Ujerumani yashangazwa kutoendelezwa Reli ya Kati

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Ujerumani yashangazwa kutoendelezwa Reli ya Kati

Na Mashaka Mgeta

Serikali ya ujerumani imesema ni aibu kwa Tanzania kuiacha reli ya kati inayoendeshwa na Shirika la Reli nchini (TRL) kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.

Ujerumani ni Taifa lililojenga reli ya kati wakati wa utawala wa kikoloni na kutoa msaada wa matengenezo yake nyakati tofauti.

Balozi wa Ujerumani nchini, Guido Herz, alisema hayo juzi katika mahojiano maalum na magazeti yanayochapishwa na The Guardian Limited, ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Alikuwa akizungumzia maandalizi ya adhimisho la miaka 20 tangu Ujerumani Mashariki na Ujerumani Magharibi zilipoungana rasmi Oktoba 1990 na kuruhusu kuvunjwa kwa Ukuta wa Berlin.

Herz alisema hali ya reli hiyo hivi sasa inasikitisha licha ya kuwa katika mazingira bora ya kibiashara kwa kuhudumia abiria na mizigo upande wa Tanzania na nchi jirani.

Amesema Ujerumani haiwezi kutoa msaada wa kuikarabati reli ya kati, inayosimamiwa na Kampuni ya Reli nchini (TRL).

“Hatupo tayari kuisaidia reli ya kati hata kama serikali serikali ya Tanzania itatuomba kufanya hivyo, kwa sababu reli kwa sasa haifanyi kazi,” alisema.

Herz alisema kama pangekuwa na utawala mzuri, utoaji wea huduma wa reli hiyo usingeibua mazingira yaliyosababisha ishindwe kufanya kazi.

Alisema reli ya kati ni miongoni mwa fursa kubwa za kiuchumi nchini, na akaonyesha mshangao wake kwa nini serikali imeshindwa kuifufua na kuiboresha ili ifanye kazi kwa ufanisi……..

Habari zaidi katika Nipashe leo Ukurasa wa 3.


My take:

1. Kwenye red: Balozi anajua ni ufiisadi tu uiliokithiri ndani ya CCM, ila hakutaka tu kumuumbua JK wakati huu. Dr Slaa akifika Tabora na Kigoma aliongelee sana sana hili, hadi masikio ya mashabiki wa JK yapasuke.

2. Ingekuwa ndiyo Dr Slaa kayasema haya, Kinana angejibu kwamba anatafuta umaarufu. Siyo kweli Kinana?
 
Tumechoka bwana hakuna kitu kinachoenda vizuri mpaka saizi duuuu!
 
hii reli ya kati will always haunt us,sisi watanzania,hii ni backbone ya nchi imetushinda sasa what else tutaweza?
 
jibu analo Muungwana, "HATA SIJUHI KWA NINI TANZANIA NI MASIKINI"
 
JK hana uchungu kabisa na nchi hii, its so sad yaani hadi watu wa nje wanatuona sisi sote hatuko organised - kwa sababu tu ya utawala mbovu usio na uzalendo. Kama huimarishi miundombinu unajenga uchumi gani? wa kimatonya?

Wakuu tumshangaze huyu mtu na CCM yake 31st October, imetosha apumzike hatufai - anakaribia kutumwaga shimoni.
 
Yaani ukija kwenye reli ya kati unaweza kulia!!!

JK sijua anafiria nini? Huu uchumi siju ni uchumi gani tunaoongelea!!!

CCM & its government sucks!!
 
Lakini na hawa wawakilishi wa nchi za "wafadhili" pamoja na serikali zao ni wanafiki tu. Wanazo data kamili za kila kinachoendelea nchini lakini hawako tayari kukosana na serikali kwa kuchukua moral high ground hasa pale pesa zao zinapotumika ama kifisadi au ku-justify uhalali wa uozo unaoendelea serikalini. Wanapotoa kauli kama hizi wengine tunaanza kujiuliza kuna nini hapa. Ni vigumu kuamini kama huyo mheshimiwa balozi kweli "anashangaa" hali ya reli ya kati. Ni kama tulivyopewa tuzo ya MDG kwa "kuandikisha" watoto wengi shuleni bila kugusiwa kuhusu uozo wa mfumo mzima wa elimu nchini. Namna hii jumuiya ya kimataifa haitusaidii kuwa makini katika mambo yetu. Hivyo akitokea mtu kutoa critique ya nguvu hivyo inakuwa kama unafiki tu.
 
Nchi imepoteza mwelekeo big time! hata ktk kampeni zake huyu msanii sijui anawaambia nini wananchi, na chochote anachowaambia hivi hao wana CCM wananchi wanatarajia kumpigia kula huyu jamaa kweli! ama kweli tumerogwa. Hivi mtu na akili yake aliyojaaliwa na mungu na wazazi wake kweli atadiriki kupigia kula CCM! Wht the Hell!!:A S 13:
 
Lakini na hawa wawakilishi wa nchi za "wafadhili" pamoja na serikali zao ni wanafiki tu. Wanazo data kamili za kila kinachoendelea nchini lakini hawako tayari kukosana na serikali kwa kuchukua moral high ground hasa pale pesa zao zinapotumika ama kifisadi au ku-justify uhalali wa uozo unaoendelea serikalini. Wanapotoa kauli kama hizi wengine tunaanza kujiuliza kuna nini hapa. Ni vigumu kuamini kama huyo mheshimiwa balozi kweli "anashangaa" hali ya reli ya kati. Ni kama tulivyopewa tuzo ya MDG kwa "kuandikisha" watoto wengi shuleni bila kugusiwa kuhusu uozo wa mfumo mzima wa elimu nchini. Namna hii jumuiya ya kimataifa haitusaidii kuwa makini katika mambo yetu. Hivyo akitokea mtu kutoa critique ya nguvu hivyo inakuwa kama unafiki tu.

Nakubaliana kabisa na ulichoandika. Kama kweli hawa wafadhili hawaridhiki na hali ya maendeleo Tanzania pamoja na kutoa 40% ya bajeti kila mwaka basi wasimamishe haraka utoaji huo wa mapesa chungu nzima hapo ndiyo tutawaona kwamba si wanafiki. Vinginevyo kulalamika kila mwaka kwamba hawaridhiki na hali ya maendeleo Tanzania na kisha kutoa mabilioni ya fedha ni unafiki maana wanajua wazi nyingi zinaishia kwa mafisadi gharama za juu ambazo hazina maana katika kuendesha Serikali.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom