Ghulaam
JF-Expert Member
- May 10, 2016
- 1,847
- 1,440
Pole sana Roma!
Mara ya kwanza nilikuambia Hongera, lakini leo nakwambia POLE!
wimbo wako unatuonesha kuwa unajuta kuimba Ukweli, Unajuta kusimama upande wa Watu na Unaonesha kuwa Mtindo uliotumika kukunyamazisha na kukubadilishia Muelekeo umefanikiwa.
Mdogo wangu, Mwanaharakati wa Haki za binadamu hatorudi nyuma hata kwa gharama ya Uhai wake.
'Mbegu huota, kukuwa na kutoa Matunda baada ya kutupwa chini, kufa na kuoza'
Uliimba nyimbo nzuri kaka, lakini usiwatishe au kuwakatisha tamaa wapambanaji wengine wa haki za Binaadamu kwa kutumia Muziki!
Dunia ni tamu, Maisha ni Matamu kwa wenye chochote, hivyo nikitafuta sababu ya kurudi nyuma sitaikosa na itakuwa ni ya maana kwangu.
Lakini nawezaje kunyamaza wakati wanyonge wengi hawapati haki zao kama binadamu.
Naweza nyamaza kwa kufikiri kuwa nawasaidia Viongozi, lakini hata nao Viongozi wetu na watunga Sera wana haki ya kupata Ushauri kutoka kwa wasanii na kupata hisia za wanajamii ili wafanikishe Maendeleo.
kama naimba Masaibu yangu pekee nikipozwa nitanyamaza, lakini kama naimba hisia na ukweli, sauti ya wanajamii sitageuka nyuma mpaka tone la mwisho la Damu yangu.
Msikilize FELA KUTI, Wapambanaji waoga au wabinafsi hawakosi sababu ya kurudi nyuma.
"Watu wangu wanaiyaishi Majonzi, Machozi na Damu!
Hiyo ndiyo alama yao wakati wote!
Kila mtu anakimbia kimbia
Watu wanatawanyika ovyo ovyo!
Wengine wanapoteza Mkate
Wengine wanakaribia kufa Wengine wanakufa!
Lakini...
Tumekuwa waoga sana
Tunaogopa kitu ambacho hatukioni
Tunaogopa hewa inayozunguka
Tunaogopa kupigania uhuru wetu
Tunaogopa kupigania haki yetu
Tunaogopa kuipigania furaha yetu.
Siku zote tunajipa sababu za kuogopa!
Tunaanza kujiambia....
Sitaki kufa
Sitaki kujeruhiwa
Nina mtoto mmoja
Nna Mama Nyumbani
Nna baba Nyumbani
Sina nyumba
Nataka kujenga Nyumba
Sitaki kujichosha
Nataka kuinjoi
Sitaki kuondoshwa
Hizo zote ni sababu muhimu lakini je, hivyo ndiyo watu waliopewa vipaji waisaidie jamii wanapaswa kufikiri?
Usimkatie tamaa mtu aliyepotea njia, Usijiunge na Upotevu wake, mrudishe kwenye mstari kwa gharama yoyote.
Usipambane kwa Chuki, pambana kwa Upendo. Mwisho wa siku tunataka kukaa na adui Meza moja tukiwa marafiki na kuijenga nchi.
Na hiyo ndiyo kazi ya Muziki.
Mara ya kwanza nilikuambia Hongera, lakini leo nakwambia POLE!
wimbo wako unatuonesha kuwa unajuta kuimba Ukweli, Unajuta kusimama upande wa Watu na Unaonesha kuwa Mtindo uliotumika kukunyamazisha na kukubadilishia Muelekeo umefanikiwa.
Mdogo wangu, Mwanaharakati wa Haki za binadamu hatorudi nyuma hata kwa gharama ya Uhai wake.
'Mbegu huota, kukuwa na kutoa Matunda baada ya kutupwa chini, kufa na kuoza'
Uliimba nyimbo nzuri kaka, lakini usiwatishe au kuwakatisha tamaa wapambanaji wengine wa haki za Binaadamu kwa kutumia Muziki!
Dunia ni tamu, Maisha ni Matamu kwa wenye chochote, hivyo nikitafuta sababu ya kurudi nyuma sitaikosa na itakuwa ni ya maana kwangu.
Lakini nawezaje kunyamaza wakati wanyonge wengi hawapati haki zao kama binadamu.
Naweza nyamaza kwa kufikiri kuwa nawasaidia Viongozi, lakini hata nao Viongozi wetu na watunga Sera wana haki ya kupata Ushauri kutoka kwa wasanii na kupata hisia za wanajamii ili wafanikishe Maendeleo.
kama naimba Masaibu yangu pekee nikipozwa nitanyamaza, lakini kama naimba hisia na ukweli, sauti ya wanajamii sitageuka nyuma mpaka tone la mwisho la Damu yangu.
Msikilize FELA KUTI, Wapambanaji waoga au wabinafsi hawakosi sababu ya kurudi nyuma.
"Watu wangu wanaiyaishi Majonzi, Machozi na Damu!
Hiyo ndiyo alama yao wakati wote!
Kila mtu anakimbia kimbia
Watu wanatawanyika ovyo ovyo!
Wengine wanapoteza Mkate
Wengine wanakaribia kufa Wengine wanakufa!
Lakini...
Tumekuwa waoga sana
Tunaogopa kitu ambacho hatukioni
Tunaogopa hewa inayozunguka
Tunaogopa kupigania uhuru wetu
Tunaogopa kupigania haki yetu
Tunaogopa kuipigania furaha yetu.
Siku zote tunajipa sababu za kuogopa!
Tunaanza kujiambia....
Sitaki kufa
Sitaki kujeruhiwa
Nina mtoto mmoja
Nna Mama Nyumbani
Nna baba Nyumbani
Sina nyumba
Nataka kujenga Nyumba
Sitaki kujichosha
Nataka kuinjoi
Sitaki kuondoshwa
Hizo zote ni sababu muhimu lakini je, hivyo ndiyo watu waliopewa vipaji waisaidie jamii wanapaswa kufikiri?
Usimkatie tamaa mtu aliyepotea njia, Usijiunge na Upotevu wake, mrudishe kwenye mstari kwa gharama yoyote.
Usipambane kwa Chuki, pambana kwa Upendo. Mwisho wa siku tunataka kukaa na adui Meza moja tukiwa marafiki na kuijenga nchi.
Na hiyo ndiyo kazi ya Muziki.