Uchaguzi 2020 Ukara: Wananchi wamuua mtu aliyetaka kumteka mgombea udiwani wa kata ya Bwisya kwa tiketi ya CHADEMA

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,558
35,887
Mtu mmoja ameuawa asubuhi hii na wengine wawili kufanikiwa kutoroka baada ya kujaribu kumteka mgombea udiwani wa kata ya Bwisha Ukara kwa tiketi ya CHADEMA.

Inadaiwa watu hao wamezingirwa baada ya mgombea huyo kupiga ukunga na ndipo walipozingirwa na kushushiwa kipigo ambapo mmoja ameuawa huku wawili wakifanikiwa kutoroka.

Hilo ni tukio la kwanza la mauaji yanayohusishwa na mambo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ambapo kunatabiriwa kuwepo kwa visa vingi vya vurugu kutokana na sintofahamu ambazo zimeanza kujitokeza.

Habari hii imethibitishwa na Katibu wa kanda ya Victoria- CHADEMA ndugu Zacharia T. Obad
 
Jamani, inakuaje CCM wanakuwa waoga kiasi hiki? Mbona atukuyaona wakati wa j.k?
Yaani hii ni ishara kuwa CCM ni mbovu hakuna mfano na ukiona MTU anaiunga mkono lazima ana matatizo kichwani.

Angalia jinsi wanavyo hangaika kujitangaza! Hata treni kuanza CCM yote inaambatana na mitelevision kila kona utadhani hicho ni kitu cha ajabu !
 
Hii roho mbaya ya kutekana inaonekana kushamiri. Kama waliweza kumthibiti wasingemua ili tujue ni akina nani waliowatuma.....
Hata hivyo wamepeleka somo zuri sana kwa watekaji wengine na wanaoratibu huu utekaji
 
Mungu atuepushie huu ujinga, Tanzania ni nchi ya amani na naomba usiku na mchana amani, upendo , kuheshimiana kubaki kama mojawapo ya tunu zetu
Mkuu Kiukweli ni mjinga tu ndio ataamini kuwa haya matukio yanaratibiwa na ccm, yaani wafanye huu utekaji na uuaji kwa makusudi kabisa huku wakijua kabisa lawama zitatupwa kwao na kuwapaka matope tena kwenye kipindi hiki cha uchaguzi?
Basi kama ni hivo watakuwa wapumbavu kweli kweli.
 
Hii roho mbaya ya kutekana inaonekana kushamiri. Kama waliweza kumthibiti wasingemua ili tujue ni akina nani waliowatuma.....
Popote inapomwagika damu jua dhuruma ilianza kwa baadhi kujiona Wana haki kuliko wengine.

Sisi ni binadamu kama wa Somalia, Mali, Congo ama Sudan

Hivyo yanayotokea huko hata hapa yanaweza kutokea.

Mheshimiwa Rais Magufuli huu ndio ulikuwa muda wa kuwaunganisha Watanzania kwa vitendo.

Sababu Jicho linalotuangalia huko nje sio la kheri, Wanasubiri tusambaratike wapite katikati.

Mungu iepushe Tanzania na hili pepo linalotunyemelea.
 
Back
Top Bottom