fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,412
- 7,966
Hii biashara ilikuwepo enzi na dahari hakuna wa kuiwezaWanabodi nianze kwa kuwasalimu wote,
Naomba kuelezea masikiiko yangu makubwa juu ya hali ya ukahaba unaofanyika Msamvu karibu na stand kuu eneo la maduka na kwa kina mama nitilie wakati wa usiku, ni hatari sana ukichukulia sheria ya usalama barabarani ya kuzuia mabasi yanayotokea mikoani kulazimishwa kulala pale baada ya saa 4 za usiku.
Kunakuwa na abiria wengi na wasichana wanajiuza na wanafanya ufusika huu nyuma ya magari au chini ya malori au nyuma ya mabanda bila kificho, na bei zao ni sh 2000.
Nimeshuhudia uchafu huu ambao ni njia mojawapo ya kusambaza maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app