Ujumbe maalumu kwa wazazi

Ujumbe maalumu kwa wazazi

maji ya gundu

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2018
Posts
3,120
Reaction score
4,850
Nianze kwa kusema asanteni wazee wetu kwa kutulea na kutukuza kwene misingi mema

Ila leo kuna kitu naomba kuwakumbusha au kuwaambia huenda kitasaidia kuwaondoa migogoro na sie watoto wenu

Suala la mzazi kumlea mtoto ni la lazima yaani ni jukumu lake maana yeye ndio alie mtafuta kwa nguvu zote

Ila wazazi mnapotulea na kutusomesha msitegemee na sisi tutakuja kuwasaidia kwa asilimia kubwa maana kipindi ambacho nyie mtakua mnazeeka na sie ndo kipindi chentu cha kuandaa future yetu koo inabidi tuwe makini tusije wekeza nguvu kubwa kwene kuwasaidia ninyi kuliko kuangalia yanayotukabiri

Narudia suala la mzazi kumlea mtoto ni la lazima, ila suala la mtoto kumsaidia mzazi ni la hiari inategemeana na kipato alichonacho koo wazazi msituhukumu kwa mambo kama hayo

Kivyangu huwa siamini kana kwamba eti kuna wazee ujana wao walibweteka huku wakitegemea wanawe waje wawa saidie si kweli
 
Mzazi yupi kakuvuruga mkuu???😄😄

Anyway...agreed. Mzazi ana JUKUMU la kumlea mtoto ila sio JUKUMU la mtoto kumlea mzazi.
 
Ndio maana wazazi wengi hupenda watoto wa kike, watoto wa kike wengi wao hujali sana wazazi.. Ulichokieleza ni mitazamo na matendo mengi ya sisi wanaume kwa wazazi wetu.
 
familia nyingi za kiafrika wazazi wetu utasikia, nazaa watoto wengi ilibwanisaidie badae...

utasikia tena "unazaa watoto wawili tu, mungu anaangalia hapo nawe unaangalia hapo, ongeza angalau wawe watano"
 
Wewe unafuga mbuzi au kuku wakupatie maziwa na mayai...na wazazi wanakufuga wewe uje uwapatie mkate
 
Back
Top Bottom