Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 26,060
- 23,942
Dar es Salaam. Wakati waumini wa madhehebu ya Kikirsto nchini, wakiwamo Wakatoliki wakiwa katika siku 40 za mfungo wa Kwaresima ambao ni mahususi kwa ajili ya maandalizi ya Pasaka, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe mzito kwa mwaka 2014.
Ujumbe huo wenye kaulimbiu ‘Ukweli utawaweka huru', umeeleza wajibu wa kuishi ndani ya ukweli, kuulinda na kuusimamia ukweli pamoja na umuhimu wa Watanzania kujenga jamii yenye utu, haki, amani, upendo na mshikamano wa kweli.
"Wapendwa Taifa la Mungu, tunapoanza safari ya Kwaresma (kipindi cha kukumbuka mateso ya Yesu) ya mwaka huu, sisi maaskofu wenu tungependa kuwakumbusha ninyi na watu wote wenye mapenzi mema kuhusu umuhimu wa kuishi katika ukweli. Kuuishi ukweli na kuishi maisha yaliyojengwa juu ya msingi wa ukweli ni kushiriki hasa maisha ya Mungu... Pasipo ukweli, jamii itasambaratika kwa sababu itakuwa imejengwa bila msingi."
Hali halisi ya taifa letu
Waraka huo umeeleza miaka zaidi ya 50 ya uhuru wa Tanzania na kusema kuwa ni taifa lililovuka uchanga na lililo katika umri wa kujengwa juu ya misingi iliyowekwa kwa manufaa ya wote, yaani taifa linalojitegemea.
Wraka huo umeendelea kueleza kuwa bila msingi huo, mengine yote, hata kama yanaonekana yanang'aa, yatakuwa yanasaliti mustakabali wa kweli wa taifa letu.
"Tusijidanganye, bila msingi wa kujitegemea na kutafuta manufaa ya wote, taifa hili litaanguka. Kama halianguki leo, ni lazima kesho litaanguka. Tunajiuliza, uko wapi ujasiri wa taifa letu? Imepotelea wapi fahari ya kujitawala, si kisiasa tu, bali kiuchumi, kifikira na kijamii?" unahoji waraka huo.
Waraka huo wenye sura tatu unaendelea kuhoji ilipotelea wapi mbegu ya uzalendo iliyopandwa na waasisi wa taifa, heshima ya kuthamini utu, kuheshimu imani ya asiyeamini kile ‘nisichokiamini' na kutafuta ufumbuzi halisi wa matatizo yanayotukabili?
"Tumepoteza dira ya kujitegemea kiuamuzi na kimkakati. Tumefikia mahali pa kuamini kwamba maendeleo yataletwa kwa kaulimbiu zinazobadilika badilika kila siku.
Katika mazingira ya sasa, watu wachache, kwa sababu binafsi na kwa manufaa binafsi wanapotosha ukweli na kutafuta njia za kulinda masilahi yao kwa kutumia mifumo isiyokubalika, lakini inayosimikwa na kuhalalishwa ili kulinda masilahi binafsi," unaeleza waraka huo.
Waraka huo uliotiwa saini na maaskofu wa Kanisa Katoliki wa majimbo yote nchini umekemea matumizi mabaya ya madaraka, mikataba mibovu, kupindisha sheria, kufumbia macho uhalifu na kusema uhuru wa kweli haujengeki katika misingi dhaifu ya ubinafsi na haulengi kumfanya mtu yeyote yule awe juu ya sheria za haki na taratibu za uadilifu.
Kimsingi, hakuna maendeleo ya kweli kama watu hawaheshimu haki ya msingi ya kuujua ukweli na kuishi kadiri ya ukweli huo.
Waraka huo umeeleza kuwa katika mazingira kama hayo Kanisa Katoliki haliwezi kukaa pembeni na kutazama kwa kuwa linao wajibu wa kuijenga jamii.
"Kanisa lina wajibu wa kuangalia, kuboresha na kuikosoa mienendo ya kijamii na kisiasa inayohatarisha ustawi wa jamii nzima na hivyo kuathiri kazi ya Kristo ya kumkomboa mwanadamu na kuusimika Ufalme wa Mungu," unaeleza.
Pia, unaendelea kueleza waraka huo kuwa kanisa hilo litaendelea kusisitiza ukweli ili kuunda maisha ya kisiasa yaliyo kweli ya kibinadamu, kwa maelezo kuwa hakuna lililo bora zaidi kuliko kustawisha ndani ya watu hisia za haki, upendo na huduma kwa manufaa ya wote.
Uvunjifu wa amani
Wanaeleza maaskofu hao kuwa mambo yanayolivuruga taifa na kusababisha lizidi kupoteza tunu bora ya amani iliyoachwa na waasisi wa taifa kuwa ni matukio ya uvunjifu wa amani yakiwemo mauaji, watu kumwagiwa tindikali kwa sababu ya imani yao au visasi.
"Amani lazima ilindwe ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu….Amani siyo tunu inayojitegemea peke yake kwa kuwa amani ya kweli inazaliwa ndani ya mioyo yenye kujali misingi ya utu, haki, heshima, ukweli na umoja. Fikra tofauti na hizo, huzaa mioyo potofu na mioyo potofu haiwezi kutoa amani," walisema.
Kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya, hayo yamegeuka kuwa wimbo unaochosha kwa sababu hakuna dhamira ya dhati ya kuitokomeza.
"Uongozi wa juu unapotamka hadharani kuwafahamu watoa rushwa, wapokea rushwa na wafanyabiashara wa madawa ya kulevya lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa ni hali inayotisha sana….Wakati umefika ambapo lazima tuwe wakweli kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na madawa ya kulevya," wanaeleza viongozi hao.
Waraka huo unasema pia kuwa taifa haliwezi kuwa huru kuhusu rushwa na dawa za kulevya kama watu hawajawa wakweli kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya.
Wanasema taifa halina budi kuunda misingi imara ya utawala bora huku kila mmoja akikumbuka kuwa utawala bora bila uwajibikaji na kuwajibishana ni kiini macho.
"Wanaopiga vita rushwa majukwaani, ndiyo wanaoomba na kupokea nje ya jukwaa. Isitoshe, rushwa ndiyo ngazi waliyoitumia na wanayoitumia kufika jukwaani…Katika mazingira kama haya hatujengi taifa bali tunalibomoa na historia itatuhukumu.
Kukua kwa matabaka katika jamii
Wanaeleza maaskofu hao kuwa kuwepo kwa tofauti kubwa za kiuchumi ambazo walisema zinapanua utengano wa kimatabaka kati ya wenye nguvu za kiuchumi na wasio na kitu.
"Wenye nguvu kiuchumi sasa wanamiliki uchumi, wanamiliki siasa na hatima ya fukara, na kwa fedha wananunua haki ya wanyonge… Mgawanyo mbovu wa rasilimali za nchi unatisha. Ardhi inamilikiwa na wachache kwa kivuli cha uwekezaji mkubwa huku wananchi wakiahidiwa ajira kwa kuwa vibarua kwenye mashamba hayo badala ya kuwezeshwa kumiliki ardhi na kuitumia kwa faida."
Waraka huo unasema lipo tatizo la siasa kuingilia weledi mambo waliyosema yanatia hofu mtu yeyote anayejali na kuthamini mustakabali wa taifa la Tanzania.
Wanaelezea athari za siasa kutawala mifumo ya ujenzi wa misingi ya maendeleo na kuelezwa kuchoshwa na kuwapo kwa maneno mengi na mipango ya zimamoto isiyofanyiwa utafiti wa kina.
"Kwa mfano, siasa na wanasiasa wanaathiri mfumo wa utoaji wa elimu nchini kiasi cha kulifanya taifa hili kuwa kama taifa lisilojali mustakabali wake…Uthabiti katika kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo hauonekani na badala yake porojo zimetawala," unaeleza waraka huo.
Waraka huo umekemea wale waliopewa dhamana ya kusimamia masuala ya elimu kukosa unyenyekevu wa kuwasikiliza na kushauriana na wataalamu na badala yake zinaibuka sera ambazo msingi wake ni ubunifu usiozingatia weledi na kusababisha elimu kudidimia.
Mchakato wa Katiba Mpya
Waraka huo pia unaelezea mchakato wa Katiba Mpya na kusema kama moyo wa taifa katiba ni chombo kinachopaswa kutengeneza misingi ya mfumo wa maisha mazima na uhai wa taifa.
"Ukweli wote na uhuru wote wa taifa unabebwa na katiba. Tunarudia tena kutamka kuwa zoezi hili adhimu na la muhimu kwa mustakabali wa taifa limeharakishwa mno. Sasa tunaona zoezi zima limehodhiwa na wanasiasa," wamesema viongozi hao wa dini.
Wanasema katiba si mali ya wanasiasa, bali ni mali ya wananchi na kutaka hekima iongoze katika kulinda umoja wa taifa na uepushe na kishawishi cha kubaguana na kutengana.
"Kwa kuzingatia hilo umoja huo utatuongoza katika njia ya amani," wanamalizia.
Source: Mwananchi
Ujumbe huo wenye kaulimbiu ‘Ukweli utawaweka huru', umeeleza wajibu wa kuishi ndani ya ukweli, kuulinda na kuusimamia ukweli pamoja na umuhimu wa Watanzania kujenga jamii yenye utu, haki, amani, upendo na mshikamano wa kweli.
"Wapendwa Taifa la Mungu, tunapoanza safari ya Kwaresma (kipindi cha kukumbuka mateso ya Yesu) ya mwaka huu, sisi maaskofu wenu tungependa kuwakumbusha ninyi na watu wote wenye mapenzi mema kuhusu umuhimu wa kuishi katika ukweli. Kuuishi ukweli na kuishi maisha yaliyojengwa juu ya msingi wa ukweli ni kushiriki hasa maisha ya Mungu... Pasipo ukweli, jamii itasambaratika kwa sababu itakuwa imejengwa bila msingi."
Hali halisi ya taifa letu
Waraka huo umeeleza miaka zaidi ya 50 ya uhuru wa Tanzania na kusema kuwa ni taifa lililovuka uchanga na lililo katika umri wa kujengwa juu ya misingi iliyowekwa kwa manufaa ya wote, yaani taifa linalojitegemea.
Wraka huo umeendelea kueleza kuwa bila msingi huo, mengine yote, hata kama yanaonekana yanang'aa, yatakuwa yanasaliti mustakabali wa kweli wa taifa letu.
"Tusijidanganye, bila msingi wa kujitegemea na kutafuta manufaa ya wote, taifa hili litaanguka. Kama halianguki leo, ni lazima kesho litaanguka. Tunajiuliza, uko wapi ujasiri wa taifa letu? Imepotelea wapi fahari ya kujitawala, si kisiasa tu, bali kiuchumi, kifikira na kijamii?" unahoji waraka huo.
Waraka huo wenye sura tatu unaendelea kuhoji ilipotelea wapi mbegu ya uzalendo iliyopandwa na waasisi wa taifa, heshima ya kuthamini utu, kuheshimu imani ya asiyeamini kile ‘nisichokiamini' na kutafuta ufumbuzi halisi wa matatizo yanayotukabili?
"Tumepoteza dira ya kujitegemea kiuamuzi na kimkakati. Tumefikia mahali pa kuamini kwamba maendeleo yataletwa kwa kaulimbiu zinazobadilika badilika kila siku.
Katika mazingira ya sasa, watu wachache, kwa sababu binafsi na kwa manufaa binafsi wanapotosha ukweli na kutafuta njia za kulinda masilahi yao kwa kutumia mifumo isiyokubalika, lakini inayosimikwa na kuhalalishwa ili kulinda masilahi binafsi," unaeleza waraka huo.
Waraka huo uliotiwa saini na maaskofu wa Kanisa Katoliki wa majimbo yote nchini umekemea matumizi mabaya ya madaraka, mikataba mibovu, kupindisha sheria, kufumbia macho uhalifu na kusema uhuru wa kweli haujengeki katika misingi dhaifu ya ubinafsi na haulengi kumfanya mtu yeyote yule awe juu ya sheria za haki na taratibu za uadilifu.
Kimsingi, hakuna maendeleo ya kweli kama watu hawaheshimu haki ya msingi ya kuujua ukweli na kuishi kadiri ya ukweli huo.
Waraka huo umeeleza kuwa katika mazingira kama hayo Kanisa Katoliki haliwezi kukaa pembeni na kutazama kwa kuwa linao wajibu wa kuijenga jamii.
"Kanisa lina wajibu wa kuangalia, kuboresha na kuikosoa mienendo ya kijamii na kisiasa inayohatarisha ustawi wa jamii nzima na hivyo kuathiri kazi ya Kristo ya kumkomboa mwanadamu na kuusimika Ufalme wa Mungu," unaeleza.
Pia, unaendelea kueleza waraka huo kuwa kanisa hilo litaendelea kusisitiza ukweli ili kuunda maisha ya kisiasa yaliyo kweli ya kibinadamu, kwa maelezo kuwa hakuna lililo bora zaidi kuliko kustawisha ndani ya watu hisia za haki, upendo na huduma kwa manufaa ya wote.
Uvunjifu wa amani
Wanaeleza maaskofu hao kuwa mambo yanayolivuruga taifa na kusababisha lizidi kupoteza tunu bora ya amani iliyoachwa na waasisi wa taifa kuwa ni matukio ya uvunjifu wa amani yakiwemo mauaji, watu kumwagiwa tindikali kwa sababu ya imani yao au visasi.
"Amani lazima ilindwe ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu….Amani siyo tunu inayojitegemea peke yake kwa kuwa amani ya kweli inazaliwa ndani ya mioyo yenye kujali misingi ya utu, haki, heshima, ukweli na umoja. Fikra tofauti na hizo, huzaa mioyo potofu na mioyo potofu haiwezi kutoa amani," walisema.
Kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya, hayo yamegeuka kuwa wimbo unaochosha kwa sababu hakuna dhamira ya dhati ya kuitokomeza.
"Uongozi wa juu unapotamka hadharani kuwafahamu watoa rushwa, wapokea rushwa na wafanyabiashara wa madawa ya kulevya lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa ni hali inayotisha sana….Wakati umefika ambapo lazima tuwe wakweli kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na madawa ya kulevya," wanaeleza viongozi hao.
Waraka huo unasema pia kuwa taifa haliwezi kuwa huru kuhusu rushwa na dawa za kulevya kama watu hawajawa wakweli kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na dawa za kulevya.
Wanasema taifa halina budi kuunda misingi imara ya utawala bora huku kila mmoja akikumbuka kuwa utawala bora bila uwajibikaji na kuwajibishana ni kiini macho.
"Wanaopiga vita rushwa majukwaani, ndiyo wanaoomba na kupokea nje ya jukwaa. Isitoshe, rushwa ndiyo ngazi waliyoitumia na wanayoitumia kufika jukwaani…Katika mazingira kama haya hatujengi taifa bali tunalibomoa na historia itatuhukumu.
Kukua kwa matabaka katika jamii
Wanaeleza maaskofu hao kuwa kuwepo kwa tofauti kubwa za kiuchumi ambazo walisema zinapanua utengano wa kimatabaka kati ya wenye nguvu za kiuchumi na wasio na kitu.
"Wenye nguvu kiuchumi sasa wanamiliki uchumi, wanamiliki siasa na hatima ya fukara, na kwa fedha wananunua haki ya wanyonge… Mgawanyo mbovu wa rasilimali za nchi unatisha. Ardhi inamilikiwa na wachache kwa kivuli cha uwekezaji mkubwa huku wananchi wakiahidiwa ajira kwa kuwa vibarua kwenye mashamba hayo badala ya kuwezeshwa kumiliki ardhi na kuitumia kwa faida."
Waraka huo unasema lipo tatizo la siasa kuingilia weledi mambo waliyosema yanatia hofu mtu yeyote anayejali na kuthamini mustakabali wa taifa la Tanzania.
Wanaelezea athari za siasa kutawala mifumo ya ujenzi wa misingi ya maendeleo na kuelezwa kuchoshwa na kuwapo kwa maneno mengi na mipango ya zimamoto isiyofanyiwa utafiti wa kina.
"Kwa mfano, siasa na wanasiasa wanaathiri mfumo wa utoaji wa elimu nchini kiasi cha kulifanya taifa hili kuwa kama taifa lisilojali mustakabali wake…Uthabiti katika kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo hauonekani na badala yake porojo zimetawala," unaeleza waraka huo.
Waraka huo umekemea wale waliopewa dhamana ya kusimamia masuala ya elimu kukosa unyenyekevu wa kuwasikiliza na kushauriana na wataalamu na badala yake zinaibuka sera ambazo msingi wake ni ubunifu usiozingatia weledi na kusababisha elimu kudidimia.
Mchakato wa Katiba Mpya
Waraka huo pia unaelezea mchakato wa Katiba Mpya na kusema kama moyo wa taifa katiba ni chombo kinachopaswa kutengeneza misingi ya mfumo wa maisha mazima na uhai wa taifa.
"Ukweli wote na uhuru wote wa taifa unabebwa na katiba. Tunarudia tena kutamka kuwa zoezi hili adhimu na la muhimu kwa mustakabali wa taifa limeharakishwa mno. Sasa tunaona zoezi zima limehodhiwa na wanasiasa," wamesema viongozi hao wa dini.
Wanasema katiba si mali ya wanasiasa, bali ni mali ya wananchi na kutaka hekima iongoze katika kulinda umoja wa taifa na uepushe na kishawishi cha kubaguana na kutengana.
"Kwa kuzingatia hilo umoja huo utatuongoza katika njia ya amani," wanamalizia.
Source: Mwananchi