Raphael phockus
JF-Expert Member
- Nov 4, 2018
- 778
- 4,518
Habari ya mda huu wanajanvi!
Bila kupoteza mda, kutokana na kauli iliyo tolewa na muheshimiwa Rais juu ya maendeleo ya ugonjwa wa Corona hapa nchini.
Kwa mtu mwenye mtazamo mpana kimsingi ni kauli inayo pelekea mtu ajiulize maswali mengi na pengine yasiwe na majibu:-
Ikiwa Rais yeye mwenyewe kwa kinywa chake alikili kuwa mashine za kupimia virusi vya Covid-19 zina matatizo, imewezekanaje akazipata takwimu hizo za wagonjwa wa Corona?
Amewezaje kuziamini takwimu hizo kama ni sahihi?
Ikiwa maendeleo dhidi ya udhibiti wa ugonjwa wa Corona nchini ni mazuli, inakuwaje madereva wa magari ya mizigo kutokea upande wa Tanzania wakutwe na maambukizi ya virusi vya Covid-19?
Inamaana Kenya, Uganda, Rwanda, Zambia wanahuhadaa ulimwengu kuwa idadi kubwa ya watanzania wameathirika na virusi vya Covid-19. Wanafanya hivyo kwa faida ya nani?
Muheshimiwa Rais anapofikilia kutoa maamuzi juu ya ufunguzi wa vyuo nchini, anahuakika gani kuwa maambukizi yameisha mitaani. Ametumia mbinu gani kuwapima wananchi wote nakuthibitisha hilo?
Linapo kuja swala la kufunguwa vyuo hapa nchini Rais atambue kwamba kuna wanafunzi wanaotokea nnje ya nchi na wanasoma hapa nchini.
Kimsingi Rais anatowa maamzi kwa kupaniki . Rais anataka kila mtu akubaliane na mawazo yake.
Kuwa kiongozi hakukufanyi wewe uonekane una akili nyingi na mitazamo mipana kuliko wananchi wote unao waongoza. Hata mtu wa mwisho darasani kwenye mitihani anaweza akapewa dhamana ya kuwa kiongozi.
Kalibuni kwa maoni...
Not everyone is willing to take the risk!
Bila kupoteza mda, kutokana na kauli iliyo tolewa na muheshimiwa Rais juu ya maendeleo ya ugonjwa wa Corona hapa nchini.
Kwa mtu mwenye mtazamo mpana kimsingi ni kauli inayo pelekea mtu ajiulize maswali mengi na pengine yasiwe na majibu:-
Ikiwa Rais yeye mwenyewe kwa kinywa chake alikili kuwa mashine za kupimia virusi vya Covid-19 zina matatizo, imewezekanaje akazipata takwimu hizo za wagonjwa wa Corona?
Amewezaje kuziamini takwimu hizo kama ni sahihi?
Ikiwa maendeleo dhidi ya udhibiti wa ugonjwa wa Corona nchini ni mazuli, inakuwaje madereva wa magari ya mizigo kutokea upande wa Tanzania wakutwe na maambukizi ya virusi vya Covid-19?
Inamaana Kenya, Uganda, Rwanda, Zambia wanahuhadaa ulimwengu kuwa idadi kubwa ya watanzania wameathirika na virusi vya Covid-19. Wanafanya hivyo kwa faida ya nani?
Muheshimiwa Rais anapofikilia kutoa maamuzi juu ya ufunguzi wa vyuo nchini, anahuakika gani kuwa maambukizi yameisha mitaani. Ametumia mbinu gani kuwapima wananchi wote nakuthibitisha hilo?
Linapo kuja swala la kufunguwa vyuo hapa nchini Rais atambue kwamba kuna wanafunzi wanaotokea nnje ya nchi na wanasoma hapa nchini.
Kimsingi Rais anatowa maamzi kwa kupaniki . Rais anataka kila mtu akubaliane na mawazo yake.
Kuwa kiongozi hakukufanyi wewe uonekane una akili nyingi na mitazamo mipana kuliko wananchi wote unao waongoza. Hata mtu wa mwisho darasani kwenye mitihani anaweza akapewa dhamana ya kuwa kiongozi.
Kalibuni kwa maoni...
Not everyone is willing to take the risk!