
Kwa jina anaitwa AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Picha hii ilipigwa huko mkoani KILIMANJARO,
Wakati MWALIMU NYERERE alipokuwa anafanya ziara mkoani humo,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE alikuwa ni tajiri mkubwa mkoani KILIMANJARO,
Aliyetoa mchango wa kipekee kwa chama cha TANU,
Ikiwemo kuwashawishi na kuwaingiza wananchi wa ARUSHA na KILIMANJARO,
Kwenye chama cha TANU wakiwemo machifu,
Kiufupi mzee MBOWE ni moja ya wapigania uhuru wakubwa hapa nchini,
Kutokana na kitendo hicho MWALIMU NYERERE,
Alimpenda sana mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Hatimae wakawa marafiki wakubwa wakati wa uhai wao,
Na ilifika hatua mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Akawa akitaka kwenda IKULU anaenda muda wowote,
Kumuona NWALIMU NYERERE na kuzungumza nae,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE ndio mzee aliekwenda IKULU,
Mara nyingi zaidi kuliko mzee yoyote enzi za mwalimu NYERERE akiwa IKULU,
Na mara nyingi alipokua akienda alikua anaenda na mwanawe aitwae FREEMAN MBOWE,
Na hapo ndipo ilipozuka dhana kuwa FREEMAN MBOWE amelelewa IKULU,
Kwasababu FREEMAN MBOWE hajaanza juzi kwenda IKULU,
Ameanza kwenda IKULU tangu akiwa mdogo,
Na urafiki wa mwalimu NYERERE na mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Ulisababisha hata familia zao ziwe na urafiki wakubwa,
Kama ulikua hujui ni kwamba FREEMAN MBOWE na MAKONGORO NYERERE,
Wamecheza pamoja mara nyingi sana wakiwa wadogo,
Kwasababu mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE kama nilivyosema hapo juu kuwa alikua rafiki mkubwa wa NYERERE,
Na kwa kuthibitisha hilo kuwa familia hizi zina urafiki mkubwa,
Mwezi Octoba mwaka 1983 mtoto wa mwalimu NYERERE aitwae MAKONGORO NYERERE alipotaka kuoa,
Aliempelekea barua ya posa MAKONGORO NYERERE ni mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE,
Huyu ndie alikua mshenga katika ndoa yake,
Mzee AIKAEL ALFAYO MBOWE alifanya hivyo,
Baada ya kuombwa na MWALIMU NYERERE kufanya hivyo kama rafiki yake,
Hatimae ndoa kati ya MAKONGORO NYERERE na mkewe aitwae AISHA ikafungwa,
Mke wa MAKONGORO NYERERE kitaaluma,
Yeye ni mwanasheria na kwasasa mkewe ni JAJI,
Na kitu chengine usicho kijua ni kwamba,
Wakati FREEMAN MBOWE anabatizwa tarehe 9/12/1961,
Siku ambayo uhuru wa nchi hii ulipatikana,
Aliekuwa baba wa ubatizo wa FREEMAN MBOWE siku hiyo,
Alikua ni MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,
Na jina la FREEMAN mtu aliechagua jina hilo,
Siyo mwengine ni MWALIMU NYERERE.

Makala hii imeletwa kwenu ✍️✍️

KURA ZOTE-TWENDE NA MAMA 2025-30
Maelezo marefu haiondoi Ukora alionao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom