Ujue ukweli uliofichwa juu ya elimu ya nyota

Undava King

JF-Expert Member
Aug 11, 2017
3,205
5,332
Siku moja nikiwa usingizini ndipo maono yakaniijia kama ilivyokuwa kwa yohana wa ufunuo tofauti yake na mimi ikawa ndogo yeye alifunuliwa(aliambiwa maana ila mimi sikuambiwa maana zaidi ya kushuhudia),

Tazama nafsi ilikaribia mbingu mbele ya kiza kinene na tazama nilipofumbua macho yangu katika roho naliona mpangilio wa ajabu na kustaajabisha wa nyota mbalimbali

Tazama kulikuwako na mbingu mbili moja ni ile tuionayo kila siku lakini nyuma yake kulikuwako na ile mbingu ya pili na katika hii mbingu yakustaajabisha ipo tafsiri ya yale makundi ya nyota niliyoyaona katika mbingu ile ya kwanza yaani zile zodiac signs(constellations)

Kilichonishangaza zaidi nikuziona nyota zote jinsi zilivyo na michoro yake niliyoifahamu kupitia kwenye magazeti,vitabu n.k katika dunia hii tuishio zikiwa katika umbile la binadamu,wanyama, wadudu, mashujaa n.k

Nilikosa jibu kwanini iwe hivyo kule mbinguni? Na je ni nani huyo aliyeichora mbingu nakuinakshi kwa maumbo yenye rangi ya kupendeza na maumbile mbalimbali?

Pale pale nikasadiki kuwa Mungu yupo na ndie mchoraji,muhunzi na mratibishaji wa kila kilichopo pale kwa maana hata pamoja na uwezo waziada niliokuwa nao katika maono sikuweza kukaribia hata nukta ya umbali zilipo nyota zile nilizozishuhudia,

Ila swali lililonitesa hata baada ya kuzinduka nakutoka kwenye maono hayo ambayo siwezi kuelezea maajabu na siri chache nilizoshuhudia huko, nilijiuliza je ni wangap wameshayashuhudia yale niliyoyaona?

Na kama bado imekuaje michoro ile ile na maumbo yaleyale niliyoyashuhudia kwa macho yangu tuwe tukiyajua nakuyachora katika dunia yetu?

Tumeenda mbali zaidi na kuiba baadhi ya siri zilizoko kule kuhusiana na mahusiano yaliyopo kati ya nyota na maisha ya mwanadamu(kwa kutumia tarehe ya kuzaliwa)n.k

Je,mwanadamu amejua hivi vyote kupitia msaada wa viumbe visivyoonekana, ama kwa njia kama yangu au kuna siri kubwa ya uumbaji ambayo baadhi ya watu wanayo lakini wameifumba dunia kwa makusudi ya mazuri au mabaya? Au wenda mwanadamu angefunuliwa elimu hii angeweza kumjua vyema muumba wake nakumpa sifa au ingemletea dhahama ya uasi na kutenda maovu?

Naomba kushusha kalamu nakuishia hapa, yumkini sikulazimishi huyaamini haya niyanenayo ila imekupasa kutafakari kwa kina kwa nini wapo wasoma nyota toka zama za kale na walikuwa wakibashiri na vitu vinatokea kweli hata kabla ya kristo, Je, ni siri gani iliyofichika katika elimu hii?
 
"Kuna nyota inafanana na..." Mimi nitaanza na hapa, Mkuu unafikiri hizi nyota zinafanana na maumbo ya wanyama/vitu zinazoitwa kwa majina yake?

Kama ndio, basi mkuu naungana na comment ya kwanza juu.

Kama hapana mbona umeuliza swali la ajabu kwenye iyo aya?

Anyway tujifunze
 
"Kuna nyota inafanana na..." Mimi nitaanza na hapa, Mkuu unafikiri hizi nyota zinafanana na maumbo ya wanyama/vitu zinazoitwa kwa majina yake?

Kama ndio, basi mkuu naungana na comment ya kwanza juu.

Kama hapana mbona umeuliza swali la ajabu kwenye iyo aya?

Anyway tujifunze
Ndio ni kweli zinalandana, pitia status tena.
 
Kwanza ni kweli Kuna Nguvu mbili na zinafanya kazi yaani nuru na Giza Ila Nguvu zote hizi zipo kwenye ulimwengu wa kiroho sio ya mwili Sasa kupitia hapa huweza kupata maono na jua roho kamwe haifi Sasa inategemea na wew una Imani kiasi gani...
 
Siku moja nikiwa usingizini ndipo maono yakaniijia kama ilivyokuwa kwa yohana wa ufunuo tofauti yake na mimi ikawa ndogo yeye alifunuliwa(aliambiwa maana ila mimi sikuambiwa maana zaidi ya kushuhudia),

Tazama nafsi ilikaribia mbingu mbele ya kiza kinene na tazama nilipofumbua macho yangu katika roho naliona mpangilio wa ajabu na kustaajabisha wa nyota mbalimbali

Tazama kulikuwako na mbingu mbili moja ni ile tuionayo kila siku lakini nyuma yake kulikuwako na ile mbingu ya pili na katika hii mbingu yakustaajabisha ipo tafsiri ya yale makundi ya nyota niliyoyaona katika mbingu ile ya kwanza yaani zile zodiac signs(constellations)

Kilichonishangaza zaidi nikuziona nyota zote jinsi zilivyo na michoro yake niliyoifahamu kupitia kwenye magazeti,vitabu n.k katika dunia hii tuishio zikiwa katika umbile la binadamu,wanyama, wadudu, mashujaa n.k

Nilikosa jibu kwanini iwe hivyo kule mbinguni? Na je ni nani huyo aliyeichora mbingu nakuinakshi kwa maumbo yenye rangi ya kupendeza na maumbile mbalimbali?

Pale pale nikasadiki kuwa Mungu yupo na ndie mchoraji,muhunzi na mratibishaji wa kila kilichopo pale kwa maana hata pamoja na uwezo waziada niliokuwa nao katika maono sikuweza kukaribia hata nukta ya umbali zilipo nyota zile nilizozishuhudia,

Ila swali lililonitesa hata baada ya kuzinduka nakutoka kwenye maono hayo ambayo siwezi kuelezea maajabu na siri chache nilizoshuhudia huko, nilijiuliza je ni wangap wameshayashuhudia yale niliyoyaona?

Na kama bado imekuaje michoro ile ile na maumbo yaleyale niliyoyashuhudia kwa macho yangu tuwe tukiyajua nakuyachora katika dunia yetu?

Tumeenda mbali zaidi na kuiba baadhi ya siri zilizoko kule kuhusiana na mahusiano yaliyopo kati ya nyota na maisha ya mwanadamu(kwa kutumia tarehe ya kuzaliwa)n.k

Je,mwanadamu amejua hivi vyote kupitia msaada wa viumbe visivyoonekana, ama kwa njia kama yangu au kuna siri kubwa ya uumbaji ambayo baadhi ya watu wanayo lakini wameifumba dunia kwa makusudi ya mazuri au mabaya? Au wenda mwanadamu angefunuliwa elimu hii angeweza kumjua vyema muumba wake nakumpa sifa au ingemletea dhahama ya uasi na kutenda maovu?

Naomba kushusha kalamu nakuishia hapa, yumkini sikulazimishi huyaamini haya niyanenayo ila imekupasa kutafakari kwa kina kwa nini wapo wasoma nyota toka zama za kale na walikuwa wakibashiri na vitu vinatokea kweli hata kabla ya kristo, Je, ni siri gani iliyofichika katika elimu hii?
Mkuu,ilimu ya nyota ni sehemu ndogo sana ya ilimu ya ulimwengu.Katika ulimwengu kuna kitu tunaitwa oneness ambacho ndicho hicho ambacho una kiona katika ilimu ya nyota.Patern ya nyota angani ni moja kati ya patern nyingi ambazo zipo duniani.

Kuna patern za majina ya watu na location.patern za maneno fulani ambayo ukiyasikia yanakuwa yanaashiria jambo fulani kwa kiwango fulani.Ili kuelewa zaidi inakubidi uwe na utulivu wa akili.

Kwa mfano Patern ya muda wako wa kulala na routine inaweza kukufanya uwe mtu tofauti kitabia na hata kimaisha.Kuna mengi sana ambayo tukiyajua tunaweza shindwa hata kutembea barabarani.
 
Mkuu andoza mtizamo wangu unatofautiana na wewe kidogo kwa upande wangu naamini hii ni elimu kubwa mno ambayo haijafafanuliwa vyema kwa wanadamu wote kuielewa vizuri labda pengine ni ugumu wa kufanya tafiti zake nakuzithibitisha katika ulimwengu wa mwili au pengine nikutokana na uzito wa siri zilizomo ndani yake ambazo endapo zikianikwa italeta mtizamo mwingine(ambao hauna faida kwa minority or majority) juu ya imani na maisha yetu kiujumla ulimwenguni, mfano:-

Nyota(jua),sayari,mwezi uhusika katika imani karibia zote za kidini duniani kama ishara,asili ya nguvu, utukufu, uungu,n.k
Nitakupa mifano michache, anza na imani zinazohusisha tahajudi au nature zote utagundua ishara kadhaa za kinyota na mahusiano yake na wao kuanzia mikao yao,alama/nembo zao, imani yao juu ya miale na mwanga ama rangi n.k
Njoo katika imani za wana-ibrahimu zote(wakristo,waislamu na Judaism) utagundua ishara za jua,mwezi na nyota kila mahali katika ibada zao,mavazi yao,madhabahuni/mahekaluni kwao, matendo yao,nembo, na ndani ya maandiko yao,
Njoo katika imani za kipagani na kishetani au uchawi hapa utakutana na matumizi mbalimbali ya michoro ya nyota,mahesabu ya mikunjo yake na matumizi yake katika njia za giza, hapa utakutana na mapentagram na maoctagram n.k pia miungu yenye kuabudiwa utakutana na mabaali/babylon (mungu jua),miungu ya mwezi au sayari na alama mbalimbali za dini za kipagani ikiwemo za kishetani kama baphomet pia utumia alama za nyota n.k

Katika sayansi ya ubashiri/utabiri/astrolojia ambayo kwa asilimia kubwa ni sayansi ya kiimani zaidi(isiyoweza kuthibitishwa) kwa njia ya nyota pia utagundua siri mbalimbali kupitia hapa juu ya ujio wa binadamu katika sayari hii,siri za hatima/majaliwa yake, historia ya mbingu, miungu,siri ya kifo n.k

Katika sayansi yetu ya dunia(ya uthibitisho)utagundua kuwa elimu hii ilileta mapinduzi makubwa katika kufanikisha masomo ya hesabu,fizikia nakadhalika na vilevile sayansi imejitahidi kufafanua kwa uwazi juu ya nyota,sayari na mwezi na magimba mengine katika ulimwengu

japo bado tafiti zake zimebaki kuwa mtihani mzito ambao umejaa makisio na uthibitisho kiduchu ambapo endapo binadamu akifikia hapo (akifanikiwa kugundua/kujua)atajihesabu kuwa amefikia kiwango cha juu zaidi cha ufahamu katika kujielewa yeye na mazingira yake.

Hivyo ukiachilia mbali huo ufafanuzi wangu juu ya kwanini naona kama elimu hii ni pana zaidi, naomba uielezee kidogo pattern ya nyota kupitia ilimu ya ulimwengu jinsi inavyohusiana na huo upekee kwa faida ya wengi
Mkuu,ilimu ya nyota ni sehemu ndogo sana ya ilimu ya ulimwengu.Katika ulimwengu kuna kitu tunaitwa oneness ambacho ndicho hicho ambacho una kiona katika ilimu ya nyota.Patern ya nyota angani ni moja kati ya patern nyingi ambazo zipo duniani.

Kuna patern za majina ya watu na location.patern za maneno fulani ambayo ukiyasikia yanakuwa yanaashiria jambo fulani kwa kiwango fulani.Ili kuelewa zaidi inakubidi uwe na utulivu wa akili.

Kwa mfano Patern ya muda wako wa kulala na routine inaweza kukufanya uwe mtu tofauti kitabia na hata kimaisha.Kuna mengi sana ambayo tukiyajua tunaweza shindwa hata kutembea barabarani.
 
IMG-20201030-WA0019.jpg
 
Unajimu na dini: Dunia moja, Mungu mmoja, Majina mengi, Sura Nyingi:

Elimu ya unajimu ndio chanzo cha imani zote za kale: Misri, Babiloni, Ugiriki, Roman, Zoroastrian, Mithraism, druids, na miungu ya Norse.." Pia unajimu ndiyo kitovu(moyo) wa imani za Mayan, Aztec na Inca ndani ya amerika wakiabudu jua kama mungu mkuu(Sun the supreme God).

Hivyo haishangazi kukuta sayari kama moyo(egemeo) la imani za dini za kale zidumuzo leo: Judaism,Wakirsto,Waislam,Buddhism,Hinduism, na Tao.

Yahweh (Jehovah) na Allah, the merciful and the compassionate(Mwenyezi Mungu,wa msamaha na huruma), ni majina ya mungu ndani ya Judaism na Waislam,
Allah,'Mungu wa msamaha na huruma' ina tafsiri ya ujumuisho wa Sagittarian(mshale) na piscean(samaki) sifa za jupita na Sagittarian sephira au mwangaza mmoja(shining one)yake, huitwa hesed mercy.
Asili ya huruma ya samaki bado inatia shaka kidogo miongoni mwa wanajimu.

Tetragrammation sacred(tetragramatoni takatifu)maarufu, Yod-He-Vau-He, ambayo utamkwa jina Yahweh, inajumuisha herufi nne kutoka kwenye triad(utatu) ya juu ambayo ukaa kwenye ufalme wa jupita katika msamaha(mercy).

Hawa ni miungu yaani roho ya kimungu isiyoelezeka(indefinable divine spirit),hivyo isichanganywe na ile ya unajimu ya jupita ya kila siku.
Mundane(kawaida) inaweza mulika divine(kimungu) lakini kimungu ni ya oda ya juu tofauti.
Kabbalah(tamaduni) huwa wazi kabisa na viwango vya metafizikali vinavyopanda na mwishowe unapata uungu.Roho hizi zikipanda.

Sifa kuu 8 za miungu ya Hindu inafit (inaingiliana) na sifa kuu 8 za Saphiroth au Mwangaza mmoja wa mti wa uzima.

Haya ni maajabu yanayothibitisha ufanano kati ya stori za uzao wa Krishna na Ukiristo, Ganesh(Mungu wa mwanzo mpya,mafanikio na busara, muondoaji wa vikwazo/mikosi),kujitanua na mpole(beneficent) mungu tembo ambae uwakilisha roho ya kiuungu ya jupita huko India, utafsiriwa kama Bwana wa majeshi,moja ya majina yanayopendwa na jehovah.
Buddha dogmatically(uhaminisha) kukataa miungu yeyote ya nje bali tu iwe kwa vitendo. Tibetan buddhism wao utambua vipengele vinne vya unajimu yaani udongo, hewa,moto na maji, kama moyo wa imani yao.

Ushahidi dhahiri zaidi wa mila ya mti wa uzima zinaweza kuonekana katika taswira ya avaiokitesvara, Mungu wa huruma, ambacho uzalisha moyo wa safu ya mti.
Vipengele kadhaa katika historia ya Buddha zinakazia sana tamaduni ya mti, hasa paa(ascension) yake katika kilele cha mti wa bodhi hasa ikipata mwangaza.

Kilele au taji ya mti wa uzima, mng'ao mmoja wa Neptune ni taji pendwa la ufalme wa mabwana wa kipindi kilichopita cha Samaki, Kristu, Krishna na Buddha.

Pengine ushahidi thabiti wa ufahamu wa dunia nzima kuhusu mti wa uzima unaweza patikana katika far-flung(kutupwa mbali) zaidi na robo ya matarajio.

Gramu tatu (tri-grams)8 ya Tao ilianza kuwapo zaidi ya miaka 3000 na inatumiwa na watu wa mila, waganga, kwa ajili ya imani ambazo huwa na hekalu(temples) za wasaidizi(ancestors) zaidi kuliko miungu, japo Tao haitambui uwepo wa Umoja mkuu(supreme unity),Roho kuu(supreme spirit)au Mungu.

Gramu tatu 8 ni tamaduni iliyowekwa katika gurudumu ikiwakilisha pande 8 za uelekeo, katika mpangilio huu sifa za vipengele (elements) zao tofauti uelekeana kwa ukaribu na sifa za zodiaki ya sayari kuu zenye mwitikio(corresponding) na mpangilio wa nafasi zake katika mti. Uzazi sahihi wa kushangaza wa mti wa uzima.
 
Mti wa uzima katika Biblia:Kuishi milele(immortality) na Upatanisho(Reconciliation):

Unajimu na Kabbalah(tamaduni) ya utakatifu wa mti wa maisha inathibitisha busara ya mbingu na alama kama moyo wa agano jipya na pia katika agano la kale toka kitabu cha mwanzo mpaka ufunuo.

Nae Mwenyezi Mungu akasema.."tazama, asije chuma na matunda ya mti wa uzima na akala na akaishi daima,hivyo basi Mwenyezi Mungu akamtoa nje ya bustani ya edeni" Mwanzo 3:22.

Mistari ya kitabu cha mwanzo inabeba ahadi ya kuishi milele kwa wote wanaotambua asili ya roho ya mti, Nguvu ya roho ambazo katika zenyewe ndimo unajimu unapojiendesha nakuthibitisha asili ya roho zetu na roho isifikwe na mauti ambazo dini zote usherehekea kwa millennia nyingi, wakikana kifo.

Kwa wale 'wenye masikio ya kusikia' kama injili iliwekavyo. Kwa wale ambao hawaoni hekima wamepotea nawatakufa kila siku ya maisha yao, mpaka mwisho watakapo onja ule ukombozi wa mwisho.
Ufunuo 22"..kulikuwa na mti wa uzima wa uhai unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa"

Ufunuo unathibitisha katika terms zisizo na mashaka sifa za kinajimu za mti: Mavuno ya mwezi ya roho za mbinguni kumi na mbili za mti katika mzunguko wake wa kila mwezi wa zodiac.

Cha muhimu zaidi, mstari huu una unabii wa ufunuo wa mti wa uzima; mti wa uzima 'utatibu mataifa yote' ufunuo pia umeahidi 'siri ya Mungu itamalizwa' (ufunuo 10.7) tunapotambua ukweli mkuu nyuma ya dini zetu tofauti, mioyo yetu kwa pamoja nje ya rangi ya ngozi zetu, mataifa na imani zao watalakiana kila mmoja wao kama ndugu badala ya kugeuka kuwa maadui.Na tutatupilia mbali mahusiano yetu yasiyo na afya,yasiyo endelevu na yasiyo na furaha juu ya vitu.

Tunaona dini zikichochea vita na kujihusisha na siasa imefikia hadi kujihusisha na ugaidi, badala ya kuleta amani na maelewano. Hats hivyo haifanyi kuwepo na Mungu zaidi ya mmoja anayezidi sayari yetu ndogo au kwa Mungu mmoja anayezidi sayari yetu ndogo au kwa Mungu kuwa mkweli na mwingine kuwa mwongo, mtizamo/tunachukulia inaweza isizuhilike au kuwa muhimu katika kipindi cha kale, kama jadi na majimbo yalipambana vikali na ilituletea urithi chanya ya maoni tofauti mbalimbali ya siri ya Mungu isiyoeleweka.

Lakini historia ya imani zote ina geuzi (evolution) moja, daima ubadilika kukidhi nyakati na atutakiwi kuinvoke zama mpya za kondoo( Aquarius) kutambua nyakati zetu ambazo ziko katika mabadiliko ya kasi kuliko ilivyowahi kutokea kabla na altitude zetu za zamani zimeshabadilika na siyo endelevu tena.

Ufunuo wa chanzo kimoja cha mbinguni kwa imani zote, sura mbalimbali za Mungu mmoja,Siku moja zitawaleta watu wenye nia nzuri pamoja katika ufahamu wa juu ya nini roho ya kiuungu hasa inahitaji. Hiki ndicho ukweli ambacho kila mmoja wetu anakitaka,upendo ni ushuhuda wa kila moyo, roho ya kiuungu katika kila moyo, tukiweza kusikiliza.

Manabii na wahenga wameweka ubinadamu wa kawaida wa mwanadamu katikati ya ujumbe wao na kufundisha Mungu ni Upendo na Roho ya Upendo, ubinahadamu na kusamehana ndiyo roho ya uungu inayofanya kazi kwetu wanadamu.
Kufunuliwa kwa roho ni hakika ya maisha kama dhihirisho haya mafunzo siyo tu kuwa ni theolojia lakini inafungamana kabisa na metafizikia ya unajimu, maisha ya kiroho ambayo siye tumeibeba ndani mwetu.
Upendo wa dhati ni kiini cha baraka za jua, kifizikia na kimetafizikia, maisha yanatutesa mioyoni, katika vifungo, katika mioyo ya kila atom. Nim-quote Ananda Coormarasway" This is poetry, but none the less science"
 
Mti wa uzima katika Biblia:Kuishi milele(immortality) na Upatanisho(Reconciliation):

Unajimu na Kabbalah(tamaduni) ya utakatifu wa mti wa maisha inathibitisha busara ya mbingu na alama kama moyo wa agano jipya na pia katika agano la kale toka kitabu cha mwanzo mpaka ufunuo.

Nae Mwenyezi Mungu akasema.."tazama, asije chuma na matunda ya mti wa uzima na akala na akaishi daima,hivyo basi Mwenyezi Mungu akamtoa nje ya bustani ya edeni" Mwanzo 3:22.

Mistari ya kitabu cha mwanzo inabeba ahadi ya kuishi milele kwa wote wanaotambua asili ya roho ya mti, Nguvu ya roho ambazo katika zenyewe ndimo unajimu unapojiendesha nakuthibitisha asili ya roho zetu na roho isifikwe na mauti ambazo dini zote usherehekea kwa millennia nyingi, wakikana kifo.

Kwa wale 'wenye masikio ya kusikia' kama injili iliwekavyo. Kwa wale ambao hawaoni hekima wamepotea nawatakufa kila siku ya maisha yao, mpaka mwisho watakapo onja ule ukombozi wa mwisho.
Ufunuo 22"..kulikuwa na mti wa uzima wa uhai unaozaa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, yaani kila mwezi; na majani yake ni dawa ya kuwaponya watu wa mataifa"

Ufunuo unathibitisha katika terms zisizo na mashaka sifa za kinajimu za mti: Mavuno ya mwezi ya roho za mbinguni kumi na mbili za mti katika mzunguko wake wa kila mwezi wa zodiac.

Cha muhimu zaidi, mstari huu una unabii wa ufunuo wa mti wa uzima; mti wa uzima 'utatibu mataifa yote' ufunuo pia umeahidi 'siri ya Mungu itamalizwa' (ufunuo 10.7) tunapotambua ukweli mkuu nyuma ya dini zetu tofauti, mioyo yetu kwa pamoja nje ya rangi ya ngozi zetu, mataifa na imani zao watalakiana kila mmoja wao kama ndugu badala ya kugeuka kuwa maadui.Na tutatupilia mbali mahusiano yetu yasiyo na afya,yasiyo endelevu na yasiyo na furaha juu ya vitu.

Tunaona dini zikichochea vita na kujihusisha na siasa imefikia hadi kujihusisha na ugaidi, badala ya kuleta amani na maelewano. Hats hivyo haifanyi kuwepo na Mungu zaidi ya mmoja anayezidi sayari yetu ndogo au kwa Mungu mmoja anayezidi sayari yetu ndogo au kwa Mungu kuwa mkweli na mwingine kuwa mwongo, mtizamo/tunachukulia inaweza isizuhilike au kuwa muhimu katika kipindi cha kale, kama jadi na majimbo yalipambana vikali na ilituletea urithi chanya ya maoni tofauti mbalimbali ya siri ya Mungu isiyoeleweka.

Lakini historia ya imani zote ina geuzi (evolution) moja, daima ubadilika kukidhi nyakati na atutakiwi kuinvoke zama mpya za kondoo( Aquarius) kutambua nyakati zetu ambazo ziko katika mabadiliko ya kasi kuliko ilivyowahi kutokea kabla na altitude zetu za zamani zimeshabadilika na siyo endelevu tena.

Ufunuo wa chanzo kimoja cha mbinguni kwa imani zote, sura mbalimbali za Mungu mmoja,Siku moja zitawaleta watu wenye nia nzuri pamoja katika ufahamu wa juu ya nini roho ya kiuungu hasa inahitaji. Hiki ndicho ukweli ambacho kila mmoja wetu anakitaka,upendo ni ushuhuda wa kila moyo, roho ya kiuungu katika kila moyo, tukiweza kusikiliza.

Manabii na wahenga wameweka ubinadamu wa kawaida wa mwanadamu katikati ya ujumbe wao na kufundisha Mungu ni Upendo na Roho ya Upendo, ubinahadamu na kusamehana ndiyo roho ya uungu inayofanya kazi kwetu wanadamu.
Kufunuliwa kwa roho ni hakika ya maisha kama dhihirisho haya mafunzo siyo tu kuwa ni theolojia lakini inafungamana kabisa na metafizikia ya unajimu, maisha ya kiroho ambayo siye tumeibeba ndani mwetu.
Upendo wa dhati ni kiini cha baraka za jua, kifizikia na kimetafizikia, maisha yanatutesa mioyoni, katika vifungo, katika mioyo ya kila atom. Nim-quote Ananda Coormarasway" This is poetry, but none the less science"
Undava King naomba namba yako
Au nichek 0625352984
 
Unajimu ni Ushirikina tu wa shetani na majini wala mungu sio mungu

Mtu aliesoma Book of Enoch hashangai,
Ulifunuliwa na majini labda sio mungu
Hicho kitabu ulichosoma cha book of enoch nani kakithibitisha kuwa rejea ya vitabu viteule vya biblia? Pili nikuulize kama umesoma kwa upeo vipengele viwili vya unajimu nilivyoelezea mwishoni nakuvielewa, Tatu Ukisema kuwa unajimu ni ushirikina wakijini unapaswa kuthibitisha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom