Ukarabati wa bunge la katiba wagharimu sh. bilioni 8.2

Sitachoka

JF-Expert Member
Nov 17, 2011
3,030
1,303
Dodoma. Kiasi cha Sh8.2 bilioni kimetumika kufanya ukarabati mkubwa wa Ukumbi wa Bunge pamoja na miundombinu yake kwa ajili ya shughuli za Bunge la Katiba litakalokutana kwa zaidi ya siku 70.

Mbali ya gharama hizo, imeelezwa pia kuwa kila mbunge wa Bunge hilo maalumu la Katiba atalipwa Sh300,000 kwa siku katika kipindi chote litakapokuwa linakutana.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah aliwaambia waandishi habari Mjini Dodoma jana kuwa posho hizo za wabunge zimechanganuliwa katika sehemu mbili.

Alisema Sh220,000 ni kwa ajili ya posho ya kikao, usafiri na dereva na Sh80,000 ni posho ya kujikimu na kwamba hicho ndicho kiwango kilichoidhinishwa na Rais Jakaya Kikwete.

"Tuliposikia kuwa wabunge watalipwa posho ya Sh700,000 kwa siku na sisi hatukujua ilitokea wapi kwa sababu Rais hakuidhinisha malipo ya aina hiyo," alisema Dk Kashililah.

Gharama za ukarabati

Kuhusu ukarabati wa ukumbi na miundombinu yake iliyogharimu Sh8.2 bilioni, Dk Kashililah alisema viti vipya 678 vilivyofungwa kwenye ukumbi huo vimegharimu takribani Dola za Marekani milioni moja (sawa na Sh1.6 bilioni) pamoja na gharama za usafiri.

Alisema gharama nyingine zimetokana na marekebisho ya mfumo wa sauti ambao ulikuwa ukilalamikiwa na wabunge kutokana na kutosikika vizuri kwa baadhi ya vipaza sauti.

Dk Kashililah alisema ukarabati huo umehusisha, mfumo mpya unaotumia teknolojia ya dijiti na kuboresha mitambo ya Idara ya Kuhifadhia ya Kumbukumbu Rasmi za Bunge ili iweze kuhimili idadi ya wabunge hao zaidi ya 600.

Alisema gharama nyingine zimetokana na ukarabati wa mifumo ya kuimarisha usalama pamoja na kuweka vioo visivyopenya risasi katika baadhi ya kumbi.

Alisema fedha nyingine zimetumika kukarabati paa la Ukumbi wa Bunge ambalo lilikuwa linavuja.

Pia fedha hizo zimetumika kurekebisha mitambo ya kufua umeme, maji, kuzima moto na viyoyozi na kumalizia ujenzi wa jengo ambalo litakuwa likitumika kwa ajili ya sehemu ya mazoezi, benki na ofisi za wabunge zaidi 100.

Dk Kashililah alisema kiasi hicho kimetumika kwa ajili ya kununua samani za ofisi za wabunge na kuongeza eneo la mgawaha na kuboresha miundombinu kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Alisema fedha zote zilizotumika katika ukarabati huo zimetokana na bajeti ya mipango ya maendeleo iliyopitishwa na Bunge mwaka jana na kwamba si jambo geni huku akisema kazi zote zimefanywa kwa mara moja.

Ratiba ya Bunge la Katiba

Kwa upande wa ratiba ya Bunge la Katiba, Dk Kashililah alisema litaanza shughuli zake rasmi kesho kwa kusomwa kwa tangazo la kuitishwa kwa Bunge Maalumu la Katiba la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Siku hiyo pia kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa muda ambaye kazi yake kubwa itakuwa ni kuandaa kanuni za Bunge Maalumu la Katiba ambalo litakuwa na wajumbe 629.

Alisema baada ya kupatikana kwa kanuni, Ijumaa kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti na makamu wake kwa kuzingatia sheria ya Mabadiliko ya Katiba iliyopitishwa mwaka jana.

Alidokeza kwa kusema pia kuwa wateuliwa, Katibu na msaidizi wake wa Bunge hilo na kwa mujibu sheria hiyo, ataanza kazi baada ya kuapishwa na Rais na baada ya kuapishwa naye atamwapisha mwenyekiti wa Bunge hilo.

Baada ya mwenyekiti kuapishwa, atawalisha kiapo wajumbe wengine wa Bunge hilo, kazi ambayo itafanyika kwa siku tatu hadi Jumatatu asubuhi na mchana wake, Rais Kikwete atalizindua rasmi.

Chanzo:Mwananchi
 
Mkuu rekebisha kichwa cha habari kisomeke,
UKARABATI WA JENGO LA BUNGE LA KATIBA.......... na sio, 'UKARABATI WA BUNGE LA KATIBA.....
 
Tanzania ni nchi tajiri sana kiasi ambacho vipaumbele vya matumizi ya fedha zake ni kiashiria tosha tosha kuwa kitu fulani kwa wanauchumi wa nchi hii hakiko sawa!
 
Mkuu mshunami nchi hii ni tajiri sana, halafu unaambiwa katiba itakayopendekezwa na hilo bunge maalum la katiba isipopitishwa tunarudi katika katiba ya zamani, hayo mabilioni yanateketea hivyo jumlisha na yale ya tume ya Warioba
 
Last edited by a moderator:
Halafu eti tukiikataa rasimu hii mpya kwenye kura ya maoni eti tutarudi kwenye katiba yetu ya sasa!!! Ambayo hata Rais anaamini(?) kuwa haifai (amenukuliwa akisema kuwa katiba hii mpya ni ya kutupeleza miaka hamsini na zaidi ijayo).
Something is wrong with us upstairs. Someone can do the math for me please, how much will cost us to 'get' our present katiba when referendum will not favour the new constitution (and yes-the obstacle is this CCM belief for serikali mbili).

By anyways, we will ask our dear President to go out and 'beg' for money when things goes wrong. Remember mtaji wa masikini ni kuomba.
 
Mkuu mshunami nchi hii ni tajiri sana, halafu unaambiwa katiba itakayopendekezwa na hilo bunge maalum la katiba isipopitishwa tunarudi katika katiba ya zamani, hayo mabilioni yanateketea hivyo jumlisha na yale ya tume ya Warioba
Hata haingii akilini mwa mwenye akili kwamba eti sababu yao ya kupinga muundo wa serikali tatu ni gharama kubwa ya uendeshaji! Kama twaweza kukarabati ukumbi kwa bilioni nane kwa kikao cha siku sabini tu, na kuwalipa wabunge mia sita milioni 21 kila mmoja kwa siku 70 tu, na wakiongeza siku 20 mtunawaongezea kila mmoja milioni 6, kabla ya gharama nyingine za mabilioni za kuendesha bunge hilo, tunasindwaje kuendesha serikali tatu? Tusikubali kudanganywa!
 
mshunami Ukubwa wa serikali na hofu ya kuvunjika kwa muungano kisa serikali tatu hiyo ni janja tu ya wabunge wengi kuhofia kupoteza majimbo yao katika bungw la jamuhuri kama rasimu inavyoelekeza kuwa bunge la jamuhuri ya muungano litakuwa na wabunge 75 tu hamsini kutoka Tanganyika na 25 kutoka Zanzibar uku uwakilishi wa jinsia ukiwa sawa kati ya wanaume na wanawake, ikiwa na maana ya kuwa majimbo ya uchaguzi ya ubunge wa wabunge wa jamuhuri yatakuwa hasini tu
 
Last edited by a moderator:
Hatimaye siri zimevuja kuwa ukarabati wa jengo la bunge una ufisadi ndani yake. Mh. Spika wa bunge anna makinda ni mtuhumiwa nambari one kwani matengenezo hayo hupata baraka zake ndipo pesa hutoka.
Wabunge wanalalamika kuwa bajeti ya matengenezo hayo ni kubwa sana kiasi kwamba nchi inatafunwa kimya kimya hadi kubakia mifupa mitupu.
Makinda tuhurumie wananchi maskini tunaokosa mikopo ya kusoma vyuo vikuu huku ukiendelea kufanya ufisadi na kutafuna fedha za wananchi na tanzania kwa ujumla.
Nawasilisha ndg.zangu kwa masikitiko makubwa sana kwa muhimili huu kulitafuna taifa hili tanzania.
 
hakuna aja kulaumu nadhani kumchinja kama wale ISIS wanavyochinja imekaa poa sana.
 
Watanzania tunaongoza kwa kulalama. Na cha ajabu mafisadi hao hao watashinda kwa kishindo uchaguzi ujao.
 
dodoma. Kiasi cha sh8.2 bilioni kimetumika kufanya ukarabati mkubwa wa ukumbi wa bunge pamoja na miundombinu yake kwa ajili ya shughuli za bunge la katiba litakalokutana kwa zaidi ya siku 70.

Mbali ya gharama hizo, imeelezwa pia kuwa kila mbunge wa bunge hilo maalumu la katiba atalipwa sh300,000 kwa siku katika kipindi chote litakapokuwa linakutana.

Katibu wa bunge, dk thomas kashililah aliwaambia waandishi habari mjini dodoma jana kuwa posho hizo za wabunge zimechanganuliwa katika sehemu mbili.

Alisema sh220,000 ni kwa ajili ya posho ya kikao, usafiri na dereva na sh80,000 ni posho ya kujikimu na kwamba hicho ndicho kiwango kilichoidhinishwa na rais jakaya kikwete.

"tuliposikia kuwa wabunge watalipwa posho ya sh700,000 kwa siku na sisi hatukujua ilitokea wapi kwa sababu rais hakuidhinisha malipo ya aina hiyo," alisema dk kashililah.

Gharama za ukarabati

kuhusu ukarabati wa ukumbi na miundombinu yake iliyogharimu sh8.2 bilioni, dk kashililah alisema viti vipya 678 vilivyofungwa kwenye ukumbi huo vimegharimu takribani dola za marekani milioni moja (sawa na sh1.6 bilioni) pamoja na gharama za usafiri.

Alisema gharama nyingine zimetokana na marekebisho ya mfumo wa sauti ambao ulikuwa ukilalamikiwa na wabunge kutokana na kutosikika vizuri kwa baadhi ya vipaza sauti.

Dk kashililah alisema ukarabati huo umehusisha, mfumo mpya unaotumia teknolojia ya dijiti na kuboresha mitambo ya idara ya kuhifadhia ya kumbukumbu rasmi za bunge ili iweze kuhimili idadi ya wabunge hao zaidi ya 600.

Alisema gharama nyingine zimetokana na ukarabati wa mifumo ya kuimarisha usalama pamoja na kuweka vioo visivyopenya risasi katika baadhi ya kumbi.

Alisema fedha nyingine zimetumika kukarabati paa la ukumbi wa bunge ambalo lilikuwa linavuja.

Pia fedha hizo zimetumika kurekebisha mitambo ya kufua umeme, maji, kuzima moto na viyoyozi na kumalizia ujenzi wa jengo ambalo litakuwa likitumika kwa ajili ya sehemu ya mazoezi, benki na ofisi za wabunge zaidi 100.

Dk kashililah alisema kiasi hicho kimetumika kwa ajili ya kununua samani za ofisi za wabunge na kuongeza eneo la mgawaha na kuboresha miundombinu kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Alisema fedha zote zilizotumika katika ukarabati huo zimetokana na bajeti ya mipango ya maendeleo iliyopitishwa na bunge mwaka jana na kwamba si jambo geni huku akisema kazi zote zimefanywa kwa mara moja.

Ratiba ya bunge la katiba

kwa upande wa ratiba ya bunge la katiba, dk kashililah alisema litaanza shughuli zake rasmi kesho kwa kusomwa kwa tangazo la kuitishwa kwa bunge maalumu la katiba la jamhuri ya muungano wa tanzania.

Siku hiyo pia kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa muda ambaye kazi yake kubwa itakuwa ni kuandaa kanuni za bunge maalumu la katiba ambalo litakuwa na wajumbe 629.

Alisema baada ya kupatikana kwa kanuni, ijumaa kutafanyika uchaguzi wa mwenyekiti na makamu wake kwa kuzingatia sheria ya mabadiliko ya katiba iliyopitishwa mwaka jana.

Alidokeza kwa kusema pia kuwa wateuliwa, katibu na msaidizi wake wa bunge hilo na kwa mujibu sheria hiyo, ataanza kazi baada ya kuapishwa na rais na baada ya kuapishwa naye atamwapisha mwenyekiti wa bunge hilo.

Baada ya mwenyekiti kuapishwa, atawalisha kiapo wajumbe wengine wa bunge hilo, kazi ambayo itafanyika kwa siku tatu hadi jumatatu asubuhi na mchana wake, rais kikwete atalizindua rasmi.

Chanzo:mwananchi

makinda ni fisadi mkubwa sana .anaifirisi nchi hafai hata kuwa monitor darasani
 
Back
Top Bottom