Ujio wa sheykh Sudeys Tanzania

Ujio wa sheykh Sudeys Tanzania

Mimi ni Mkristo ila nitakuja (kama nisipozuiwa getini) kwani nipo free.

Shukraan.
 
Hujamalizia mkuu, Quran ni kitabu chenye ubabaishaji ambacho hakijitoshelezi ndomaana kikasema ukiwa na swali uje utuulize watu wa kitabu sasa nyie badala ya kuuliza mnalazimisha kuongozwa na kitabu cha majini
Quran imejitosheleza katika masuala yote ya msingi. Aidha, waislam wameamini yote, yaliyoteremshwa kwa Muhammad na kwa mitume waliokuwepo kabla yake kwani wote walikuja na kauli moja tu, "muabuduni Mwenyezi MUNGU na mtii yale mitume wanawafundisha". Hakuna mtume yoyote alikuja na ujumbe tofauti na huo, wala hakuna mtume aliyekuja na akasema "niabuduni mim", hilo ndio msingi wa Kitabu chochote Kilicho cha Mwenyezi MUNGU.
 
Sasa suala la nyama ya Nguruwe unalitoa wapi katika uzi huu? Au lengo ni kuharibu mada ya mtoa mada?

Na ujue sio mara yangu ya kwanza kuhudhuria mikutano ya kiislam na hata majuzi nilikuwa katika sherehe zenu huko Arusha na kula msosi wa ukweli tena nilikaribishwa kukaa katika meza na viongozi wa dini na walijua kbs mimi ni Mkristo.

Siwezi kula nguruwe hadharani kwani nitawaudhi Waumi'nin hivyo usijali mkuu

Wasiwasi wangu ni pale getini kuingia bila kanzu na barakashia kama wengine wengi, nahisi sintaruhusiwa.
Hakuna atakayekuzuia mkuu, Hakika hakuna.
 
Wasiwasi wangu ni pale getini kuingia bila kanzu na barakashia kama wengine wengi, nahisi sintaruhusiwa.
Mimi mwenyewe nimevaa bukta na niko uwanjani tokea salaa ya alfajiri,juu ya bukta nimejaladia msuli sarong kitu ya indonesia.
 
Kama inavyojulikana leo ndo kile kilele cha mashindano ya Qur'an ya kumi na sita chini ya waandaji wa taasisi ya Al-hekma foundation inayosimamiwa na Sheikh Nurdin Kishki.

Mashindano hayo yatahudhuriwa na Shkh mkuu wa msikiti wa makha na madina, Shkh Assudeis yakishirikisha washindani wa usomaji kutoka nchi zote za Africa.

Baadhi yetu tulitamani kuwepo lakini ndo hivyo nyudhuru za kimaisha zimetupata. Mliopo eneo la tukio fanyeni kutoa updates kupitia uzi huu.

Baraqa-llah fiikum !
 
tapatalk_1495817291809.jpeg
haya watayaweka lini?
 
Kwa niaba ya Taasisi ya Al-Hikma foundation tunatanguliza shukrani zetu za dhati kwa kujaa kwa wingi uwanjani na kuitikia wito kwa ajili ya MwenyeziMungu, pia tunawataka radhi watu wote walioshindwa kuingia kutokana na uwanja kujaa, haikuwa dhamira yetu. Mwisho kabisa tunamuomba Allahu Subhana wataala apate kutuongoa sote na aiepushe nchi yetu na kila aina ya mabalaa. Aamyin Aamyin Aamyin
 
Back
Top Bottom