Mkuu Ghorofa sio sana Tofali, Tofali ni nyama za kujazia tu, bali ghorofa ni ZEGE, (Nondo, Cement /Mchanga/Kokoto(ratio nzuri) ), Ningekushauri umtafute mtaalamu wa Soil kwanza aangalie hilo eneo lako (aina ya udongo, mfinyanzi, mchanga nk) na pia aangalie hilo eneo ni kavu ama ni eneo yowevu, ukishapata hayo majibu mtafute mtaalamu wa ujenzi akushauri utumie Nondo za milimeter ngapi kwenye Msingi, Colum na jamvi lenyewe,
badala ya kuvyetua tofali ningekushauri uanze kukusanya Nondo, kokoto, Mchanga na weka pesa ya cement, Tofali wala sio kitu cha kuumiza kichwa kama unajenga ghorofa