Ujumbe kwa wanaume

Hilo la wanawake kubadilika kwenye ndoa na kuwa tofauti na kwenye uchumba mmelitaka wenyewe wanaume kwa sababu wanawake ambao wamefikisha miaka 30 au zaidi na hawajaolewa mnawaperceive vibaya tofauti na wanaume wenye miaka 30 na kuendelea na hawajaoa na hakuna binadamu anayependa jamii imfikirie vibaya

Hivyo hii inapelekea wanawake kutaka ndoa sana kuliko wanaume kwahiyo wakipata wachumba wanajaribu kufanya kila kitu ambacho wanaume wanataka ili tu hao wanaume wawaoe sasa wakishaolewa si tayari azma yao ya kuolewa imetimia kwanini waendelee tena kujituma kama kwenye uchumba wakati walichokihitaji wameshakipata?
 
What? Kinachosababisha tuoe ni tamaa. Kasome kitabu cha wakorinto pale Paulo anasema mngeweza mngekuwa kama mimi ila kwa sababu tamaa zenu yawafaa muwe na Mwanamke.

Kutokana na hayo, tunaoa kwa sababu ya tamaa.
 
Mwanamke ukiwa kwenye ndoa angalia unatimiziwa mahitaji yako. Wajibu Wa Mme ni kuhakikishia familia, kula, kuvaa, watoto wanaenda shule na mambo mengine. Ukitaka kujua mmeo anamicjepuko mingap mtafariki Wa bp kila Siku.
Wanaume tuna huruma sana, huko nje kuna wanawake wenzenu tukiwaacha wataadhirika, so tunajitahidi kuwaweka Sawa na Kwa Mungu tuna thawabu.
 
Ni kweli unachosema mkuu,kwa kuliona hilo mke na watoto ndio wenye maamuzi katika vitu ninavyomiliki
 
Well spoken.

Hapo sasa ndipo cheating huanzia ili mtu apate kile alichokuwa anapewa ila leo hii hakipati.
 
Wanaume ni wanaume tuu, hata awe na wake 4 bado lazima tutamani mizigo mupyaaa, so pole Sana
 
Una lako jambo wanawake bil 5.6 wanaume bil 2.2 wengine nani atawapiga mswaki mwanaume wa kuenziwa. Hakuna ati mjinga Mungu ndy kafanya iwe hivyo furahi tu wewe hupendi wenzako wapate huduma?
Kwani ni wapi Mungu aliposema wanaume muwe na wanawake wengi kwa sababu wanawake ndo wapo wengi kuliko wanaume duniani yeye kataka iwe hivyo ana sababu zake ila hajawaambia kwamba ndiyo sababu ya wanaume kusaliti wake zao kuoa mke zaidi ya mmoja ni sawa unasema kwamba kwa sababu Mungu kaiotesha bangi basi ndo ameruhusu tutumie hata kama hajasema si ndiyo?

Halafu kumbuka siyo kila mtu hapa duniani alikuja kutimiziwa haja zake zote kama Mungu angetaka kila mtu atimiziwe haja zake zote basi kusingekuwa na watu masikini angemfanya kila mtu awe tajiri maana hakuna asiyependa kuishi maisha mazuri ila ndo hivyo ili dunia ibalance lazima kuwe na waliopata na waliokosa, waliooa/walioolewa na wasiooa/wasioolewa, masikini na tajiri, warefu na wafupi, wanene na wembamba, wazuri na wabaya n.k keep that in your mind
 
Huu ujumbe ulimuambia mume,?? Usije ukawa unafundisha wanaume za watu alafu wakwako bado bila bila
 
What? Kinachosababisha tuoe ni tamaa. Kasome kitabu cha wakorinto pale Paulo anasema mngeweza mngekuwa kama mimi ila kwa sababu tamaa zenu yawafaa muwe na Mwanamke.

Kutokana na hayo, tunaoa kwa sababu ya tamaa.
Nakazia hapo kwenye uwe na mwanamke na siyo wanawake basi kumbe hizo tamaa zenu zina uwezo wa kumalizwa na mwanamke mmoja tu wengine wote mnaochepuka kwa kisingizio cha kuwa wake zenu wanashindwa kuhimili mahitaji yenu mnajiendekeza tu

Maana siku ambazo mwanamke anakuwa hayuko kwenye hali ya kufanya zinavumilika sana tu sababu hakuna madhara makubwa mnayopata mfano ugonjwa au kifo hakuna ingekuwa mnapata madhara makubwa kama hayo basi tungewaelewa ila hamuumwi wala hamfi
 
Mkuu siyo kila binadamu alikuja duniani kutimiziwa mahitaji yake yote kama ingekuwa Mungu anataka kila binadamu atimiziwe mahitaji yake yote basi kusingekuwa na watu masikini wote angewafanya matajiri

Ili kila mtu awe na maisha mazuri maana hakuna anayependa kuishi maisha mabaya ila ndo hivyo ili dunia ibalance lazima kuwepo na waliopata na waliokosa kwahiyo msitumie dhambi zenu wanadamu kumsingizia Mungu kuwa karuhusu
 
Well spoken.

Hapo sasa ndipo cheating huanzia ili mtu apate kile alichokuwa anapewa ila leo hii hakipati.
Hapana solution siyo kucheat solution ni kuacha kuwapressurize wanawake kuolewa mapema kwa kuwadanganya kuwa eti kuna umri wakifika wanakuwa wameshachakaa hivyo hawawezi kuolewa wala kuzaa mkiacha hizo imani mtawafanya wanawake waingie kwenye ndoa kwa hiari yao wakiwa tayari kubeba majukumu ya mke na mama maana siyo kila mwanamke anakuwa atayari kubeba hayo majukumu kwenye umri ambao mnasema ndo anafaa kuolewa

Ila sasa hivi inaonyesha wanawake wengi wanaingia kwenye ndoa ili tu wafiche aibu ya kutokuolewa halafu pia wanaume msifanye ndoa ionekane kama mwenye mapungufu ni mwanamke tu kwani nyie hamna mapungufu yenu? Kwanini mwanamke tu ndo inaonekana kama mapungufu yake hayavumiliki na ni lazima apewe adhabu badala ya kukaa tu na kusuluhisha wenyewe?
 
Wanaume ni wanaume tuu, hata awe na wake 4 bado lazima tutamani mizigo mupyaaa, so pole Sana
Basi ndo muone kwamba kuoa wake 4 siyo solution ya nyie kuacha kuchepuka bali solution ni kuamua kutulia na mke 1 tu maana mwanaume aliyeamua kutulia mke 1 anamtosha ila mwanaume ambaye bado anataka kutembeza rungu hata aoe wanawake dunia nzima bado atamuomba Mungu amuumbie wengine kwahiyo msituchoshe na visingizio vyenu
 
Pia nanyi mnachangia sana wanaume kucheat.
Kwa sababu gani kwa sababu ya mapungufu yetu au kwani nyie hamna mapungufu yenu? Kwahiyo unataka kusema kuwa na nyie mnapokuwa na mapungufu yenu na sisi tuwacheat si ndiyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…